Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Washabiki wengine ligi ikianza mnakimbia mnawaacha MBU,AW & Balantanda
 
Soka la miguvu lishapitwa na wakati ndio maana hata kwenye World cup mwaka huu kina England, France, Italy walipata vichapo vya haja huku Spain, Uruguay, Germany na Holland zikipita maana wanacheza kwa mbinu na akili sio miguvu. Man U na Chelsea mwaka huu hamuambulii kitu subiri uone moto wa the Gunners vijana wa kugusa na kuteleza

Hehehe kila mwaka mnasemaga hivi hivi alafu mnaambulia patupu.
 
.................Arsenal can confirm that Eduardo has joined Ukrainian champions Shakhtar Donetsk for an undisclosed fee.........arsenal.com
 
Mkuu tupo pamoja japo nilipata ajali mbaya sana mwezi wa tano,ndo nimerudi naendeleza matibabu.
Dah pole sana mkuu, tupo pamoja na Mungu atakupa nguvu za ku-recover haraka, meanwhile.........i Man Citeh wanamnyemelea Drogba! naona bado kutakuwa na twist and turn kabla ya msimu kuanza! yetu macho.
 
Asanteni sana wakuu kwa msgs mlizonitumia na wale mlionitakia kupona haraka hapa jukwaani,nasema tena asanteni na Mungu aendelee kuwa nanyi,nina imani kuwa nitarudi barabarani soon.Asanteni sana
 
N'gwanza Madaso pole sana mungu akupe nguvu upone haraka.

...duh, upo aisee? long tym!

Hehehe nipo mkuu, vipi naona baada ya msimu kuisha ukaingia mitini au uko likizo?
Huyo Eduardo mbona mumemuuza kwa bei poa?
 
aaaah, acha tu mkuu. Tatizo linapokuja suala la kununua wachezaji Arsene atasema pesa hazikutosha. Mpaka sasa GALLAS, SILVESTRE, SENDEROS, EDUARDO, ndio weshaaga hao. kumbukumbu yangu inaonyesha tumenunua wapya wawili tu!

We'll be among the leaders for few months (nguvu ya soda), around October/November most of our key players will be out for 2 weeks to 2 months due to injuries (as usual). In my opinion the team to beat is still Chelsea although there is a possibility that MANCITY will be able to challenge them for the top spot.
 
Angalieni wenzenu Liverpool wanaanza era nyingine,hapo Emirates bado sijaona mabadiliko yeyote.XAVI anasema Fabregas anacheza Arsenal kwa mkopo soon atarudi kwenye timu yake
 
Wakubwa samahani kidogo ,MASANILO anagombea jimbo gani?
 
Hehehe nipo mkuu, vipi naona baada ya msimu kuisha ukaingia mitini au uko likizo?
Huyo Eduardo mbona mumemuuza kwa bei poa?

...ha ha, yap...nilichukua likizo jukwaa la Sports na Starehe. Sikuwa mshabiki wa timu yoyote World Cup. France waliniangusha bana.
Tunarudi sasa kwa Ari zaidi, Nguvu zaidi, kasi Zaidi... kama JK vile hehehehe....

We'll be among the leaders for few months (nguvu ya soda), around October/November most of our key players will be out for 2 weeks to 2 months due to injuries (as usual). In my opinion the team to beat is still Chelsea although there is a possibility that MANCITY will be able to challenge them for the top spot.

...dah, msimu uliopita ulitabiri the worse ikatokea kweli, sasa unaanza tena..aaaah!
Wapi 'Paul the Octopus' jamani,
najiskia kama nichukue likizo msimu mzima kutoishabikia Arsenal kwa mtaji huu.
 
Soka la miguvu lishapitwa na wakati ndio maana hata kwenye World cup mwaka huu kina England, France, Italy walipata vichapo vya haja huku Spain, Uruguay, Germany na Holland zikipita maana wanacheza kwa mbinu na akili sio miguvu. Man U na Chelsea mwaka huu hamuambulii kitu subiri uone moto wa the Gunners vijana wa kugusa na kuteleza
spain ya zamani ilikuwa kama arsenal ukicheza mpira wa kutumia ubavu rafu unawafunga,ila sasa nao wanajua kucheza mpira wa fujo,ronaldo ulimuona jinsi alivyokuwa anachezewa kibabe na sergio busquets,mpira wa reyes chenga nyingi ulikwisha kwa rafu za phil na gary neville mechi ya man utd vs arsenal,chenga twawala huwezi kumfunga ujerumani au hata england,inabidi chakula,spain ina alonso,busquets na xavi,ndio mana fabregas alikuwa benchi 7bu mojawapo hana nguvu kama hao niliowataja juu au hata kwa iniesta,kwa staili hiyo arsenal itafungwa daima na timu za chelsea na man utd
 
...ha ha, yap...nilichukua likizo jukwaa la Sports na Starehe. Sikuwa mshabiki wa timu yoyote World Cup. France waliniangusha bana.
Tunarudi sasa kwa Ari zaidi, Nguvu zaidi, kasi Zaidi... kama JK vile hehehehe....



...dah, msimu uliopita ulitabiri the worse ikatokea kweli, sasa unaanza tena..aaaah!
Wapi 'Paul the Octopus' jamani,
najiskia kama nichukue likizo msimu mzima kutoishabikia Arsenal kwa mtaji huu.


Hahahahahahaha Naijua timu yetu ndugu yangu na miaka ya karibuni pamoja na kutandaza mpira wa hali ya juu kuliko timu yoyote ile lakini hatupati ushindi na usajili katika msimu mpya unaonza in 3 weeks si wa kuridhisha. Ningekuwa na accuracy kama ya PTO mbona ningejidai LOL! lakini kwenye timu yetu sidhani kama utabiri wangu utakuwa na makosa makubwa. Ngoja tusubiri tuone.
 
...hehehehe....mnaanza sasa, mzee wa mapicha Wacha1 akirudi likizo hapatakalika hapa!
Wazi hii ni Preemtive measure, ngoja nitume pm kwa Wacha1 arudi likizo, matusi yameanza sasa, wanawaogopa noisy neighbour Citeh na ile welcome to manchester Tevez bado imewabamba, sasa wamerukia kwetu daah, ila hii ni ishara ya uwoga labda wanachungulia nafasi ya 5 mwaka huu, kule kwetu dizaini hii tunawaita "nguvu-mdomo" wanatawaliwa na hofu Citeh ameshawapa indicator anawa-overtake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom