Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

From || Fiorentina intend on pulling out of the race for Lucas Torreira, as Arsenal refuse to agree on a 2-year loan with obligation. Torino now leading the charge with a bid of €24m (£21.5m) [via - @LucaFiorino24].


There has allegedly been a new offer made, for Lucas Torreira. Unsure if it’s the €24m (£21.5m) from Torino, or another one [via - @MatteoPedrosi].
 
Alienda Anfield na huu mfumo ,Diamond style , halafu hakuwahi kuwafundisha wachezaji kwenye preseason ,

Hadi Klopp nakumbuka alisema Huu mfumo hakuwahi kuona Arsenal wakiucheza hata preseason , na huo mfumo ulisababisha Zile fullbacks zao zipande sana


Yaani emery ndio maana namuona ni kocha wa ovyo kuwahi kumshuhudia,

Alikuwa hajui kwanza characters za wachezaji, alikuwa hajui huyu nikimuweka hapa atanipa Product flan sababu ya alichonacho

Ndio maana alikuwa anabahatisha , kila mech anakuja na mfumo mpya ,

Eti toreira anampeleka no.8 au 10 au box to box MD .
Aisee siku ile Anfield tuliteseka sana hadi nikachukia, yaani tulinyanyaswa utadhani ni non league team (team ya ndondo).

Kama ulivyosema Unai anajua mifumo mingi ya soka ila tatizo hajui kwa mfumo huu nataka players gani watao deliver vizuri.

Anabadili mfumo kila mechi akiulizwa anajibu, 'we want to be unpredictable during the game'. Unakuwa unpredictable hadi kwa players wako?

Mfano kwa sasa 4-3-3 ni mfumo bora sana lakini ili uutumie lazima uwe na wachezaji ambao ni mafundi wa mpira kwenye kila idara kuanzia kipa.
 
Aisee siku ile Anfield tuliteseka sana hadi nikachukia, yaani tulinyanyaswa utadhani ni non league team (team ya ndondo).

Kama ulivyosema Unai anajua mifumo mingi ya soka ila tatizo hajui kwa mfumo huu nataka players gani watao deliver vizuri.

Anabadili mfumo kila mechi akiulizwa anajibu, 'we want to be unpredictable during the game'. Unakuwa unpredictable hadi kwa players wako?

Mfano kwa sasa 4-3-3 ni mfumo bora sana lakini ili uutumie lazima uwe na wachezaji ambao ni mafundi wa mpira kwenye kila idara kuanzia kipa.
Kweli kabisa ,ndio maana Arteta anahitaji sana kutumia 4-3-3 lakini kashindwa kukurupuka nao ,hadi apate mafundi taratibu

Kwanza kashampata LCB , alihangaika pia kaaumbakisha Xhaka ambaye atamtumia Eneo la kati kama Pep anabyomtumia Rodri

Niliona sehemu anasema hata Willian atamtumia kama no.10

Akifanikisha kuwapata hawa kina Partey , naona ndio ataelekea kutumia 4-3-3

Partey yule hata Box to Box nimeona anacheza, hata DM anacheza
 
4 3 3 mfumo bora? Nitakataa hadi basi.
Ha haaa, kwa nini unasema hivyo Castr? Kwangu me, kwa modern football 4-3-3 ni the best formation ila unatakiwa kuwa na mafundi haswa wa mpira kutokana na mfumo ulivyo.

4-3-3 ( tiki taka) ina variations nyingi sana na kutokana na kuwa ni mfumo unaotumia short passes nyingi kwenye build ups, inatakiwa everytime players wamaintain triangular shapes wakati wa passing ili kumpa more options player mwenye mpira kupiga pasi.

4-3-3 hutengeneza triangles zenye 'M' shape ukiwa kwenye half yako ili uwe more defensive na 'W' shape ukiwa umesha move kwenye half ya mpinzani ili uwe na more offensive players.

Changamoto kubwa ya huu mfumo ni kuwa na players wenye uwezo wa kucheza under pressure bila kupoteza mipira hovyo kuanzia kipa kwa sababu mnalinda kama unit na kushambulia kama unit kwa hiyo kunakuwa na space ndogo kati ya players wako na wa timu pinzani.

Mfano wake ni kama ile 'hangaisha bwege' yenye duara dogo afu wakabaji watatu.

Screenshot_20200908-133453.jpeg
 
Kweli kabisa ,ndio maana Arteta anahitaji sana kutumia 4-3-3 lakini kashindwa kukurupuka nao ,hadi apate mafundi taratibu

Kwanza kashampata LCB , alihangaika pia kaaumbakisha Xhaka ambaye atamtumia Eneo la kati kama Pep anabyomtumia Rodri

Niliona sehemu anasema hata Willian atamtumia kama no.10

Akifanikisha kuwapata hawa kina Partey , naona ndio ataelekea kutumia 4-3-3

Partey yule hata Box to Box nimeona anacheza, hata DM anacheza
Arteta kabla ya yote nilimpa credit kwa kuicheza vizuri diamond ya 3-4-3 ambayo kimsingi ndiyo mfumo unaoweza kudhibiti variations almost zote za 4-3-3 kwa kuwa unamuweka mpinzani katikati wakati unamkaba na kumzuia kupiga penetration passes wala hakuna space ya counter attacks.

3-4-3 ina offer pressing wakati wa kumkaba mpinzani almost equally kwenye 1st, 2nd na 3rd ground of the pitch kwa hiyo kwa maoni yangu mimi ni mfumo unaoleta balance nzuri kwa timu hasa ukikutana na hawa miamba wa 4-3-3.

Ukitaka kulibaini hilo hata kama huna skills za mpira cheki tulivyo wadhibiti Liver na City kwenye mechi tulizokutana nao baada ya ujio wa Arteta. Tuliwalazimisha kufanya makosa wakati wao ndio huwa wanatupress sisi.
 
Bila ubishi mzee.. Kwa sasa huo ndio mfumo bora.

Tunaona wakitumia timu kubwa kama PSG, Man City, Barcelona, Real Madrid, na timu nyingine nyingi tu.
Nakuunga mkono, huu mfumo team zitaukwepa kwa kutokuwa na players husika tuu ila ni mfumo bora sana kwa sasa. Ni mfumo unaoleta burudani ya soka na madhara kwa mpinzani.
 
Arteta kabla ya yote nilimpa credit kwa kuicheza vizuri diamond ya 3-4-3 ambayo kimsingi ndiyo mfumo unaoweza kudhibiti variations almost zote za 4-3-3 kwa kuwa unamuweka mpinzani katikati wakati unamkaba na kumzuia kupiga penetration passes wala hakuna space ya counter attacks.

3-4-3 ina offer pressing wakati wa kumkaba mpinzani almost equally kwenye 1st, 2nd na 3rd ground of the pitch kwa hiyo kwa maoni yangu mimi ni mfumo unaoleta balance nzuri kwa timu hasa ukikutana na hawa miamba wa 4-3-3.

Ukitaka kulibaini hilo hata kama huna skills za mpira cheki tulivyo wadhibiti Liver na City kwenye mechi tulizokutana nao baada ya ujio wa Arteta. Tuliwalazimisha kufanya makosa wakati wao ndio huwa wanatupress sisi.
Umeeleza vzr sana , aisee kwa mfumo wa 3-4-3 nimeuangalia hata Jana YouTube jinsi Arteta anabyoutumia ,ndio usemacho hapa

Kwanza nimeshangaa sana jinsi Lacazette kumbe huwa anatakiwa arudi chini kama kiungo ,kwenye mech na City alirudi chini kumbana Gundogan , halafu xhaka na ceballos wanakuwa free kupeleka mipira haraka kwenye wings au kwa wingback

Mpira unapokuwa kwa Pepe , Lacazette anakuja katikati ya zile CBs Mbili ,hivo zinaacha space kwa Auba kufunga
IMG_20200906_182947.jpg
 
Nakuunga mkono, huu mfumo team zitaukwepa kwa kutokuwa na players husika tuu ila ni mfumo bora sana kwa sasa. Ni mfumo unaoleta burudani ya soka na madhara kwa mpinzani.
Nadhan Arteta atakuwa akikutana na hizi timu kama Liverpool au man city atacheza 3-4-3

Akiwapata Partey na Aouar atakuwa huru sasa kutumia 4-3-3 na 3-4-3

Nimeona hadi kwenye buildup , zile CBs tatu, mmoja anaachwa free iwapo itatokea hawa wawili wamebanwa wakati kipa kaanzisha mipira. Na anayekuwa free huwa ni KT, halafu xhaka au ceballos wanakuwa karibu sana na hawa CBs , ili hawa CBs wawe na option nyingi sana ya kupiga pass za buildup

Vitu kama hivi kwa Unai ilikuwa hakuna , wachezaji walishindwa kupiga buildup ,kwanza kupiga pass had wageuke nyuzi 360 , pia wakipresiwa tu wanakosa option ya kumpa ,lkn Kwa Arteta katengeneza structure Beki anakuwa na option had 3 za kupeleka mpira

IMG_20200908_140618.jpg
 
Yah aisee Lacazette kwenye huu mfumo anamudu vizuri sana ndio maana me sikupenda auzwe, wengi wanatahmini performance yake kama CF ila kwenye huu mfumo wa 3-4-3 amepewa majukumu mengine ambayo kwa maoni yangu anayafanya kwa ufanisi wa zaidi ya 90%.

Amemfanya Auba kuwa na more space kama ulivyosema kutokana na movements zake ambazo zinawafanya defenders wa opponent wawe off positions na kwa speed ya Auba anawaua kiulaini akitokea pembeni. Ndio maana Arteta hawezi mpanga Auba kama CF sababu atakosa kuitumia ile speed yake vizuri.

Ukiangalia muda wote anapocheza Xhaka na Ceballos hatuna defensive midfielder na kazi hiyo hufanywa na Lacazette.

Kama kuna mtu kamnyima namba Torreira ni huyu Laca, ukiwaangalia Xhaka na Ceballos kiuchezaji hata hawafanani na Torreira ambaye ni mzama uvunguni, mtu wa kupiga viatu na kupunguza speed ya wapinzani kama Kante.

Umeeleza vzr sana , aisee kwa mfumo wa 3-4-3 nimeuangalia hata Jana YouTube jinsi Arteta anabyoutumia ,ndio usemacho hapa

Kwanza nimeshangaa sana jinsi Lacazette kumbe huwa anatakiwa arudi chini kama kiungo ,kwenye mech na City alirudi chini kumbana Gundogan , halafu xhaka na ceballos wanakuwa free kupeleka mipira haraka kwenye wings au kwa wingback

Mpira unapokuwa kwa Pepe , Lacazette anakuja katikati ya zile CBs Mbili ,hivo zinaacha space kwa Auba kufunga View attachment 1563164
 
Ndugu zangu Aaron Arsenal gspain MalcolM XII 4 3 3 ingawa gspain amepoint kua ni tiki taka lakini hii hufanya kazi vyema ikiwa formation itakua na attacking fullbacks wa uhakika, kariba ya Hakimi, Davies, Arnold, Bellerin, Marcelo n.k.

Lakini ikitokea attacking fullbacks wakabanwa ndiyo utaona Liver anapigwa, Man City atapigwa na Wolves games mbili n.k. pia hii formation hua ngumu kushinda ikitokea timu pinzani ikacheza 3 5 2. Yaani hii formation ukikutana na mid ya upinzani yenye nguvu na pumzi basi mipango ndiyo inakua imeishia hapo.

Game ya PSG na Bayern tuliona jinsi Bayern alivyokaziwa akashinda moja bila tena aliyescore ni Coman mid ilishikiliwa na Davies akabanwa haswa.

Man U alivyocheza na Barcelona msimu uliopita UCL alicheza 4 3 3 mid yake ilishikiliwa kooni mpaka Man U nzima ikarudi golini.

Binafsi naamini sababu pekee timu zenye 4 3 3 zinafungwa ni ikitokea timu pinzani zinaweka 3 5 2 mfumo ambao timu ndogo nyingi ndiyo zinautumia na ndiyo zinazisurprise timu kubwa.

Kwa Arsenal yenye strikers zaidi ya 2 naamini 4 2 2 2 au 4 3 1 2 ni best kwetu, pia formation hii ni rahisi kushambulia na kurudi kukaba kwa haraka pia inakupa uwanja wa kucheza tiki taka au kaunta ukiamua.
 
Nadhan Arteta atakuwa akikutana na hizi timu kama Liverpool au man city atacheza 3-4-3

Akiwapata Partey na Aouar atakuwa huru sasa kutumia 4-3-3 na 3-4-3

Nimeona hadi kwenye buildup , zile CBs tatu, mmoja anaachwa free iwapo itatokea hawa wawili wamebanwa wakati kipa kaanzisha mipira. Na anayekuwa free huwa ni KT, halafu xhaka au ceballos wanakuwa karibu sana na hawa CBs , ili hawa CBs wawe na option nyingi sana ya kupiga pass za buildup

Vitu kama hivi kwa Unai ilikuwa hakuna , wachezaji walishindwa kupiga buildup ,kwanza kupiga pass had wageuke nyuzi 360 , pia wakipresiwa tu wanakosa option ya kumpa ,lkn Kwa Arteta katengeneza structure Beki anakuwa na option had 3 za kupeleka mpira

View attachment 1563169
Uko sahihi nadhani lengo kuu la Arteta ni kutumia 4-3-3 na tukikutana na hawa wabishi tunaswitch kwenye 3-4-3.

Kwa sasa hatufungwi kwa counter attacks hovyo na option iliyobaki ni kutipiga kwa set-pieces ndio maana Arteta kachukua mtaalam wa set-pieces kutoka Brentford ili kulitatua hilo.

Ukishakuwa hupotezi mipira hovyo ukipresiwa na hauruhusu counter attacks za hovyo na uko vema kwenye set pieces, hizi timu ndogo zote ambazo hutegemea set pieces na counter una uhakika wa kuzipiga na huko ndipo kuna points nyingi.
 
Ndugu zangu Aaron Arsenal gspain MalcolM XII 4 3 3 ingawa gspain amepoint kua ni tiki taka lakini hii hufanya kazi vyema ikiwa formation itakua na attacking fullbacks wa uhakika, kariba ya Hakimi, Davies, Arnold, Bellerin, Marcelo n.k.

Lakini ikitokea attacking fullbacks wakabanwa ndiyo utaona Liver anapigwa, Man City atapigwa na Wolves games mbili n.k. pia hii formation hua ngumu kushinda ikitokea timu pinzani ikacheza 3 5 2. Yaani hii formation ukikutana na mid ya upinzani yenye nguvu na pumzi basi mipango ndiyo inakua imeishia hapo.

Game ya PSG na Bayern tuliona jinsi Bayern alivyokaziwa akashinda moja bila tena aliyescore ni Coman mid ilishikiliwa na Davies akabanwa haswa.

Man U alivyocheza na Barcelona msimu uliopita UCL alicheza 4 3 3 mid yake ilishikiliwa kooni mpaka Man U nzima ikarudi golini.

Binafsi naamini sababu pekee timu zenye 4 3 3 zinafungwa ni ikitokea timu pinzani zinaweka 3 5 2 mfumo ambao timu ndogo nyingi ndiyo zinautumia na ndiyo zinazisurprise timu kubwa.

Kwa Arsenal yenye strikers zaidi ya 2 naamini 4 2 2 2 au 4 3 1 2 ni best kwetu, pia formation hii ni rahisi kushambulia na kurudi kukaba kwa haraka pia inakupa uwanja wa kucheza tiki taka au kaunta ukiamua.
Mimi kwakweli 4-2-3-1 huu mfumo siupendi kabisa

Binafsi sio muumini wa lone straiker , kwa siku za karibuni nimeona Bayern Munich akifanikiwa nao ,lakini na yeye anaposhambulia Fullbacks zinapanda na kufanya wawe wengi

4-3-3 Dawa yake ni 3-4-3 au 3-5-2

Hitaji la Arteta ni siku moja Atumie 4-3-3 ,
 
Mimi kwakweli 4-2-3-1 huu mfumo siupendi kabisa

Binafsi sio muumini wa lone straiker , kwa siku za karibuni nimeona Bayern Munich akifanikiwa nao ,lakini na yeye anaposhambulia Fullbacks zinapanda na kufanya wawe wengi

4-3-3 Dawa yake ni 3-4-3 au 3-5-2

Hitaji la Arteta ni siku moja Atumie 4-3-3 ,
Chief nimeandika 4 3 1 2
 
Kama Ozil akiwa 100% committed sioni Arsenal wakihangaika na Aouar msimu huu labda kwa next season wakati Ozil atakuwa free agent.

If that will be the case then Arsenal will be in pole position to complete the signing of Thomas Partey from ATM.
Jaman ozil sio mchezaji wa kutegemea tena amebaki na jina tu
 
Back
Top Bottom