Muda bado mkuu.....Ndo kwanza dakika ya 25Leo vijana mbona hawapo mchezoni kabisa...
Mbona wananipa mashaka!!
Newcastle wanataka kutoka sare na wanacheza mtondo wa 4-3-3 na Arsenal wanacheza 4-3-2-1.
Arsenal wanashindwa kupenya ngome ya Newcastle ambayo imepanga kusumbua leo.
Lakini kutafanyika mabadiliko muda si mrefu.
Washambuliaji wa Newcastle Sisse na Ghoufran ndio wasumbufu kwa sasa kwani wanapenya kuipita back four.
Arteta ameshindwa kuendelea na mchezo na Alex Oxlade Chamberlain anaingia kuziba nafasi yake.
Cheick Tiote na Yohan Kabaye naona wameazimia kuvuruga kila mpango. Wanacheza kama wapo kwenye fainali!