Wakulu mambo vipi,
Kuna wale wapenzi ambao hudhani kwamba baadhi yetu huwa tunakimbia hapa jukwaani, jibu ni hapana.
Mimi kwa upande wangu huwa sikimbii hapa jukwaani bali huwa naingia uwanjani kushuhudia mwenyewe mechi za timu yetu.
Kwa kweli matokeo ya jana yameniacha na maswali juu ya maamuzi au judgement ya Wenger kuhusu usajili, upangaji na matatizo ya majeruhi kwa baadhi ya wachezaji wake ambao huonekana ndio wachezaji muhimu kwenye first XI yake.
Nimegundua kwamba Wenger anacheza kamari katika uendeshaji wa timu yake ikiwapo uwanjani.
Ntaelezea baadhi ya michezo yake ya kamari kwenye maeneo mbalimbali ya timu yake.
Kipa:
Hili eneo Wenger amekuwa hajaweza kusajili golikipa imara langoni na Wojciech Szczesny inasemwa kwamba wiki karibia sita sasa amekuwa akitumia dawa za kutuliza maumivu na kucheza hivyohivyo. Szczesny ni kipa mzuri lakini amekuwa akipata maumivu mara kwa mara.
Lukasz Fabianski nae bado ni majeruhi na huenda asicheze kabisa msimu huu. Kwahio hali hii inaiacha timu bila kipa namba 1 na namba 2. Ingawa kuna kipa namba 3 Vito Manone ambae atabaklia kuwa kipa namba 3 na hata uwezo wake ulijaribiwa katika mechi za mwanzoni mwa ligi lakini kutokana na mabeki kutojipanga vizuri Manone hajakaa vizuri.
Wenger ameacha kumsajili Julio Cesar kutoka Inter Milan ambae ameishia timu ya QPR, Alan McGregor kutoka Rangers ya Scottland timu ilipatwa namatatizo ya kifedha jambo ambalo lisingekuwa tatizo kwa Arsenal. Kuna kipa kama Jussi Jääskeläinen wa Bolton ambae amekwenda na timu hiyo daraja la pili, Paddy Kenny wa QPR ambae amekuwa kipa namba 2 wa timu hiyo.
Hawa makipa wangesajiliwa kama cover kwa namba 1 na 2 Arsenal isingemtumia Szczesny akiwa anacheza na maumivu bali ingesajili makipa wazoefu wenye ujuzi, hivyo kamari hii ya Wenger imefeli.
Beki wa kushoto:
Kieran Gibbs ndie beki wa kushoto wa Arsenal namba 1 na anapoumia, Santosa huchukua nafasi yake, lakini Santos hatazamwi kama beki imara sana. Katika mechi ambazo Arsenal imecheza bila Gibbs imekuwa ikipata shida sana kiuchezaji maana Wenger anaamua kumtumia Vermaelen kama beki wa kushoto na kwa kuwa Vermaelen si beki wa asili wa nafasi hiyo, anakuwa anachanganyikiwa na ndio mechi na Fulham magoli yakarudi.
Watani wetu Man U walipomuachia Fabio akacheze kwa mkopo kwenye nafasi ya beki wa kushoto pale QPR wakawa wamebaki na Patrie Evra lakini wakaenda kumnunua dogo aitwae Butner ambae huwa anacheza pale Evra anapokuwa majeruhi.
Kwahio hapa tena Wenger amekosea kwa kutomsajili mtu kama Leighton Baines wa Everton ambae angekuwa ama beki wa kushoto au kucheza pale Gibbs anapokuwa majeruhi, hivyo karata hii ya kumtegemea Vermaelen kama beki wa kushoto pale Gibbs anapokuwa majeruhi imefeli.
Sehemu ya kiungo:
Baada ya kumuuza Alex Song kwa Barcelona, Arsene Wenger angeingia benki na kutoa hundi ya kununua mchezaji wa aina ya Marouane Fellaini au angeongeza dau kwa Nuri Sahin ambalo lilikuwa likihitaji kusema iwe ni manunuzi kabisa na sio mkopo (kwa Sahin) na pia angedharau wasiwasi wa tabia ya ugomvi wa Yann M'Vila ambae ni mtukutu awapo nje ya uwanja.
Mzee Wenger akatia karata zake za kamari kwa Abu Diaby ambae inajulikana historia yake ya kuwa majeruhi pale anapopigwa kiatu cha uhakika. Na ni9 mechi na Liverpool ndio Diaby alionyesha kwamba akiwa mzima anawezakufanya vitu vya uhakika na baada ya hapo amerudi meza ya majeruhi.
Arsena haina mchezaji imara wa katikati wa kulinda ile "back four" na ukiangalia goli la kwanza utaona Michu akichukua mpira kabla ya kufunga hakuzuiwa na mtu yoyote. Na ni jana Wenger ameona umuhimu wa watu kama Gilberto au Makelele wa Chelsea. Huku tena ni kufeli kwa kamari za Wenger.
Nafasi ya mshambuliaji:
Wenger alipomuuza RVP alipaswa mara moja azibe nafasi kwa kumsajili mshambuliaji makini ambae angeweza kufunga magoli ya uhakika. Wazo la awali la kumnunua Giroud lilikuwa ni kwa kucheza kama mchezaji wa akiba kwa namba 9 wa first XI ambae angekuwa labda ni Llorente au Cavani.
Tokea Giroud aanze kucheza amefunga magoli 4 kwenye mechi 14 wakati RVP akiwa Man U amefunga magoli 10 kwenye mechi 15 ambazo amekwishacheza.
Pia Wenger anacheza karata ingine kwa kuwachezesha Podolski na Gervinho kwenye nafasi ya mshambuliaji namba 10 jambo ambalo jana limejionyesha kwamba halifai kwani pale anapoamua kumchezesha Giroud kama namba 9 basi Podolski na Gervinho ni mmoja wao tu ndie acheze kama namba 10 au 11 na sio wote maana wanakuwa hawajui wanafanya nini uwanjani na Gervinho jana amepoteza nafasi nyingi sana kipindi cha kwanza.
Kuna washambuliaji ambao wana uzoefu wa kimataifa na hasa kwenye ligi ya Uingereza kama Kevin Mirallas au Steven Fletcher wa Sunderland, Dimitar Berbatov wa Fulham na Jermain Defoe wa Tottenham Hotspurs. Defoe alikuwa akitaka kuhama timu ya Spurs na kama Arsenal wangemnunua akawa "first striker" basi angeleta ushindani maana angechezeshwa na Podolski na Giroud akawa anajifunza namna ya kumalizia mipira wavuni.
Kitendo cha Wenger kuamua kutosajili mshambuliaji na kutupa karata zake na kuamua kumtumia Olivier Giroud kama mshambuliaji na Gervinho na Podolski wawe wasaidizi wake, ni kamari ingine iliyofeli.
Sasa wapenzi wa Arsenal tunasubiri kuona kwamba Arsene Wenger anarekebisha makosa yake na kununua wachezaji namba moja katika maeneo niliyoyaongelea na ni hapo tu ndio Arsenal inaweza kushinda mechi zake za mzunguko wa pili.