Arsenal wamewasilisha kwenye makao makuu ya UEFA, orodha ya wachezaji 25 ambao watashiriki kwenye mashindano ya kombe la klabu bingwa za Ulaya.
Orodha hio imepangwa katika sehemu mbili yaani A na B na Orodha A ina wachezaji 17 na orodha B ina wachezaji 7 ambao wana nyota ikimaanisha kwamba wao pia wachezaji walokuuzwa na Arsenal Academy yaani "Home Grown Players".
Meneja Arsene Wenger ameamua Joel Campbel abakie kwenye timu ili kuongeza idadi ya washambuliaji sita pamoja na wadogo wawili yaani Alex Iwobi na Chris Willock.
Pia Mathieu Flamini nae ameambiwa ataendelea kuchezea Gunners hadi mwisho wa mkataba wake.
Mechi ya kwanza ya Arsenal itakuwa ugenini mjini Zagreb kati yake na Dynamo Zagreb.
Ifuatayo hapo chini ni orodha kamili.
COYG!!!!