Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hivi lile lijamaa linaloletaga matokeo ya manchester liko wapi leo????
Hili huku
1600410443399.jpg
 
Pointi 3 zimeenda timu sahihi

Mikel Arteta amefanyaa ‘ homework’ vizuri sana aliona Man United walivyocheza mfumo wa diamond kwenye kiungo dhidi ya Leipzig , Leipzig walianzia kukaba kwa mabeki lakini Arteta kawaacha mabeki wawili wa kati wawe na mpira halafu wakaziba njia ya pasi kwenda Bruno na Pogba ....well done Mikel

Bellerin na Saka waliutanua sana uwanja ili kuwatawanya Fred na Scott kutoka kati na kuwapa uhuru Elneny na Partey na kama wasipoenda basi AWB na Shaw wanakaba watu wawili ( Auba + Saka na Bellerin + Willian )

United walikuwa chini sana ya kiwango, hakuna njia za pasi zilizofunguliwa, washambuliaji wanakuja kwenye mpira badala nyuma ya safu ya ulinzi , wingbacks hawasogei mbele na walifanya kazi ya Gunners kuwa rahisi sana . Wapo taratibu sana, hakuna mikimbio mizuri . Timu iliyocheza Jumatano ni tofauti na iliyocheza leo .

Ukitaja wachezaji ambao hawana nidhamu ya uzuiaji basi usimsahau Pogba ( hana Defensive awereness ) kabisaaaa ... alifanya kosa dhidi ya Ben Davies Vs Spurs na leo kafanya tena kosa lile lile .... sehemu kama ile nini cha kufanya !!??? Tembea na aliyepigiwa pasi mpaka mwisho, zinga na sio unaanguka chini unampa nafasi ya kusogeza mpira na wewe kumgusa yeye .... PENALTY

NOTE :

1: Najua Elneny hatotajwa sana lakini kulikuwa na sababu yake kucheza leo badala ya Xhaka ..why ?? Ana energy sana ya kwenda juu na kushuka chini kwa haraka

2: Hatimaye Arteta kavunja mwiko wa muda mrefu sana wa tangu 2006 , kupata pointi 3 Old Trafford . Na pia kamtungua Ole mara mbili tayari katika mechi zote 2

3: Tunawakumbuka United nafasi ya 15, pointi 7 katika mechi 6 . OLE AT THE WHEEL .


Credit to Ambangile
 
Gabriel ni Bonge la beki kaizoea EPL ndani ya muda mfupi. Ana miaka 22 lakini anacheza kama mtu mzima mwenye miak 30.

Ana vigezo vingi vya beki bora, mrefu (6'3 ft) umbo kubwa, anajua kucheza na mpira, anakaba sana, mzuri kwenye mipira ya juu.

Thamani yake itaongezeka sana ndani ya miaka 2-3 na atakuja kuwa moja ya beki bora duniani akiwa fiti na asipo Pata majeraha.

#coyg View attachment 1617426
Lille wametupiga kwa Nico na Eddu alivyo mnyambilisi akaamua kuwaibia huyu Gabriel, huyu hatujanunua, TUMEWAIBIA
 
Kwa namna tumemiliki mpira tungekua na namba 8 magoli yangekua mengi.

Iifikia hatua man u haipigi pasi zaidi ya tatu bila mpira kunaswa.

Baada ya lile shuti greenwood aligusa tena mpira mara ngapi? Fernandes?

Pressing ilikubali.

Lacazette naona kashasahau hata kupiga pasi. Nketiah hana speed wala skills. Timu inahitaji improvement ya forward.
 
Mohamed Elneny v #MUFC

66 passes (most for Arsenal player)

55 completed passes (most for Arsenal player)

39 passes in opponents half (more than anyone on the pitch)

Conceded just one foul up against Bruno, Pogba, Van De Beek etc.

•Mohamed Elneny started just 5 PL games in 2018/19
•He was loaned to Besiktas last season & rediscovered his form
•Arteta gave him another chance & has been rewarded

Played some excellent forward passes today and was key to implementing the high press behind Arsenal’s front 3

89% pass accuracy
72 touches
62 passes
5 ball recoveries
3 interceptions

Excellent Performance!
 
Back
Top Bottom