Kwa wale tuliokuwa tunahoji kwa nn Xhaka na Perez wasianze katika mechi ya leo:
Xhaka ni mchezaji mzuri hilo halina shaka. Tangu akiwa Bundesliga na hata ktk Euro 2016 amedhihirisha hilo. Perez pia amecheza vizuri sana dhidi ya N. Forest juzi ktk EFL Cup.
Lkn tukirejea katika partnership ya Carzola na Coquelin ndiyo bora kwa upande wa Arsenal kabla ya kuumia kwa Carzola karibu nusu ya msimu uliopita na pia Coquelin kuanza kuandamwa na majeruhi pia.
Kwa hivyo, Wenger kumuanzisha Coquelin na Carzola hakukosea kwa maana ya mafanikio wawili hao waliyomletea tangu waanze kucheza pamoja.
Kuna wakati Wenger alitaka kubadili kwa kumchezesha Ramsey na Coquelin na Carzola kumpeleka pembeni. Matokeo hayakuwa mazuri ikabidi arejee kulekule kwa Coquelin na Carzola.
Kubadili partnership ya wachezaji wanaofanya vizuri tena katika mechi muhimu ni sawa na kubet suala ambalo hakuna kocha aliye tayari kulifanya.
Vilevile, Xhaka na Perez bado wageninwa BPL wanahitaji muda wa kuifahamu na kuendana na kasi na fiziki ya ligi. Kingine ambacho ni cha muhimu pia Arsenal wana mechi nyingi tu za EFL Cup, FA, BPL na UCL na hapa ndiyo kwanza msimu umeanza.
Kadhalika, kuna wachezaji kuchoka na kushuka kiwango mechi zinapochanganya. Hivyo, kuwa na wachezaji wengi au kikosi kikubwa ni muhimu sana inapofika kipindi hicho.
Mfano mzuri ni sasa baada ya kuumia Coquelin ktk mechi dhidi ya Chelsea, Xhaka kaingizwa kuziba nafasi yake. Na kadri mchezo unavyokwenda kunaweza kutokea marekebisho yatakayo hitaji mabadiliko kwa wachezaji ambayo yatamlazimu mwalimu kuyafanya.