Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kama kawaida tushasahau....Wenger anajua!
Wenger in? Wenger out?

Wenger anachagua siku na wakati wa kuwapulizia perfume itokayo basaburi mashabiki, akiuachia kila aliyekuwa anasumbuliwa na msongo wa mawazo au maumivu ya moyo, hupata uzima wa dharura na kusahau yaliyopita. Wenyewe husema, yaliyopita si ndwele, .........

Conte anajutia kumfahamu Abrahamovic.

Conte atatufaa kwa Kilimanjaro Stars
 
Nimefurahishwa na backline ya the gooooons, huyu Mustafi anaweza kufanya clearances vizuri sana, nadhani anaanza kutengeneza combo nzuri sana na Laurent. Right & left back pia wamecheza vizuri.

Nadhani midfield ya Coquelin - Carzola ni nzuri kuliko Xhaka - Carzola. Labda jamaa hawajafahamiana vizuri, tuna options nyingi sana katikati.

Lastly, Iwobi anaifurahisha kila nikimuona akicheza. Very talented youngster.
Mkuu @Eli9 uzuri kwa sasa hata timu ipangwe vipi, bado sub kuna WATU. Huyu dogo IWOBI ana vitu flani kama Kanu, anajua KUUFICHA!
 
MECHI YA JANA NILICHOGUNDUA

1) Kante hamuwezi ozil tangu akiwa leicester jana kaburuzwa

2) ili umpite mustafi unatakiwa upite juu

3) bora aanze coquelin kuliko xhaka

4) chelsea beki aliyebaki ni zouma tu

5) jana hazard angecheza mechi chelsea ingeshinda

6) xhaka a.k.a pweza ndio mchezaji anayependwa zaidi arsenal kila akigusa mpira hata akiwa golini kwake watu wanamwambia shooot

7) ozil hata angekua amejifunga kitambaa usoni angecheza vizuri maana zile pasi za kupiga kushoto na kuangalia kufika kilikua kitu cha kawaida sana

8) baada ya messi yale magoli anashinda sanchezi tu

9) yule the flash (google it) hamuwezi bellerin kwa kukimbia

10) Arsenal imefuta uteja
 
Back
Top Bottom