OZIL master wa Assist
Binafsi silaumu kwa mchezaji wa kariba ya Ozil kuwekwa bench...
Kuna kipindi sikuwa namuelewa kabisa huyu mchezaji. Hata kipindi wakati Sanchez anataka kuondoka kuna mtu alishawahi kuniuliza 'hivi kati ya Sanchez na Ozil ukiambiwa uchague mmoja aondoke utamchagua nani?'
Kwa haraka nilijibu Ozil lakin baada ya kutafakari nijicheka sana.
Ozil ni mtu wa kipekee sana, kuna kitu tunakikosa kwenye timu yetu kwa sasa. Hatuna mtu wa kupiga risk passes.
Hii namaanisha mtu wa kupiga pass ambazo kama zikipita mabeki basi hatari yake ya kusabisha goli ni zaid ya 90%.
Viungo wetu wengi tulionao ni wale ambao wakifika eneo la mita 30 kutoka lango la mpinzani basi atapiga pass kwa mtu ambae yuko karibu na ana uhakika pass itafika bila kupotea ( square pass).. yani namaanisha kwa mtu ambae watu wengi wanaona kuwa lazima atapewa pass tu mchezaji yule..
Hii inarahisisha hata kwa mabeki kumkaba mtu kirahisi na kumnyima nafasi kwakuwa walishajua atapewa pass na kweli anapewa.
Sasa hii inakuwa tofauti kwa upande wa Ozil.
Yeye akifika eneo la kuanzia mita 30 kutoka lango la mpinzani huwa anakua na jicho la tofauti kabisa, anapiga pass ambayo kama ikipita lazima isababishe madhara hata kama haitakua goli basi lazima Auba ama Laca atakosa goli litakalokuacha mdomo wazi..
Anapiga pasi kwa mtu ambae hujamdhani kabisa. Anaweza akageuka kushoto(kwa Kolasinac) afu akajikunja kama samaki kupiga pass kulia(kwa Belle)
Hata kama haitakua ni pass ya mwisho (assist) basi itakuwa ni pass inayomrahisishia mtoa assist apige pasi yake ki rahisi zaidi.
Na kwa Ozil hizi pass uwezo wake wa kuzifikisha kwa mtu ni zaid ya 50% .
Wachezaji wa namna hii ni wachache sana, unaweza kumpata labda Cazorla, Wilshire,David Silva, Fabregas Debruyne nk.
Tukubali tukatae, ukimtoa Ozil mtu wa kuvaa viatu vya kutimiza hili jukumu kwa sasa hatuna kwenye kikosi chetu, na waliopo hata wakijaribu ni mara chache sana wameweza kusifikisha hizi pass maeneo husika....
Akicheza mtu kama Ozil utaona hata kama hatufungi magoli mengi lkn unaona kuna kosakosa nyingi sana za magoli ya wazi..
Lkn kwa wachezaji tulionao nafasi za magoli na hata kosakosa huwa ni chache sana
Kwaio binafsi sipingi Ozil kukaa bench lakin je, ni nani wa kuvaa viatu vyake na akatengeneza muunganiko na kazi rahisi kati ya kiungo wakabaji na striking force yetu??