Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kwahiyo kwa logic hii ni kwamba;

Crystal Palace alimfunga man. Chelsea akadraw na man so Crystal alitakiwa atoe suluhu au aifunge chelsea...

Leicester kamfunga city tano. Liva kasuluhu na city so leicester akikutana na liva ni atamfunga au atasuluhu naye...

Logic ngumu hii

Not likely hasa draw zinapokuwa involved.

BTW hii point iko kiushabiki zaidi, isituchukulie muda sana kujadili.

Ila jana kwa jinsi Aston Villa nilivyowaona, maombi yangu ya wao kushuka daraja sioni yakifanikiwa.
 
Hahaha kiukweli nimecheka mpaka watu wananishangaa.

Ndo uelewe kwamba haya majukwaa ni yetu sote, na kitu kinacho tukutanisha zaidi kama ndugu ni msiba.

Nisipokuja msibani kwako utanilaumu na unaweza kukata hata undugu.

Sema hapa kwenye hii familia misiba minne ndani ya mechi nane ni misiba mingi sana, ndiyo maana wenyewe mnalalamika kwa kuona eti tunakula sana msibani.

Tunawaahidi kwamba misiba ijayo tutakuja na vyakula vyetu.
 
Not likely hasa draw zinapokuwa involved.

BTW hii point iko kiushabiki zaidi, isituchukulie muda sana kujadili.

Ila jana kwa jinsi Aston Villa nilivyowaona, maombi yangu ya wao kushuka daraja sioni yakifanikiwa.
Kiukweli maombi yako hamishia kutaka wawe nje ya top six.

Au Grealish, Barkley na Watson waumie kwa miezi minne.
 
Ndo uelewe kwamba haya majukwaa ni yetu sote, na kitu kinacho tukutanisha zaidi kama ndugu ni msiba.

Nisipokuja msibani kwako utanilaumu na unaweza kukata hata undugu.

Sema hapa kwenye hii familia misiba minne ndani ya mechi nane ni misiba mingi sana, ndiyo maana wenyewe mnalalamika kwa kuona eti tunakula sana msibani.

Tunawaahidi kwamba misiba ijayo tutakuja na vyakula vyetu.
Ngoja. Tutajitahidi kupunguza vifo.
 
Mkuu kwenye kukosa nafasi siwezi kuwalaumu wachezaji wetu moja kwa moja.

Ukitaka kufunga ni lazima kama timu utengeneze nafasi za kutosha, pitia stats za Liver na City kuanzia msimu uliopita utaona wanapiga jumla ya shots hadi 20+ wanashinda 2 au 3. Tafsiri inayokuja kichwani ni kwamba unahitaji kutengeneza nafasi nyingi sana ili kuongeza chances za kufunga magoli.

Tatizo jingine ni namna kocha anavyo mtumia Willian, sijaelewa kama tulimnunua ili tumtumie namna ile... kwa kazi anayopewa muda wote, naamini hawa vijana wetu kina Willock wanamudu kuifanya kwa ufanisi zaidi kwa kuwa wana speed zaidi na ni more energetic kuliko Willian.

Mistake iliyofanywa kwenye mechi ya Liver, jana imaejirudia zaidi ya mara tatu na kocha hata haoni/harekebishi. Willian hana speed ya kucope na watu kama Grealish hivyo hana msaada kwa Bellerin wakati wa kukaba, the same ilikuwa kwa Robertson kwny game dhidi ya Liver.

Kwa hili kocha wetu hana kichaka cha kujificha,.


Ingawa bado hatujawa vizuri ktk finishing,

Willian kakosa nafasi ya wazi,
Nketia kakosa nafasi ya wazi
Lacazette the same,

Nafasi ambazo Jarmie Vardy hakuachi,

Mimi naamini tunahitaji AM na CF huyu Lacca asubiri kwanza
 
Wageni wote, tunawashukuru kwa ushirikiano wenu,
Taarifa iliyotolewą kutoka ktk kikao cha familia ni kuwa, hatutakuwa na tanga la wote kutokana na hali ngumu ya kiuchumi iliyosababishwa na COVID19.
Tutakuwa na tangandugu tu, hivyo haina haja ya kuja ni mikeka, shuka na mito...

Ahsanteni.
Vizuri ila watakuja astonvilla kuanua tanga
 
Mkifanya hivyo mtapunguza watu, sisi mpaka sasa tuna msiba mmoja tu, tena wa kimazingara, ila kila siku majirani wanakuja kuhani wakati msiba ulishapita zaidi ya mwezi.
Daaah...kaka umenichekesha sana kwa hii kauli "ila kila siku majirani wanakuja kuhani wakati msiba ulishapita zaidi ya mwezi" haha...hahaaaaaa........!

Sent from my ONEPLUS A3010 using JamiiForums mobile app
 
Tunaomba mtupe taarifa za Mazishi.

Marehemu anasafirishwa kwenda kuzikwa Nakuru au Atazikiwa hapa hapa nyumbani kwake.
 
Back
Top Bottom