Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arteta is cheap option hasa kwenye budget,he's amatuer na sababu kubwa ya kung'ang'aniwa ni ubahili tu nawaza tu yeye mwenyewe alikosa game time kwenye misimu miwili ya mwisho sijui ata-command vipi dressing room yake naona wanaompigia debe wanakomaa kua amepikwa na Pep ivyo anatosha kuja Arsenal.
Hapa ni bora yule babu kuliko tatizo tunaloletewa,kama siku zote nitam-support yoyote yule ambae atakua kocha wetu.
Mbona mmeanza kutamani Wenger arudi kabla hata mrithi wake hajapatikana?
 
Mkuu Sio Kwamba Makocha Wenye CV Kubwa Hawapo Wanaotaka Kuifundisha Arsenal! Wapo Kibao Kwani Almost Kila Kocha Anahamu Ya Kumrithi Wenger ili ajijengee Heshima Kupitia Title ya Wenger.

Lakini Problem Lipo Kwenye BUDGET! Kwasasahivi Kocha ambaye tayari Ameshajijengea CV nzuri Ukimgusa tu basi atakwambia Salary Yangu Ni £16m au zaidi per year (wakati Wenger mwenyewe alikuwa akilipwa £8m per year) Na atakuekea Sharti la Kimaandishi Kuwa Katika First window tu Yake umpe £200m za usajili na Second window umpe £100m ili akamilishe £300m Katika First Season Yake.

Sasa hapo ndiyo Owners Wanapopishana Kauli na Makocha World Class Wakati Utajiri uliyonayo Club Ya Arsenal Wanauwezo Hata Wa Kumng'oa Guardiola Pale Man City.

Lakini Ukimuangalia Arteta Hata Salary ya £7m per year yupo tayari na Hata Kama Hakupewa Hata senti ya usajili Katika Season nzima basi yupo tayari na kikosi hichohicho kwanini Matajiri Wasimkubali?

Mkuu Arteta ameshafocus Mbali hapo! Anataka Just kuja kuandika CV tu Arsenal ili Atambulikane Rasmi Katika Ukocha Hata kama akitimliwa Arsenal.
Umechambua vizuri sana.Nimekuelewa kwa sehemu hongera.
 
Kwa wapenzi wa Arsenal. Kama tumeweza kuvumilia miaka 14 chini ya Wenger naomba tutumie nguvu, imani hiyo hiyo kuvumilia miaka 14 mara 14 ijayo chini ya Mikel "no ubavu" Arteta maana inaelekea ndiye atachukuwa mikoba according to the reports
 
Aje tu hata huyo ateta maana hata tukiandika sana humu na uchambuzi uliotukuka bado mshahara atalipwa Management sis tutabak kukoment tu
 
Kwa wapenzi wa Arsenal. Kama tumeweza kuvumilia miaka 14 chini ya Wenger naomba tutumie nguvu, imani hiyo hiyo kuvumilia miaka 14 mara 14 ijayo chini ya Mikel "no ubavu" Arteta maana inaelekea ndiye atachukuwa mikoba according to the reports

Aje tu hata huyo ateta maana hata tukiandika sana humu na uchambuzi uliotukuka bado mshahara atalipwa Management sis tutabak kukoment tu

Piers Morgan alikua pioneer wa WENGER OUT kwa muda mrefu sana ila leo hii anaona kabisa movement zake hazijaleta maana yoyote kwa kitendo cha board kumpa timu Arteta.
Nimeuliza mara nyingi nini kitafuata baada ya Wenger Out,naona board inatuvua nguo ukweni mchana kweupeeee nasikia Vieira soon anakua coach wa Nice.
 
Arsenal need to find onather option maana huyu Arteta aliyetoka kustaafu two yrs ago ndo apewe club kubwa kama hii. Au sababu ni kukaa karibu na pep. Ni afadhali mara100 wangempa Hendry au hata Viera.

Kuna taarifa kuwa Arsenal wametenga 50m£ kwa ajili ya usajili msimu ujao. Na pesa nyingine watapata kwa kuuza wachezaji ambao hawapo kwenye mipango yao. Kutoshiriki kwao UCL kutawafanya wakose world class player ambao wengi wana kiu ya kucheza ligi ya mabingwa. Tarajieni wachezaji wa kawaida haswa kwa soko la ufaransa.
 
Piers Morgan alikua pioneer wa WENGER OUT kwa muda mrefu sana ila leo hii anaona kabisa movement zake hazijaleta maana yoyote kwa kitendo cha board kumpa timu Arteta.
Nimeuliza mara nyingi nini kitafuata baada ya Wenger Out,naona board inatuvua nguo ukweni mchana kweupeeee nasikia Vieira soon anakua coach wa Nice.
Vieira bado ni kocha wa New York city bado hajapata kazi au interview Ufaransa. Timu inayosemekana kumtaka yeye na wengine ni Nantes sio Nice (per Espn). Nantes wapo mbioni kumtafuta kocha mpya na wanaangalia options zote.
Nilikuwa nasapoti (bado nasapoti) kuondoka kwa Wenger. Arsenal tulikuwa stagnate chini ya Wenger for 14yrs. Soka letu limeporomoka in last 4 or 5 yrs ilikuwa ni vizuri kumove on to new era. Ndivyo maisha ya soka, biashara yalivyo. Hata hivyo hili la kumpa Arteta nina wasiwasi nalo sababu hana proven record zaidi ya kuwa msaidizi wa Pep. Arteta anaweza kuja kuwa kocha mzuri au mbaya hakuna anayejua. Watu wanadai Arteta ni very good katika tactics, analyze game play or whatever. Kama wanataka kumpa kazi kwa sababu hizo basi wanaweza kuwapa kazi hiyo watu kibao duniani. Wapo watu wengi wana hizo sifa. Tatizo la Arsenal miaka yote ni kuwa na board mbovu kama viongozi wa nchi za Afrika. Hawa kina Kroenke(family) na Ivan Gazidis watatuporomosha Championship miaka michache ijayo. Hawajui ku-run biashara ya soka. Wapo cheap kinoma. Soka la kudunduliza sumni hadi sumni limepitwa na wakati muda sana. Tusubiri tuone watakabidhi mikoba nani. Inawezekana Arteta akawa ni mmoja wa applicants to be considered.
 
Vieira bado ni kocha wa New York city bado hajapata kazi au interview Ufaransa. Timu inayosemekana kumtaka yeye na wengine ni Nantes sio Nice (per Espn). Nantes wapo mbioni kumtafuta kocha mpya na wanaangalia options zote.
Nilikuwa nasapoti (bado nasapoti) kuondoka kwa Wenger. Arsenal tulikuwa stagnate chini ya Wenger for 14yrs. Soka letu limeporomoka in last 4 or 5 yrs ilikuwa ni vizuri kumove on to new era. Ndivyo maisha ya soka, biashara yalivyo. Hata hivyo hili la kumpa Arteta nina wasiwasi nalo sababu hana proven record zaidi ya kuwa msaidizi wa Pep. Arteta anaweza kuja kuwa kocha mzuri au mbaya hakuna anayejua. Watu wanadai Arteta ni very good katika tactics, analyze game play or whatever. Kama wanataka kumpa kazi kwa sababu hizo basi wanaweza kuwapa kazi hiyo watu kibao duniani. Wapo watu wengi wana hizo sifa. Tatizo la Arsenal miaka yote ni kuwa na board mbovu kama viongozi wa nchi za Afrika. Hawa kina Kroenke(family) na Ivan Gazidis watatuporomosha Championship miaka michache ijayo. Hawajui ku-run biashara ya soka. Wapo cheap kinoma. Soka la kudunduliza sumni hadi sumni limepitwa na wakati muda sana. Tusubiri tuone watakabidhi mikoba nani. Inawezekana Arteta akawa ni mmoja wa applicants to be considered.

IMG_5963.JPG

Arteta anapata backup ya Ivan kwa sababu anajua hata kwa squad iliyopo jamaa atapiga kazi na tetesi zinasema wameandaa £ 50Million tu kwa dirisha lililofunguliwa leo unadhani kocha gani mwenye akili anaweza kukubali hiyo pesa ambayo itaishia kununua mediocre players wawili.
Sikatai Arteta anaweza kua kocha bora baadae ila kwa ilipofikia Arsenal sio kufanya gambling ya mwalimu baada ya mwenendo mbovu tulionao ni ajabu kama kuna mtu anaamini Arteta ni bora kuliko Wenger sasa kama board walijua wanaungaunga kulikua na sababu gani ya kumuambia AW a-step down simply hii board ina lack leadership maana kuna makocha wapo wanasubiri kazi ila Arsenal hawataki kutumia pesa kwa budget hizi za kichaga basi hata anaekuja tutamfanya scape goat kama ambavyo AW alifanywa lazima tukubali AW alikua anapewa budget ndogo sana ukilinganisha na wapinzani wake.
Welcome back home Mikel Arteta bila kujali haya mengine mimi shabiki wa Arsenal nitam-support kwa kila kitu mwiso wa siku Arsenal itabaki ila sisi tutaondoka.
 
Tunajaribu kuleta kila tetesi ambayo inakaribiana na ukweli jambo la muhimu ni wewe mwenyewe ku-balance hizi story ambazo zimekua nyingi dhumuni ni kupeana habari.
IMG_5977.JPG
 
*PREMIER LEAGUE SIO YA MAJARIBIO.*

Ni muda mfupi toka kocha Mkongwe wa Arsenal Arsene Wenger aliye dumu na klabu hiyo kwa miaka 22 kuondoka Emirates. Huku vuguvugu la kutafuta mrithi wa mikoba yake likionekana kuwa kubwa sana kutokana na klabu hiyo kukaa kipindi kirefu sana bila kubadilisha kocha.

Vuguvugu hili limekua kubwa sana kuliko hata lile la 2013 pindi Sir Alex Ferguson alipotangaza kuondoka Old Trafford tofauti hiyo inatokana na Ferguson kupewa maamuzi ya kuchagua mrithi wake tofauti na ilivyo kwa Mzee mwenzake Arsene ambae yeye hajapewa heshima hiyo, huenda Arsenal walijifunza kutoka Manchester maana Mteule aliyepewa nafasi na Sir Alex hakuweza kufanya kile kilicho zaniwa na wengi na mwisho kuiweka timu katika mazingira mabaya zaidi ambayo ni kinyume na desturi ya klabu hiyo.

Lakini huenda somo ambalo Arsenal walijifunza kutoka Manchester walikua wamelielewa kinyume chake maana premier league ya sasa inahitaji mtu ambae ni Matured katika kazi ya ukufunzi, ndio maana tunawaona makocha kama Sam Alladayce (Big Sam) na wengine wanazidi kujijengea heshima ya kuzinusuru klabu tofauti kwenda championship kutokana na uzoefu waliokua nao ndani ya premier league, sina maana kwamba kocha mzuri anaepaswa kufundisha klabu toka EPL awe amewahi kufundisha klabu toka England, hapana ila awe na uzoefu hata wa kutoka ligi zingine.

Jina la aliyewahi kuwa nahodha wa Arsenal Mikel Arteta ambae kwa sasa ni kocha msaidizi wa klabu ya Manchester city ndio linalotajwa zaidi kupewa Majukumu ya kuwa kocha mpya wa klabu hiyo, kitu ambacho kimekua kikiwagawa wapenzi wa soka wengi kimawazo, wapo ambao wanaona anastaili, wapo ambao wanaona bado hatoshelezi kuongoza klabu kubwa kama ile pia wapo ambao mawazo yao yapo neutral yaani wanamtaka yoyote kikubwa ni kuonja ladha ya kocha mpya tofauti na Mzee Wenger.

Arteta ana miaka 36 mpaka sasa, kiumri bado ni kijana anahitaji muda mwingi wa kujifunza kuliko kuonyesha kile kidogo alichojifunza kwa muda mfupi, kwani aliitaji kua assistant coach kwa miaka isiyopungua mitatu kutoka sasa au kuwa kocha mkuu katika ligi zisizo na ushindani kama alivyo Fanya Patrick Vieira kule Marekani, Steven Gerrard (Rangers) mapema mwezi huu nchini Scotland au Ryan Giggs alipoamua kuchukua jukumu la kufundisha timu ya taifa ya Wales maana national team hakuna presha kubwa sana kama ilivyo kwenye klabu, Itakua ni lahisi kuwaona wakina Steven Gerrard, Ryan Giggs, Patrick Vieira na wengine wanakua makocha wazuri kwa baadae kuliko Mikel Arteta endapo akaamua kuchukua majukumu yakua kocha mkuu wa Arsenal katika kipindi hiki.

Premier league sio ya majaribio ni bora akapewa kocha mwingine yoyote aliyeprove ubora wake katika ligi nyingine kuliko kumpa Arteta timu ambae bado anahitaji shule zaidi, Arsenal wasije tukaanza kumkumbuka Wenger licha ya kukaa miaka zaidi ya kumi bila kuwapa ubingwa EPL.
 
hizo bado ni tetesi tu, mimi bado nasisitiza muda ni hakimu mzuri....tusubiri
 
ila hili la france kumpiga chini LACAZETTE na kumchukua giroud NAMPA heko sana kocha si kwa utumbo ule ambao laca ametufanyia ngoja aekwe rizevu kwanza akae ktk kochi aone wanaume wanavyopambana
 
ila hili la france kumpiga chini LACAZETTE na kumchukua giroud NAMPA heko sana kocha si kwa utumbo ule ambao laca ametufanyia ngoja aekwe rizevu kwanza akae ktk kochi aone wanaume wanavyopambana

Duh imebidi nicheke tu hakuna namna sasa kati Lacazette na OG nani ni bingwa wa kufanya utumbo?Ila hata dogo Martial kaonja joto ya jiwe ingawa naona kama wamemfanyia sivyo.
 
Kama Arsenal inahitaji kocha kijana wachukue Julian Nagelsmann wa Hoffenheim (ana miaka 30).
Kama Arsenal inahitaji mchezaji wa zaman wa Arsenal basi afadhali Henry au Vieira.
Kama inahitaji kocha mzoefu basi Allegri anafaa.
Kama inahitaji kocha mwenye mafanikio ya haraka itapendeza wakikomaa na Luis-Enrique.
Kama Arsenal ina hitaji bora kocha ilimradi liende basi watuletee Arteta.
 
Jana Alhamis Arteta kafanyiwa usaili na Board ya Arsenal na leo watamfanyia pia Thiery Henry aka "Vava Voom Chogo"
Kama vipi wawekwe wote Vieira, Henry na Arteta wasaidiane na kina Bould na Lehman
 
Arsenal ina wakati mgumu sana kupata manager ambaye atatuvusha katika dimbwi la kuwa mediocre team kwa miaka mingi, Wenger alikuja na kufanya kile alichoweza, kipindi cha Wenger tumepitia mengi kama timu, tumeweka records nyingi lakini pia tumeweza kuchezea kwenye uwanja mkubwa zaidi hivyo mapato ya timu kuongezeka. Alichofanya Wenger ni kuimarisha timu kimapato Ila alishindwa kutengeneza timu ya kushinda makombe makubwa, tangu 2006 CL final hatujawahi kufika zile heights tena.


Binafsi naamini Arteta, Henry au Vieira ni daraja moja la makocha hasa katika uzoefu. Je, arsenal board wanaenda na uzoefu, wanataka cheap au consistency? Pundits wengi wanaamini arsenal wanaangalia consistency na umri wala sio proven manager. Uzoefu wa Arteta kwa miaka miwili hautoshi kuwa strong candidate kuongoza timu kubwa kama Arsenal, likewise Henry au Vieira.

Lakini je, Arsenal wanakubali kuwa na budget ya kuleta big spenders kama Ancelotti, Allegri au Enrique? Hao ni big spenders, na kwa mpira wa kisasa huwezi kukwepa "spending big", if you want to win big, you've got to spend big and wise, ndio maana RM na Barca hawashuki kimafanikio, they spend.

Sisi ni mashabiki, tunapiga vuvuzela hata ziwa Tanganyika halivuki lakini tunaitakia mema timu yetu. Tusijemaliza msimu tukiwa nafasi ya 16.
 
Jana Alhamis Arteta kafanyiwa usaili na Board ya Arsenal na leo watamfanyia pia Thiery Henry aka "Vava Voom Chogo"
Kama vipi wawekwe wote Vieira, Henry na Arteta wasaidiane na kina Bould na Lehman

Sidhani kama mzee wangu Bould atabaki maana baada ya AW kuondoka kuna vigogo wawili tayari washapoteza ajira alianza kit manager ambae amekua Arsenal muda mrefu akafuata Head of medical service Colin Lewin ambae amefanya kazi 23 years nahisi wameamua kuanza upya ni vema Bould akamfata AW au atafute hata timu ya kawaida tu apumzike.
 
Back
Top Bottom