Arsenal VS Bournemouth
Uwanja: Emirates
Baada ya kufungwa na Southampton goli 4-0 Arsenal ndani ya masaa 48 wanawakaribisha timu ya Bournemouth uwanjani EMIRATES.
Ni mechi itakayotoa mwelekeo wa timu yetu ambayo inalisaka kombe la ligi kuu ya Uingereza ikiwa inapewa nafasi ya kulitwaa kombe hilo ililolipoteza zaidi ya miaka 10 ilopita.
Katika mchezo wa jana baadhi ya wachezaii walionekana wanahitaji kupumzishwa Joel Campbell, Mathieu Flamini na Mertesacker walionekana wapo hoi.
Tusisahau kwamba ni wachezaji hawahawa pamoja na wenzao ndio wameivusha timu yetu hadi kufikia hapo tulipo ikizingatiwa kuna majeruhi kama Alexis Sanchez, Santiago Cazorla na wengine.
Nafikiri meneja Arsene Wenger bado anataka asilimia 100 kutoka kwa dream first II yake na ambayo ni juzijuzi tu waliifunga Man City.
Lakini jana Theo Walcott alionekana amepotea, Olivier Giroud akawa peke yake kule mbele na Mesut Ozil kwa kuwa amekuwa mpikaji na mtengenezaji mipira mizuri na kutoa msaada wa ushambulizi, Southampton wakaja na wazo la kumzuia kabisa asifanye yote hayo
Arsenal wakawa wamebanwa na Victor Wanyama akawa amemzidi Aaron Ramsey kwa nguvu, Southampton walikuwa wakicheza kama wapo kwenye fainali!
Sasa kwenye mechi ya kesho ningekuwa Wenger basi, Mertesacker, Ramsey na wangeanzia kwenye bench na nafasi zao zikazibwa na Gabby Calum Chambers na OX Chamberlain.
Hivyo timu itakuwa na wachezaji wapya kistamina na hivyo kutokusimama na kukaribisha mashambulizi ya mara kwa mara.
Hivyo timu ingekuwa kama ifuatavyo:
Cech, Monreal, Berrelin, Gabby na Koscielny,
katikati namba 6 Calum Chambers namba 8 Aaron Ramsey,
Kulia Theo Walcott
Kushoto Ox Chamberlain namba 10 Ozila na namba 9 ni Giroud.
Wachezaji wa akiba- Ospina, Gibbs, Mertesacker, Campbell, Iwobi na Reine Adelaide.
Ila kuendelea kuchezesha wachezaji ambao wamechoka bila kuwapumzisha hakutaisadia timu yetu na kelele za wale mashabiki uchwara za "Wenger Out", zitarudi maana sasa hivi wapo kimya na yule mjinga wao Pierce Morgan.
COYGs!