Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,382
- 10,951
Hahahaaaaaa,babu alizoea kubebwa na FA/marefa,wachezaji si ni hao hao toka misimu 3 illiyopita??
Hivi unafahamu makamu mwenyekiti wa Arsenal wa zamani David Dein (1983-2007) alikuwa pia makamu mwenyekiti wa FA kuanzia mwaka 2000 hadi 2004?!? Kipindi hicho pia ni makamu mwenyekiti na mmoja wa wamiliki wa Arsenal!! Baada ya mwaka 2004, Dein alichaguliwa kuwa mjumbe wa bodi ya FA kama mmoja wa wawakilishi wa vilabu vya premier league kupitia mgongo wa Arsenal, kuanzia 2004 hadi 2006. Kumbuka Dein amekuwepo kwenye korido za FA toka mwaka 1986 (kipindi SAF anachaguliwa kuwa meneja). Hiyo inaonyesha ni namna gani Dein alivyokuwa kigogo wa soka Uingereza, ilhali ni mmoja wa vigogo na wamiliki wa timu inayoshiriki ligi kuu!!!
Sasa kama FA ilikuwa inaibeba Manchester United, basi Dein alikuwa mpuuzi kupita maelezo. Maana naye alihusika katika kuibeba Man United huku timu yake ikiwa majanga matupu!! Maana kwa kipindi Dein yupo kwenye FA (kuanzia 1986) na Arsenal (kuanzia 1983) hadi anaondoka FA mwaka 2006, United ilichukua ubingwa wa ligi mara 9 huku Arsenal ikichukua mara 5 tu, huku Arsenal ikichukua ubingwa wa premier league (ligi ambayo Dein alishiriki kuanzisha) mara 3 tu! Hizo mara 9 za United ni za enzi ya premier league tu, na katika miaka ambayo Dein alikuwa kigogo wa Arsenal na FA kwa wakati mmoja.
Nyiye goons msiwe mnajiropokea tu vitu msivyovifahamu.