Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Sio kuwabeza, ila ukweli lazima usemwe! Weak link leo ni mabeki wa kati Na Flamini wamechangia goli tatu za kizembe, na hasa Per! Sio kubeza, ni kusema ukweli! Point 36 tunazo na tuko juu ila sababu mojawapo ni kwamba timu kubwa kama chelsea na mancity hazifanyi vizuri mpaka sasa, kwao si kawaida ndo maana kwa siso tuko juu!
Tuendelee kuomba wasifanye vizuri ili tuchukue ndoo, ila msimu ujao bahati haitakuka upande wetu maana chelsea watarudi!
Nina hofu pia na Tottenham, wanakimbiza mwizi kimya kimya na hatujaenda kwao!

Umetaja Ozil na sanchez tu peke yao

na point 36 hiz tumezipata kwa kumpiga na City huyu huyu na hao wengine wameshindwa kuzifikisha so far let's appreciate our team's efforts, na tukubali league ni ngumu kila timu ni beatable

Flamini inafahamika sio mtu wa kutuvusha mbali ila by next week dirisha litakuwa open NEW DM ni lazima

ila kauli yako kuwa wachezaji woote ni useless ispokuwa Ozil na sanchez ni kupanic tu na mshktuko wa matokeo hamna kingine

Ubingwa kuona nan anachukua Sio sasa ni hukooo march ndio unaona huyu na huyu wanabeba....

historia iko wazi walio na 35+ points by christmass ndo tittle conteders so far naona City na Arsenal mpaka mwisho

atakayekuwa consistent atakuwa bingwa next may 2016
 
Ila Bournemouth sio wa kuwabeza si uliona Chelsea walifungwa kwao?

kila game ni ngumu....ila chelsea nao walikuwa ''GONJWA SANA"

na at least bournamouth wanafunguka wanacheza mpira itasaidia sana upande wetu...

afu vuta picha game ya Britania siku tukicheza na Stoke Walivyo "AGRRESIVE" mpira kama RUGBY

balaa tupu hiyo game sipati picha
 
Wacha 1 kwema hapa?Msikate tamaa ndiyo soka ndugu yangu kuna kushinda na kushindwa!Sasa ukipigwa 4 na Soton je ukija kwa Majogoo si zitakuwa 8 jamani?
 
Last edited by a moderator:
Wapi Wacha 1?? Bado yupo bize kufungua mabox au ameamua kujifungia kwenye box kukwepa hii aibu??? Tumemiss kicheko chako bhanaaaa
 
Last edited by a moderator:
Majirani mnaweza kuja kwetu kuazima maturubali huko kwetu misiba imekuwa mingi so watu hawaji sana kama wametuchoka flan hivi.
 
Mmm nina walakini na kuutazama mpira au kipigo kimekuchanganya mbaya

vipi kuhusu Nacho? ambae so far ni best left back pale EPL, Bellerin? unazungumziaje Peter Cech

Unasema nin kuhusu Kos? Santi? Coqeulin

Isiwe kikitokea kipigo tu mnadharau timu yenu yoote so far point 36 wamepata hawa hawa wachezaji..unaowatukana na kuwabeza

walioshusha wachezaji wa bei mbaya kama Manure wako wapi?an city ana Defeats 5 so far kwenye EPL

kubali tu ligi ni ngumu hii ni imekuwa haitabiriki kbs

Dont settle for less that will transform you into midcore level.
 
Seriously WATU NA MANENO YAO

Eti Arsenal wana tatizo la kufika kileleni Wamuone
DR Mwaka
 
Mimi bado naamini kwamba tatizo la Arsenal ni Kocha,,Wenger ni tatizo.Baada ya kikosi chetu cha ushindi kutawanyika,huyu babu hajawawahi kuumiza kichwa kutengeneza kikosi zaidi ya kutuletea Adebayo,,bendtner,,Giroud,,Czech na vilaza wengine wengi.Huyu babu utashangaa akikosa ubingwa msimu huu bado kuna wazungu wataongeza imani yao juu ya huyu mzee asieenda likizo wala kupumzisha akili yake iliochoka.
 
bado tuko vizuri....matumaini ya ubingwa yako pale pale, haya ni majaribu tu katika safari yetu takatifu
 
Nimekula, wameniudhi sana! Unajua unaweza fungwa ila bado ukaikubali timu sababu ya kuonyesha kupigana mpaka jasho la mwisho, ila sio leo!
Nimepewa za uso NNE hapa uso umeumika sioni vizuri.

Pole sana ndo soka hilo...
 
Kwa Arsenal hii ni lazima kuwaombea njaa maadui hasa Mancity, kwa miguu yetu pekee sisi The Gunners ni ngumu sana, hamna fighting spirit. LAZIMA TUSEME UKWELI, unafiki sio mzuri!
Nawe naona europa nayo inataka kukukimbia!

Sisi tuko kwenye mgomo baridi mpka yatimie ya #LVGOUT
 
Back
Top Bottom