Pointi 3 zimeenda timu sahihi
Mikel Arteta amefanyaa ‘ homework’ vizuri sana aliona Man United walivyocheza mfumo wa diamond kwenye kiungo dhidi ya Leipzig , Leipzig walianzia kukaba kwa mabeki lakini Arteta kawaacha mabeki wawili wa kati wawe na mpira halafu wakaziba njia ya pasi kwenda Bruno na Pogba ....well done Mikel
Bellerin na Saka waliutanua sana uwanja ili kuwatawanya Fred na Scott kutoka kati na kuwapa uhuru Elneny na Partey na kama wasipoenda basi AWB na Shaw wanakaba watu wawili ( Auba + Saka na Bellerin + Willian )
United walikuwa chini sana ya kiwango, hakuna njia za pasi zilizofunguliwa, washambuliaji wanakuja kwenye mpira badala nyuma ya safu ya ulinzi , wingbacks hawasogei mbele na walifanya kazi ya Gunners kuwa rahisi sana . Wapo taratibu sana, hakuna mikimbio mizuri . Timu iliyocheza Jumatano ni tofauti na iliyocheza leo .
Ukitaja wachezaji ambao hawana nidhamu ya uzuiaji basi usimsahau Pogba ( hana Defensive awereness ) kabisaaaa ... alifanya kosa dhidi ya Ben Davies Vs Spurs na leo kafanya tena kosa lile lile .... sehemu kama ile nini cha kufanya !!??? Tembea na aliyepigiwa pasi mpaka mwisho, zinga na sio unaanguka chini unampa nafasi ya kusogeza mpira na wewe kumgusa yeye .... PENALTY
NOTE :
1: Najua Elneny hatotajwa sana lakini kulikuwa na sababu yake kucheza leo badala ya Xhaka ..why ?? Ana energy sana ya kwenda juu na kushuka chini kwa haraka
2: Hatimaye Arteta kavunja mwiko wa muda mrefu sana wa tangu 2006 , kupata pointi 3 Old Trafford . Na pia kamtungua Ole mara mbili tayari katika mechi zote 2
3: Tunawakumbuka United nafasi ya 15, pointi 7 katika mechi 6 . OLE AT THE WHEEL .
Credit to Ambangile