Arsene Wenger amedokeza kuwa anaweza kuhamia kwenye ukocha wa timu za taifa atakapomaliza kibarua chake Arsenal
Mkongwe huyo wa miaka 68 amebakiwa na miezi 18 kwenye mkataba wake Emirates na amekuwa akihusishwa na tetesi za kuinoa Uingereza.
Inafahamika kuwa Shirikisho la Soka Uingereza lilikuwa likitaka kumpa kibarua Wenger baada ya Roy Hodgson kujiuzulu kufuatia Uingereza kutolewa michuano ya Euro 2016, lakini Mfaransa huyo alitaka kuendelea na soka la klabu.
Inasadikika kuwa Paris Saint-Germain ndiyo klabu ambayo angeenda kuinoa ikiwa ataendelea na ukocha atakapoondoka Arsenal, lakini alipoulizwa kuhusu uwezekano wa timu ya taifa, alikiambia beIN SPORTS:
"Huenda, naam nitafanya kazi hiyo lakini kwa sasa napenda kazi za kila siku za maisha ya kwenye klabu.
"Ladha halisi ipo hapo. Wiki nne tano [kwenye michuano] ni uzoefu tofauti. Lakini naamini uzoefu wa kuinoa klabu ni kazi ya kila siku.
"Siwezi kuwa na nguvu za mwili kufanya hivyo kila siku, kwa hiyo naweza kufanya hivyo [kuinoa timu ya taifa].