Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Well, sio sisi tuliotaka kucheza na hawa BATE, mpirani unacheza na timu uliopangiwa nayo, Reserve team yetu kama kawa inafanya kweli...
COYG
 
Ft
Arsenal 6-0 Bate baritov
12 shots on target
Tuko vzr mno
Tunasubir Sunday na Soton
 
The teams who will now play in the Europa League:
1f1e9_1f1ea.png
Borussia Dortmund
1f1e9_1f1ea.png
RB Leipzig
1f1ee_1f1f9.png
Napoli
1f1f5_1f1f9.png
Sporting CP
1f1f7_1f1fa.png
CSKA Moscow
1f1f7_1f1fa.png
Spartak Moscow
1f3f4_e0067_e0062_e0073_e0063_e0074_e007f.png
Celtic
1f1ea_1f1f8.png
Atletico Madrid
 
Jack Wilshere na Theo Walcott wanatumai kwamba meneja wa Arsenal Arsene Wenger atafurahishwa kiasi cha kuwatumia kwenye mechi baada yao kucheza vyema sana Alhamisi.
Walciheza vizuri sana mechi ya Europa League ambayo walishinda kwa mabao mengi dhidi ya Bate Borisov.
Wawili hao hawajapewa nafasi ya kucheza kikosi cha kuanza mechi Arsenal katika Ligi ya Premia msimu huu, lakini wote wawili walitikisa wavu na kusaidia Arsenal kulaza Bate Borisov 6-0 na kumaliza mechi za Kundi H kwa ushindi.
"Kuna ushindani mkali unapokuwa unachezea Arsenal. Tufanya kadiri ya uwezo wetu kumfanya meneja ajikune kichwa akijaribu kuchagua wachezaji wa kutumia," Walcott amesema.

Wilshere, aliyefunga bao lake la kwanza tangu Mei 2015 aliongeza, "Jambo tunaloweza kufanya tunapopewa fursa na kumfanya meneja ajikune kichwa."
Arsenal walijiweka kifua mbele kupitia Mathieu Debuchy, kisha Walcott akafunga akifuatiwa na Wilshere.

Beki wa Bate Denis Polyakov alijifunga kutokana kwa krosi ya Walcott kipindi cha pili kabla ya Olivier Giroud kufunga mkwaju wa penalti baada ya Nemanja Milunovic kumwangusha Walcott.

Mohamed Elneny aliongeza la sita baada ya kupokea mpira kutoka kwa a Wilshere.
Baada ya Arsenal kulazwa 3-1 na Manchester United nyumbani wikendi, ilikuwa fursa kwa baadhi ya wachezaji waliowekwa pembeni kung'aa.
Wenger alifanya mabadiliko 11 kwenye kikosi chake kilicholazwa na United kwa mechi hiyo ya Alhamisi.
 
Back
Top Bottom