gspain
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 2,942
- 6,133
Ndugu zangu Aaron Arsenal gspain MalcolM XII 4 3 3 ingawa gspain amepoint kua ni tiki taka lakini hii hufanya kazi vyema ikiwa formation itakua na attacking fullbacks wa uhakika, kariba ya Hakimi, Davies, Arnold, Bellerin, Marcelo n.k.
Lakini ikitokea attacking fullbacks wakabanwa ndiyo utaona Liver anapigwa, Man City atapigwa na Wolves games mbili n.k. pia hii formation hua ngumu kushinda ikitokea timu pinzani ikacheza 3 5 2. Yaani hii formation ukikutana na mid ya upinzani yenye nguvu na pumzi basi mipango ndiyo inakua imeishia hapo.
Game ya PSG na Bayern tuliona jinsi Bayern alivyokaziwa akashinda moja bila tena aliyescore ni Coman mid ilishikiliwa na Davies akabanwa haswa.
Man U alivyocheza na Barcelona msimu uliopita UCL alicheza 4 3 3 mid yake ilishikiliwa kooni mpaka Man U nzima ikarudi golini.
Binafsi naamini sababu pekee timu zenye 4 3 3 zinafungwa ni ikitokea timu pinzani zinaweka 3 5 2 mfumo ambao timu ndogo nyingi ndiyo zinautumia na ndiyo zinazisurprise timu kubwa.
Kwa Arsenal yenye strikers zaidi ya 2 naamini 4 2 2 2 au 4 3 1 2 ni best kwetu, pia formation hii ni rahisi kushambulia na kurudi kukaba kwa haraka pia inakupa uwanja wa kucheza tiki taka au kaunta ukiamua.
Nakubaliana nawe kuwa kama huna players sahihi huu mfumo vijana wataku surprise. City ya msimu huu ambayo imekuwa na majeruhi wengi imefeli sana kwenye 4-3-3.
Hata Liver kwa viungo kama Hendo ambaye hanyumbuliki sana amewanyima ubunifu pale katikati na wamekuwa na option moja ya full backs tu ndio maana mwishoni mwa msimu team zimewabana.
Ikitokea mpinzani anacheza 3-5-2 kama Wolves na ana players wazuri namna ile, inabidi nawe ukubali kuswitch either kwenda 4-3-1-2 ama 3-4-3 ambayo ni variations za 4-3-3 za kujihami zaidi.
Tatizo la Liver na City, walikuwa wanaamini wamedevelop fear factor ambayo inawafanya wacommand game na si kufuata matakwa ya mpinzani ndicho kilicho wacost mara kadhaa, waliamini kwa pressing zao hawahitaji kuswitch formation. Sasa kinyume chake wao wanapresiwa na kufanya makosa yanayo wagharimu.
Kwa maoni yangu 4-3-3 ilichezwa effectively zaidi pale Barca ikiwa na
Fullbacks: Alves, Alba, Pique na Puyol/Mascherano
Midfilders: Xavi, Busquett na Iniesta
Mbele: Messi, Suarez na Neymar.



