Wenger atoa Onyo kwa Chelsea.
Arsene Wenger amewapongeza Chelsea kwa kutwaa Ubingwa wa EPL lakini amewaonya kwamba msimu ujao hautokuwa rahisi hasa ikizingatiwa kwamba watakuwa na mashindano ya UEFA pia.
The Blues wametwaa taji la pili la EPL ndani ya miaka mitatu bila ya kucheza Ulaya msimu huu na wanaweza angalau kumaliza juu kileleni kwa tofauti ya pointi 12 dhidi ya Gunners ambao wenyewe bado wanapigania kumaliza nafasi nne za juu.
Wenger anaamini kwamba timu kama Real Madrid na Bayern Munich wapo imara sana Ulaya kwasababu hawalazimiki kucheza katika kiwango cha juu sana katika ligi za nyumbani kupata matokeo baada ya Gunners kuondolewa hatua ya 16 katika mikono ya Wajerumani.
Kuelekea mechi ya EPL siku ya jumanne dhidi ya Sunderland Wenger amesema," Chelsea wamefanya vizuri. Hongera zao."
"Lakini katika misimu miwili iliyopita timu ambazo zilikuwa hazichezi Ulaya zimetwaa taji la EPL"
"Utakuwa msimu tofauti kwasababu watalazimika kucheza Jumamosi - Jumatano - Jumamosi kwasababu ya mechi za UEFA."
"Nahisi nchini Hispania, Real Madrid wanaweza kushinda mechi wakicheza katika daraja la wastani kuliko Uingereza. Labda pia ni wazuri kuliko sisi."
"Bayern pia ni sawa na Madrid - Wanatawala ligi ya Ujerumani kwa urahisi sana."