Game ya leo. Nilisema tukipaki basi tutashinda. Tumeingia na 3 4 3 lakini tumeperform tofauti na ile game tuliyowafunga 2 kwa 1.
Arsenal tumepiga shots 13 huku 7 zikiwa on target, liva ana shots 8 on target. Kwa kikosi kilichokuepo naon tumejitahidi.
Nketiah kwa alichofanya leo bado naona atasubiri sana kwa Martnell kama asipoongeza bidii.
Hua namlalamikia Pepe kwa kushindwa kufanya cut in na kuscore (angalia Auba alivyoscore) naona na Saka naye ni walewale, yaweza kua hatuna mtu sahihi bado. Ndiyo maana msimu uliopita tulivyohusishwa na Ziyech niliona itakua transfer tamu kwetu.
Kwa uzembe wa Nketiah na Saka tumekosa nafasi 3 za kuscore kwa uhakika.
Pale katikati Elneny na Xhaka wamepasawazisha. Elneny alikua anapiga chenga, anatafuta mtu anampa pasi, anamkosa anasonga mbele, Milner akabaki kucheza rafu tu. Xhaka na Elneny ni couple mpya pale kati ambayo inadeliver vyema.
Juzi nilisema Elneny abaki, na leo nasema tena. Elneny abaki.
Goli la kusawazisha la liva ilikua komedi kidogo. Tunakaba conservatively mno, yaani wachezaji wetu kua aggressive na kuingiza mguu ni mtihani, magoli mengi tunafungwa kwa aina yetu ya ukabaji.
Game na Chelsea kwenye FA ilikua same, na leo hivyo hivyo. Kama inawezekana tubadilishe defensive style. Inakua kama FIFA 20 bwana...
Timu katikati ilibalansi. Kulikua na connection nzuri ya mid na defense kuliko mid na forward. Hata hii connection ya mid na defense sometime ilikua inakata ila it was some sight to see.
Aubameyang arudishwe kati. Hana skills za kufanya iwe rahisi kwake kucut in. Wazia angekua na skills kama za Pepe, angeweza kuscore peke yake goli mbili.
Martinez huku Leno.... hii inaitwa nianze chai au nianze mkate... Kotekote kuzuri. Hope kila mmoja atakula play time ya kutosha.
Tulifunga msimu kwa kombe. Tumefungua msimu kwa kombe. Ni poa mno. Ila tusijisahau Arteta aliomba miaka 3 ya kujenga timu, huu ndiyo wa kwanza. So performance ya leo isikufanye ukatukane watu... Hahahaha