Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Dakika ya 30 inakwenda na ngome ya Arsenal ipo kila mahali na hawajipangi vizuri.

Ni beki mmoja tu mpaka sasa ambae hajafanya makosa nae ni Kieran Gibbs.
 
Duuh sijui kama tunapona, everton nao washajipatia kagoli kao, yaani mh
 
kwa kweli roho imekosa uvumilivu wa kuiangalia hii mechi leo, naombeni tu mnitaarifu leo wamevaa jezi za rangi gani
 
Bacary Sagna ameanza kumdhibiti Suarez na hivyo ndiyo anavyopaswa kufanya.

Dakika inaenda ya 39
 
Nafasi ya timu yetu ya Arsenal kucheza Champions League mwakani ipo mashakani.

Wenger anaagiza wachezaji wacheze mpira ambao hawajawahi kuucheza maishani mwao.

Kuna hasara kubwa itakayoikumba Arsenal ikiwa itashindwa kufuzu kucheza CL zikiwemo zile paundi milioni 16 za kufuzu tu!
 
Nafasi ya timu yetu ya Arsenal kucheza Champions League mwakani ipo mashakani.

Wenger anaagiza wachezaji wacheze mpira ambao hawajawahi kuucheza maishani mwao.

Kuna hasara kubwa itakayoikumba Arsenal ikiwa itashindwa kufuzu kucheza CL zikiwemo zile paundi milioni 16 za kufuzu tu!
-

Mkuu wacha ishindikane kufuzu huenda ikawa ndio kitu kitakachowaamsha bodi na huyu mzee, timu imekuwa kama haina mwenyewe bana!- timu ambazo zipo mbele yetu kwa pointi nyingi bado zinajiimarisha kwa kusajili, sisi tunademadema hatusajili tuko serious kweli!!
 
Tatizo mojawapo la Wenger ni kuondoa wachezaji walio chini ya viwango na kuwabadilisha na wale wenye ubora wa hali ya juu, hili ndilo tatizo kubwa.

Tatizo lingine ni recruitment policy yake kwamba inakumbana na wachezaji wabovu kabisa ambao wametutia hasara kama Chamakh na Squillaci kwan ibado wanendelea kulipwa huku wakiwa hawachezi (Squillaci).

Ndio maana hata Brighton juzi wamemuulizia Squillaci.
 
Back
Top Bottom