Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

2692.jpg

Alexis Sánchez celebrates scoring one of his hat-trick in Arsenal’s 5-1 Premier League win over West Ham at the London Stadium.
 
5184.jpg

Arsenal’s striker Alexis Sanchez celebrates after scoring their second goal
 
3106.jpg

Arsenal’s hat-trick hero Alexis Sánchez makes off with the match ball after the game.
 
3035.jpg

Arsenal’s Alexis Sánchez scores their fifth goal to complete his hat-trick
 
Richard acha kupigazana kelele siku kama ya leo unatakiwa utafute zilipo shangwe uikimbize w'end,analeta link zake leo wakati WHU kafundishwa nini maana ya nguzo 5 za uislamu pale gheto kwake.

Tujiandae na mechi jumanne na FC Basel, halafu jumamosi ijayo tunacheza na Stoke City, halafu tutakwenda kucheza na Everton na baada ya hapo tarehe 18 December tutakuwa Etihad kucheza na Man City (Aguero na Fernandinho nje).

Tutafunga mwaka kwa kucheza na West Brom, Emirates tarehe 26 boxing day.
 
4544.jpg

Winston Reid’s glum look sums up the feeling as the Hammers’ are on the wrong end of a hammering.

Bila shaka hata huu uwanja NI TATIZO jamaa wanaona kama bado wako AWAY

kucheza ground mpya nayo huwa shida.....angalia spurs WEMBLEY alivyogaragazwa UCL msimu huu

Next season Chelsea na Spurs watakuwa nje ya viwanja vyao walivyozoea kupisha upanuzi mkubwa wa Stanford bridge na White harte lane

nadhani hata arsenal Highbury walikuwa wameizoea sana....mpaka leo haijawezekana Emirates ikawa Fortress kama Highbury
 
Wazo la kiufundi juu ya madai kwamba Arsenal wanataka kumsajili Dimitri Payet.

627392436.jpg


Payet leo hakuwa katika hali yake ya kawaida ile ya kupiga chenga za maudhi na kufungua vyumba kwa wachezaji wenzie.

Alianza mchezo kwa kumtumia vizuri mchezaji wa pembeni Manuel Lanzini lakini Lanzini na wacheaji wenzie hawakumshirikisha sana Payet hivyo kumuacha peke yake yaani akawa "isolated".

Lakini muda mrefu Payet akibanwa na khasa alipowekwa chini ya uangalizi na Granit Xhaka na kushindwa kufurukuta kabisa.

Lakini baadae alipoingia Andy Carroll ni pale alipopiga mpira wa adhabu na Carroll akauweka kimiani na hivyo kuwa ni "assist" kwa Payet.

Kwa kuwa Gabriel alikuwa akipanda mara kwa mara hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya pekee kwa Payet kuitumia kuisumbua ngome ya Arsenal lakini hakuwa na uwezo wa kubaini nafasi hiyo.

Je anaweza kuisaidia Arsenal?

Huku Santiago Cazorla akiwa majeruhi kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo, Arsenal wanaweza kujaribu kumsajili Dimitri Payet akiwa kama "attacking midfieder" kwa upande wa kulia.

Mesut Ozil leo alianza kwa kutoa pasi ambayo ilisababisha goli la kwanza kwa Arsenal. Lakini pia Alex Oxdale Chmbaerlain na Theo Walcott wote leo wameshiriki kwa ufanisi mkubwa kuchangia ushindi kwa Arsenal.

Hivyo pamoja na wachezaji hawa kuwepo bado wanasaidia sana kwenye eneo la kushambulia au attacking midfielders hivyo kufuta wazo la kumuhitaji Dimitri Payet ambae bado hajamfikia Santi Cazorla kwenye idara ya upishio wa vyumba na sahani za kufungia magoli kwa washambuliaji wake.

Uwezo wa kutoa pasi murua na mbinu za kutafuta kutoa pasi hizo ndiyo silaha kuu ya Santi Cazorla sifa ambayo Dimitri Payet hana.

Kwa hiyo basi, Arsenal hawana haja ya kumsajili Dimitri Payet na itakuwa ni upotezaji wa fedha huku Alexis Sanchez na Mesuti Ozil wakihitaji maboresho ya mishahara yao.
 
Back
Top Bottom