Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Mimi sio Arsenal,ila UCL nikiangalia kihistoria na rekodi ya Wenger na anachosifiwa hususan na bodi klabu haifilisiki hajakosa UCL toka enzi zile za England anapitisha 2 alikuwa yeye na Fergie hadi sasa 4 bora hakosi,ni sawa na gem la leo kombe la mfalme Spain,toka nifuatilie mpira sijaona Atletico Madrid akimfunga Real Madrid tangu walipopanda daraja 2003,so nampa Real Madrid nafasi leo kuwa bingwa wa kombe la mfalme,hao Chelsea na Spurs kazi wanayo hasa Spurs uefa alhamisi inamhusu zaidi naona.
 
Thanx Arsenal...4 goals against FA cup winners si muchezo!! Sasa tusubiri karata ya mwisho against Newcastle!!

Nakusalimu tu.
Naona ulipotea kidogo.

Nakukumbushia tu mambo yalivyokuwa juma lililopita jijini Manchester.

Cc: Wacha1
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1368809416.345379.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1368809416.345379.jpg
    146.3 KB · Views: 28
  • ImageUploadedByJamiiForums1368809445.136062.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1368809445.136062.jpg
    86.8 KB · Views: 31
  • ImageUploadedByJamiiForums1368809464.363639.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1368809464.363639.jpg
    62.1 KB · Views: 30
  • ImageUploadedByJamiiForums1368809497.449249.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1368809497.449249.jpg
    64.6 KB · Views: 28
  • ImageUploadedByJamiiForums1368809512.714988.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1368809512.714988.jpg
    79.4 KB · Views: 31
  • ImageUploadedByJamiiForums1368809546.555864.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1368809546.555864.jpg
    71.5 KB · Views: 27
Last edited by a moderator:
Wakuu wa Gunners msiwe na wasi wasi na hawa mashoga wanaowashwa kwa kuweka mambo ya manure hapa, tunawatisha ki-soka ndio chababu hawabanduki hapa. Game yetu ya new Castle itakuwa kali sana na tegemea magoli kadhaa we are Gunners na hapo ndipo wanapoweweseka ... ...COYG.


BTW Summer imeanza mapema huku Alaska ... ..... ... ...
 
CL spot now in our hands.............

This is an act of desperation for the Goooonnneers! Badala ya kuongelea kuchukua ndoo ya EPL sasa topic year in year out imekuwa ni kupata chance ya CL ambapo hamjashinda hiyo ndoo hata Mara moja na hamtoshinda!
 
Karibu uwanjani , nikuulize tu unadaiwa humu kwenye chama yetu?
This is an act of desperation for the Goooonnneers! Badala ya kuongelea kuchukua ndoo ya EPL sasa topic year in year out imekuwa ni kupata chance ya CL ambapo hamjashinda hiyo ndoo hata Mara moja na hamtoshinda!
 
This is an act of desperation for the Goooonnneers! Badala ya kuongelea kuchukua ndoo ya EPL sasa topic year in year out imekuwa ni kupata chance ya CL ambapo hamjashinda hiyo ndoo hata Mara moja na hamtoshinda!

Huo ndo ushindi wetu,liver na spuds vipi??
 
Wakuu wa Gunners msiwe na wasi wasi na hawa mashoga wanaowashwa kwa kuweka mambo ya manure hapa, tunawatisha ki-soka ndio chababu hawabanduki hapa. Game yetu ya new Castle itakuwa kali sana na tegemea magoli kadhaa we are Gunners na hapo ndipo wanapoweweseka ... ...COYG.


BTW Summer imeanza mapema huku Alaska ... ..... ... ...
Nakutakia kila la heri kwenye mbio zako za kutetea ubingwa wako
 
Habarini gooners

Kama kawaida leo ni siku ya mwisho wa msimu wa 2012-2013 na tutasikia baadhi ya maneno kama timu Fulani inamwania “starlet” au “inakaribia kumnyakua” au “inamfuatilia kwa karibu” au Mchezaji Fulani anapenda chezea timu Fulani ni kawaida baada ya season kuisha
Hapa nitazungumzia kwa UHALISIA kinachotarajiwa msimu huu kwa klabu ya Arsenal

1. BAJETI YA USAJILI-mara nyingi huwa tumesikia kuwa season hii Arsene wenger ana bajeti ya £70 milioni na hapa kwa mara ya kwanza tangu Fabregas na Nasri waondoke Emirates 2012…Aliulizwa Jumanne iliyopita Wenger na waandishi juu ya David Moyes kwa rekodi zake pale Everton kwa kutumia bajeti kidogo akajibu “kwa kweli namkubali na naweza kukuonyesha hesabu zetu za uhamisho kwa miaka 16 na utaamini, watu wanasahau kuwa tulijenga uwanja kwa kukopa £360 milioni, hivyo tulilazimika kufanya kazi kwa kutumia bajeti finyu na kuwa katika Top level na hatukuwa na pesa kwakweli, nilikubali kubakia klabuni na nimepitia kipindi cha mpito, tumeibakiza klabu yetu katika Level ya juu (kushiriki CL) na hapa tulipo sasa tuko vizuri sana kifedha na tuna uwezo wa kupambana tena na timu tajiri, kipindi chote cha miaka 8 iliyopita kilikuwa kigumu na kinahitaji ujasiri wa hali ya juu” Hapa tunapata picha kuwa wakati wa nyuma pale ambapo tuliambiwa kuwa Arsene alikuwa na pesa ya usajiri haikuwa kweli hata kidogo, lakini kuanzia next season kutakuwa na mikataba minono ya Televisheni, mkataba mpya wa Fly emirates mpaka 2018 na mkataba mpya wa Puma unaoanza misimu miwili ijayo,.Arsenal Fc wana pesa za kuweza kununua wachezaji mahili msimu huu na kuendelea lakini nahisi hizo zisemazwo kuwa £70 milioni labda sio kweli bali ni uzushi wa Medias ianweza kuwa ni £50milioni



  1. WACHEZAJI WATAKAO ONDOKA
Kuna msululu nwa wachezaji watakao ondoka nao ni SEBASTIAN SQUILLAQI (mkataba unaisha), ANDREI ARSHAVIN (mkataba unaisha), LUKASZ FABIANSKI (mkataba unaisha), NICKLAS BENDTNER (yuko kwa mkopo Juventus) na huyu ametumia misimu miwili on loan na atauzwa sioni akirejea kama £4milioni au £5milioni zinatosha kama ada yake kama hakuna mteja mkopo tena kwingine, ANDRE SANTOS (yuko Gremio kwa mkopo) atauzwa kama sio kukopeshwa kwingine,Park chu young (Mkopo Celta vigo) hali yake kama ya Bendtner na Santos, JOHAN DJOROU (mkopo hannover 96) wenger kapoteza hopes zote kwa mswisi huyu atauzwa, DENILSON PERREIRA (mkataba unaisha), BAKARY SAGNA (mwaka mmoja umebakia kwenye mkataba wake) kuna dalili asioendelee kuwepo na kurejea kwao ufaransa, FRANSIC COQUELIN/EMMANUEL FRIMPONG (hapa itategemea yupi timu itataka kumbakisha ila mmoja tauzwa), GERVINHO (huyu naumia kichwa) kama atabaki au kuuzwa na bet atauzwa kwani amekuwa na mixed perfomances na yuko inconsistent sana,MAROANE CHAMACK (mkopo west ham utd) atarejea ufaransa…kama arsenal awatawauza na kuwaondoa hao si chini ya £10-15 milioni zitapatikana aidha kwa kuuza au kusevu mishahara ya wachezaji hawa.




  1. WACHEZAJI WANAOWEZA KUSAJILIWA

A.
Golikipa- msimu huu Arsenal lazima wanunue kipa mpya mzoefu wa kumpa presha Szczesny kwani dogo huyu ana mchanganyiko wa performance yaani hatabiriki mfano. Rene Alder,Julio Cesar, Simon Magnolet, Michel Vorm, Victor valdes wametajwa kuhusishwa na Arsenal.

B. Beki wa kati-kuondoka kwa Squillaqi na Djorou Arsenal inabakia na mabeki 3 wa kiwango cha juu na msimu ni mrefu na mechi ni nyingi at least uwe na mabeki 4-5 wa kiwango cha juu, Ashley Williams (kapteni wa Swansea) yuko na mazungumzo ya kina na Arsenal na anapatikana kwa £8 millioni

C.
Kiungo mkabaji-hii nafasi ilitakiwa kuimarishwa hata kabla Song hajaondoka na baada ya Song kuuzwa Arteta amejitahidi kuziba lakini sio (natural) position yake aliyoizoea, hapa kocha anatakiwa atafute mbadala mapema na hatuwezi jua atatokea wapui mchezaji huyu kwani nani alimjua NACHO MONREAL kabla hajatua arsenal?

D. Mshambuliaji-Usajiri hautakuwa na maana kama Arsena hawatasajiri striker (goal poacher) at least wa kufunga magoli 25 kwa msimu kama ilivyokuwa kwa RVP msimu wake wa mwisho pale London, Habari zinawahusisha na STEVAN JOVETIC (fiorentina), HIGUAIN (Real madrid) mpaka WYNE ROONEY (japo sidhani kama wataweza mlipa mshahara wa £250,000 kwa wiki)

E. Beki wa kulia-kama Sagna ataondoka nafasi itazibwa wanaotajwa ni SEBASTIAN CORCHIA na LUKASZ PISZCZEK hapa najiuliza Malaga hawana beki wa kulia watuuzie? Hahaha haaa

Bado na matumanini ya kurejea wachezaji chipukizi kama Rio miyaichi (wigan mkopo), Joel Campbell (Real Betis na Serge Gnabry, Miguel Ignas kushindania namba kama akina Gibbs na Jenkinson walivyofanya. Naweza kuwa sahihi au nimekosea kwani haya ni mawazo yangu lakini naona Arsenal kuanza kushindana tena kama Arsene atafanya vizuri sokoni na uzuri msimu huu hatupotezi key players kama miaka ya nyuma

CC: Wacha1 Ulimakafu Katavi Viper BAK MwafrikaHalisi Balantanda Richard na wengine
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kashengo salaam,

Upo spoton na mawazo yako.

Kabla ya Arsenal kwenda safari za maandalizi huko bara la Asia watathibitisha usajili wa wachezaji wawili watatu hivi.

Lakini mpaka sasa ni mchezaji mmoja tu ambae anaweza kutangazwa kukamilika usajili wake lakini ni mshambuliaji mdogo kutoka France aitwae Yaya Sanogo, ambae anachezea timu ya Auxerre.
 
Wakuu wa Gunners mambo yako mswano kabisa, New Castle wakijitahidi sana tutawafunga goli moja tu. Wakilegea inabidi walete kapu tujaze magoli khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.

BTW Serena kesha fanya mambo yake pale Rome anakabidhiwa kikombe anajaribu kuongea kitaliano khe khe khe kheeeeeeee bado tunamsubiri Rafa ammalize Fedex waswiss leo mtanichukia shida moja mtanange wa Gunners nao unaanza wakati huo huo, lakini si mbaya tutahabarishana tu ... ..... ... ...COYG
 
Nakutakia kila la heri kwenye mbio zako za kutetea ubingwa wako

Njoo uangalie mpira wewe chichi hatununui mechi wala kutoa envelopes kama kababu Fungie ... .. khe khe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Team News

Mikel Arteta hatacheza leo kutokana na kuwa majeruhi, na Jack Wilshere atacheza badala yake ingawa itabidi adungwe sindano ya kuondoa maumivu.

Olivier Giroud nae anarudi kwenye timu akiwa amemaliza kifungo cha mechi tatu baada ya kupewa kadi nyekundu kwenye mechi na QPR.

Newcastle wana majeruhi wengi sana Cheick Tiote ambae anaweza kucheza baada ya kuumia msuli na wengine Davide Santon, Steven Taylor, Moussa Sissoko, Massaido Haidara, Ryan Taylor, Haris Vuckic , kipa Tim Krul na mshambuliaji Shola Ameobi.

Hivyo kama Giroud ataanza basi Lukas Podolski nae atapisha na timu itakuwa na Szczesny, Sagna, Gibbs Mertesacker na Koscielyn, kiungo- Wilshere, Ramsey na Rosicky mbele yao na kwenye ushambuliaji ni Giroud na Walcott.

Au Rosicky anaweza kumpisha Podolski na akaja kipindi cha pili.

Kwa upande wa safu ya mabeki nadhani hakuna mabadiliko labda mtu aumie kabla mpira haujaanza.
 
Update:

Confirmed First XI kuanza dhidi ya Newcastle.

Mikel Arteta anacheza na timu ni kama ifuatavyo,.

Ni timu ileile iliyoanza dhidi ya Wigan.

Arsenal:

Szczesny, Sagna, Gibbs Mertesacker na Koscielyn, kiungo- Arteta Ramsey na Rosicky mbele yao Cazorla na kwenye ushambuliaji ni Podolski na Walcott.

Newcastle Utd:

Harper; Debuchy, S.Taylor, Coloccini , Yanga-Mbiwa; Tiote, Cabaye, Gutierrez; Ben Arfa, Cisse, Gouffran
 
Dakika zaidi ya kumi zimeenda na kila timu inaonekana inamiliki mpira 50-50.

Newcastle imejaribu shuti moja na Arsenal pia moja.

Bila kusahau mwamuzi ni Howard Webb kutoka kusini mwa wilaya ya Yorkshire.
 
Back
Top Bottom