Its finally back!
.
Hayawi hayawi sasa yamekuwa!baada ya kuikosa burudani ya soka la uingereza kwa muda wa takribani miezi mitatu sasa imerudi tena,
.
Yes ni leo utamu umerejea tena Manchester city akimkaribisha Arsenal pale Etihad,
.
Mchezo huu ulitakiwa kupigwa machi 11 lakini ukahairishwa kutokana na Corona
.
Tena ilichochewa zaidi na taarifa ya baadhi ya wachezaji wa Arsenal kusemekana kukutana na rais wa Olympiacos wakati wa mchezo wa Europa league kati ya Arsenal na Olympiacos,
.
Rais wa Olympiacos wakati huo alikuwa akiugua ugonjwa wa Corona,Basi ngoma ikahairishwa bhana.
.
Pia siku chache Arteta nae akakutwa na maambukizi ya ugonjwa huo.
.
Kama kuna kaupande kalidhani kameepuka hiki kikombe basi kalijidanganya ngoma hii hapa tena Arteta uso kwa Uso na mwalimu wake na bosi wake wa zamani Pep Guardiola,
.
Arsenal watashuka dimbani leo wakiwa na wasiwasi wa kuwakosa Callum Chambers na Lucas Torreira japo kuna matumaini baada ya kieran Tierney kuwa fit tayari kwa mchezo kama akiamua kumtumia(Arteta).
.
Lakini upande wa pili huko Manchester City wachezaji wake wote wako fiti hadi waliokuwa majeruhi wameshapona kama vile Aymeric Laporte na Leroy Sane,
.
Kurejea kwa Laporte kutaifanya safu ya ulinzi ya City kuwa salama zaidi,Itawapasa washambuliaji wa Arsenal kufanya kazi ya ziada kupenya
.
Wachezaji wengi wanaweza kuwa hawana match fitness ya kutosha hasa wale wenye umri mkubwa kiasi kama vile Aguero,David Silva na wengineo badala yake yampasa Guardiola kuwaanzisha vijana zaidi.
.
Mfano anaweza kumuanzisha Phil Foden badala ya David Silva na G.Jesus badala ya Aguero inaweza kumsaidia zaidi.
.
Upande wa Arsenal namuona Arteta akianza na mfumo wa

-

-

-

nampa nafasi Pablo Mari na Luiz pale nyuma huku Xhaka na Ceballos wakitawala dimba pale juu yao Ozil kama kawaida kule pembeni chini kabisa kushoto Tierney na kulia Bellerin.
.
Pale golini Leno kama kawaida na winga ya kushoto anakabidhiwa Aubameyang na ya kulia Pepe pale juu ataanza Lacazette
.
Kikosi cha City chaweza kuanza hivi Ederson,Walker,Fernandinho,Laporte,Zichenko,De Bruyne,Rodri,Silva,Bernado,Aguero,Sterling.
.
Japo nategemea mabadiliko zaidi ya damu changa kikosi cha City.
View attachment 1481346