Credit kubwa kwa Mikel Arteta, kuna kitu anakifanya ndani ya Arsenal ananikumbusha Pep Guardiola wakati anaingia EPL, hakuogopa kufanya makosa bali kuendelea kusimamia anachokiamini, haswa build up kuanzia eneo lake, very risky
Mohamed El Neny kwenye Kiungo ananikumbusha masimulizi ya Babu yangu juu ya Mholanzi Ruud Gullit, sikumuona ila baada ya mechi leo kanipigia na kuniambia yule MO wa leo ndio Gullit aliekuwa anamzungumzia
Sikuona sababu ya Mason Greenwood kuanza mbele ya Edson Cavani, kwa hoja ya ubora na uzoefu alipaswa kuanza, alitakiwa Mtu wa kuwapa Arsenal wakati mgumu, Cavani ni straika wa calibre ya kuwasumbua mabeki, bahati mbaya dakika hazikutosha
Thomas Partey nadhani Atletico wamepigwa, pesa Arsenal wanapaswa kuongeza Bwana, jamaa ni progressive midfielder, akikaba anaenda mpaka mwisho wa move, wakikabwa tayari yupo eneo lake, yupo kila eneo kama hewa, what a man
Kuna utawala mpya wa mabeki wa kati kutoka Brazil unajengwa pale England, mtazame Fabinho, mtazame Thiago Silva kisha Gabriel yule wa Arsenal, sio rahisi kucheza na forward yenye kasi kama United ila yeye alikuja kuipa Arsenal utulivu, katulia sana kama mvinyo kwenye chupa
Ni kazi rahisi sana kumkaba Paul Pogba mpaka nashangaa, Technician kama yeye mwenye footwork ya hatari kama yeye inakuwaje?? Nimegundua tofauti yake na Alcantara ni kuwa yeye anataka sana kukaa na mpira kuliko kuachia kwa haraka, ndio maana anakabika sana tena kirahisi
Ukitaka kumtesa Arteta ambaye anapress kama unit na anacheza kwa maelekezo mengi, ni kuwa na wachezaji wengi wazuri kwenye timu yako ambao wana ubora bila mpira, Donny Van de Beek na Edson Cavani walipaswa kuanza, wana sifa hiyo wanajua kucheza kwa eneo, hakulisoma hilo
Arsenal wamenifundisha kitu kuhusu Auba, straika anaweza kucheza kutokea pembeni, viungo wa kati wanaweza kucheza kutokea pembeni, hili neno Formation lipo tu ila muhimu ni system na maelekezo kwa wachezaji ndani ya System, Arsenal wamefaulu
View attachment 1617576