Arrgghh! Mkwe!...

Mnanikumbusha ile hadithi ya mchina alikuwa haelewani na mama mkwe wake, akaenda kwa mganga akiomba dawa ya kumwua. Mganga akamwambia nitakupa dawa inayoua taratibu kwa sababu kama akifa ghafla utashtukiwa. Mganga akampa majani yaliyosagwa vizuri akamwambia nenda mpikie chakula kizuuuuuri umwekee na hii daya kidogo. So kila siku ufanye hivyo na wewe umwonyeshe upendo yaani uwe naye karibu na umpe kila akitakaco. Akikutukana wewe cheka ni sehemu ya dawa so hata akijakufa watu hawatakushtukia wewe sana sana watakuonea huruma.

Bi dada akaanza kazi ya "kuua" akawa anajipikilisha vinono, anamcare yaani kuliko hata anavyomcare mumewe au mamake mzazi. Baada ya mwezi wakawa marafiki wa kufa yaani wakawa wanapiga story kupita maelezo. Ikabidi bi dada arudi kwa mganga amwambie anaomba dawa ya kupunguza makali ya sumu alokuwa anampa mama mkwe kwa kuwa kwa sasa hataki tena kumpoteza amekuwa rafiki yake mkubwa. Mganga akamwambia wala ile haikuwa sumu ni vitamins tu na kilichobadilisha tabia yake ni atitude yako na upendo na kujali unakompatia so endelea tu kuishi kwa furaha na rafiki yako.

So sometimes na sie wanawake tunapaswa kuangalia attitudes zetu towards wamama hawa. Ingawa nakiri wapo wale ambao hawapendeki yaani hata ufanye nini umlambe miguu kila asubuhi kama ishara ya kumshukuru kwa kukuzalia chema wapi.......atakubetulia mdomo. Mie huwa naangalia sana movie za kinigeria hasa zile za Patience Ozokwor "Mama Gee". akiamua kucheza kama mama mkwe mwenye roho mbaya huwa ananimaliza kabisa. But najifunza mengi

...MwanajamiiOne hili somo nimelipenda sana, busara tupu mydear, thanks. Hawakukosea waliosema " 'adui yako' mpende" au " 'mchawi' mpe mwana amlee!"

kaka Mbu umeniuliza chanzo cha mvutano, ni vijimambo vingi sana katika kutaka kuingilia mambo yangu ya ndani, na iliponitibua zaidi ni wakati nilipokofofishana na mr kwa kutaka niache kazi, baada ya kukosana amani ndani kwa karibia miezi 6 nikaja ambiwa chanzo ni mama yake kumshikia bango mr kwamba natakiwa niwe mama wa nyumbani, hilo tuliliongea na mr na tukasuluhisha kila kitu, baada ya hapo sasa mama akaanza kwamba cmtii mume wangu coz akitoa maamuzi ndani siyafatilii, hapo tulishaongea na mr kila kitu kuhusu mama, na akanipa support kubwa sana baada ya ule utata uliotokea, bac kwasasa support yake ndio inanipa moyo.

...Nyamayao, shukran kwa ufafanuzi murua na hitimisho zuri sana.
Nami nimejikumbusha hekima na busara aifanyayo mumeo hapo, hiyo support anayokupa.
Hata kama Mume mtu 'atauma akipuliza', so long as mama mzazi na mke watajiona wanapewa support, migogoro ya aina hii itapungua tu.

Huenda zile simulizi za busara; "kati ya baba, mama, mke na mwana nimuokoe nani?" pia zililenga kutatua migogoro kama hii :thumb:

 
Kama ni upendo wa mama kweli, mbona wamama hawasumbui ndoa za binti zao kama wanavyoingilia za wakiume? Vipi wababa, hawana upendo? Mbona wababa hawasumbui ndoa za watoto wao wa kike wala wa kiume?

...ha ha, Kithuku umeuliza maswali ya msingi sana hapa, unless kuna wanaume wenye experience za 'kunyanyapaliwa' na mama wakwe zao,
kama mpo vidole juu!
 
tatizo mama mkwe kijana wake anapooa anashikwa na wivu. na hili husababishwa mwanaume kuwa karibu na mamaake ilhali ameoa.. hata mwanaume kupeleka siri za ndani kwa mamaake
 
inabidi kuwa wapole wasije kutuulia na wa watoto wetu na ndoa nyingi zinavurugiwa na mama mkwe wakishirikiana na mawifi ...... na nyie wanaume msioe muwakumbatie mama zenu.,,,,mtoto wa kiume yuko bize tu na mama shit
 
haya sasa hapo ni wanawake kweli sometime wamama wakwe wana bubu sana hata akiona umevaa umependeza oh hela za mwanagu,mnaenda kutembea mnapoteza hela wamama wengine,ila ndo mwanamke inabidi uwe na subira,uvumilivu ujue kua mwisho wa siku ni mama wa mumeo tu hata ufanyaje,je kwa wanaume nao wasiowaheshimu wakwe zao?wasioheshim mama mkwe au baba mkwe?mwanaume hata siku moja kusema jamani mama/baba hujambo?au kuna matatizo akiitwa waongee anasema hana muda eti ana wadharau wakwe zake wakati anaishi na mtoto wao?hivi inaleta heshima kweli hapo wanaume?mimi nina rafiki yangu mfano tosha mumewe anamtukania mpaka mama yake.hii inakuaje?
 
leo umeniamulia kunivunja mbavu....MJ1 kuna mambo unaweza kuyavumilia mengine hayavumliki kabisa, anataka akiwepo nyumbani nibadilike kimavazi, ooh mbona umebanwa hivyo huko ofcn kuna usalama, mara mama kwann unapenda kuvaa nguo za kuonyesha ulivyo kwann acvae kitenge, kitenge kuendea ofcn jamani MJ1, akiwepo kila jmc inabidi nijiendee ofcn kuepuka kero, jmc yenyewe hiyo navaa ka jeans nitaulizwa mama huko ofcn ukivaa hivyo mbona kama unawatenda vibaya wafanyakazi wenzio? yaani MJ1 hapana...lakini yeye huyo huyo kwa kulalamika kwamba mtoto wake wa kike anateswa na mama mkwe hajambo, yaani akianza kulalamika hapo hadi machozi, mie kirohoni nasema sawa kabisa!.
1. Usiyaweke moyoni, Upo wakati atajua makosa yake, usiyahesabu makosa yake, mpende kwa uvumilivu, bila kucount makosa, bila kujipndelea mwenyewe. Ifike wakati ujisikie fuiraha kqwa kuchangia kum[ponya mkweo.
2.Kaa ma mmeo, mweleze hali halisi kwa upendo na kwa hofu. onyesha ni jinsi gani unampenda mweo ambaye hapendeki, inaweza kuwa mmeo anachangia kwa kiasi fulani kumpa kichwa mkweo.
3. Onyesha upo kwako, huyo mumeo mzuri Mungu amekupa, alisha ondoka kwao na wwewe ulisha achana na kwenu. feel comfortable. Usionyeshe hata siku moja kuwa umekerwa na hilo tatizo kwani ikionyesha udhaifu wowote au hasira hapo ndoo mlango wa majungu mengine.
4. Ukiona mumeo hatandiki kitanda mwambie, ukiona hajatandika tena mwambie, ukiona hajatandika tena furahia na ipende style yake hiyo. Ipo siku atakushukuru kwa kumpenda kiasi hicho.
 
**Nyamayao,kweli yanauma sana lakini usilipize jema kwa mabayaa,kimya pia nacho kinasaidia,

**Tabu huo nao mtihani mkubwa kwa mume asieheshim wakwe zake!!!Mimi nimebarikiwa nimepata mama mkwe mzuri kesi ukimpelekea basi ujue atasimamia kwenye ukweli ni 2 kati ya mia mama wakwe wa hivi.:smile-big:
 
Nakuakikishai tatizo la in laws limeanzan miaka ya hivi karibuni zamani hakukuwa na matatizo haya kama ilivyo hivi sasa.kwa kifupi wadada siku hizi hawana heshima na adabu kwa wazazi wa upande wa pili na ndio maana tatizo la in law linawaathiri wao sana y not men?hawa wadada wakiolewa basi wanajifanya ndo kila kitu kwenye ukoo alio ingia bila kujua kuwa amekuaj nayae ni mgeni inabidi afuate baadhi ya taratibu alizozikuta ambazo hazihusiani na ndoa yake.mfano kama kijana alikuwa anasaidia familia yake inabidi uendeleee kumkumbusha kwenda kwao kupeleka vitu nk kwani asipotimiza hayo inaonekana we ndo unamkataza.pia wadada wamepandikizwa tabia ya kupenda kuiga uzungu wanasahau hapa ni africa wanataka haki sawa katika ndoa na kwa kuwa mama wakwe wengi ni wakizamani na hawako exposed na westrn culture wanakuwa wanaona watoto wao wa kiume wanaonewa, ni hayo tu kwa leo wasichana mbadilike ndoa zenu zidumu huku mkimtanguliza mwenyezi mungu katika ndoa zenu
 
Siku moja shangazi yangu alitupeleka kwa mwanawe wa kiume yaani binamu yangu. Kufika kwake mkwewe yaani mke wa binamu yangu alituletea vinywaji mimi na mdogo wangu. Shangazi yangu yaani mama mkwe wake hakupewa chochote wala kuulizwa nikupe nini? Nilichoka
 
Mbu Darling hii yote inafanyika kwa ajili ya upendo mkuu walio nao hawa wawili juu yako. Mama anakupenda sana na mke anakuzimia kupita kiasi ila tu ni wivu unaowasumbua...

Wajua mama siku zote mwanae wa kiume hamwoni kama amekuwa na wala haamini kama kuna mwanake mwingine (zaidi yake) anayeweza kukutunza na kukupenda kama yeye so kila anachokifanya mke mama anaona anakosea. Ndio maana utakuta wamama wengine wanafikia hata hatua ya kulazimisha kipikwe aina flani cha chakula kwa kuwa mwanaye anakipenda yaani huwa wako emotional sana kiasi cha kujisahau.

Iama ni mke asokuwa na busara atatumia nguvu nyingi sana kukuwini wewe from your mom na kumwonyesha mamako kuwa yeye ni MWANAMKE wa shoka wakati mke mwenye busara huwa anajitahidi kumvuta mkwe upande wake kwa kumfanya rafiki yake so that aweze kupata la hapa na pale juu yako.

Hapo kwenye Red MJ1 inabidi kuwa makini sana......
mimi nilikoolewa nilikuta kuna mwenzangu alitangulia kuolewa hapo na shemeji yangu. yule dada alijitahidi sana kuwa very close na mama mkwe wetu. mimi kama kawaida yangu busy, nafanya kile ambacho naona napaswa kufanya, yasiyonihusu hayanihusu. mwenzangu kila kitu anapeleka kwa mama mkwe, wanahadithiana kila kitu mpaka mambo ya ndani (ambayo mimi labda sijui ndo ushamba naona hayapaswi kuambiwa mama mkwe)
kilichotokea sasa, siku 1 nipo kwa mama mkwe, just the 2 of us (mimi na mama) si akaanza kumsema mke mwenzangu, kaanza kuniambia mambo ambayo hayapendi ambayo mke mwenza anamuhadithia mama.na akawa anasema, mi namshangaa sana....... sasa nikawaza ntamwambiaje mke mwenza asimsimulie mama mkwe? ila baadae nikamwambia tukiwa wote na mama.... alikuja na lishida lake, kishkaji nikamwambia "sidhani kama hili ni vizuri tukiliongea mbele ya mama, twende nje tukaongee mimi na wewe" ujumbe ukafika
 
Nafikir tatizo kubwa huwa ni conflict of interest

Exactly, the main problem i can see is, formerly, the man had the ability of sending some amount to his parents, after marriage, those services will automatically get reduced. If the parents and the new couple are not wise, expect problems!
 
Wanaoneana wivu, mkwe anaona kijana wake anatawaliwa na mkewe na sijambo jema. hukumke anaona anaingiliwa katika kutuoa ushauri kwa mumewe hivyo anahofu penzi lisije kupungua
 
myluv, ingekuwa kesi za mkwe hakutengewa chakula au kanyimwa mchuzi mbona hizo kesi wanaume wengi huzifumbia macho?
Hii kesi 'kwa mkichwa' bana,... Bibie povu linamtoka mdomoni!
Anyway,...hata kwa biblia imeandikwa kwenye methali 14:1 mke wa aina hiyo.
Na mashaka na huo ustahmilivu wa mume, ...pengine wengine huwaliza machozi mamazao wazazi 'walivyodhibitiwa' wake zao.
Kumtusi mama mzazi ili upendeke kwa mke si ndio laana zenyewe?

Kwa kuongezea..kama ni kunukuu maandiko Biblia hiyo hiyo kwenye kitabu cha mwanzo..utaona Mungu akiamrisha mwanaume na mwanamke kuwaacha baba na mama zao na kwenda kuanzisha maisha yao.

Mungu hakusema wakae na wazazi...alijua migogogro hii ya kunyang'anyana attention itatokea na kuvuruga amani.

Watu wanapooana ni busara zaidi kuwa na maisha yao bila kuwa na rejea kwa wazazi. Utaona katika jamii zote - waafrika, wahindi wazungu - kuna misemo mingi sana inayoashiria hali hii ya kutokuelewana baina ya mke na mama mkwe and vice versa.Hebu angalieni hii kwa mfano michache:

- Be kind to your mother-in-law, but pay for her board at some good hotel.- Josh Billing - hapa inaonyesha kabisa anavyojitahidi awe mbali na mama mkwe.

- I see by my mother-in-law's eyes when the devil takes hold of her.

- Well-married is when you have no mother-in-law and no sister-in-law.
--Spanish Proverb

Na hili la kutokuwapenda au kuelewana na wakwe siyo wanawake tu hata wanaume hutokea kutokuelewana na wakwe zao.
 
Kwa kuongezea..kama ni kunukuu maandiko Biblia hiyo hiyo kwenye kitabu cha mwanzo..utaona Mungu akiamrisha mwanaume na mwanamke kuwaacha baba na mama zao na kwenda kuanzisha maisha yao.

Mungu hakusema wakae na wazazi...alijua migogogro hii ya kunyang'anyana attention itatokea na kuvuruga amani.

Watu wanapooana ni busara zaidi kuwa na maisha yao bila kuwa na rejea kwa wazazi. Utaona katika jamii zote - waafrika, wahindi wazungu - kuna misemo mingi sana inayoashiria hali hii ya kutokuelewana baina ya mke na mama mkwe and vice versa.Hebu angalieni hii kwa mfano michache:

- Be kind to your mother-in-law, but pay for her board at some good hotel.- Josh Billing - hapa inaonyesha kabisa anavyojitahidi awe mbali na mama mkwe.

- I see by my mother-in-law's eyes when the devil takes hold of her.

- Well-married is when you have no mother-in-law and no sister-in-law.
--Spanish Proverb

Na hili la kutokuwapenda au kuelewana na wakwe siyo wanawake tu hata wanaume hutokea kutokuelewana na wakwe zao.

...pheeewww!

WoS nilivyokuelewa mimi, huo mtizamo wa wenzetu nchi za kimagharibi una hasara zake nyingi pia. No wonder (wazungu) majority huonana na wazee wao Christmas mpaka Christmas. Wazee wa kizungu wengi wanaishia lonely lives na 'foreign' care workers kwenye hizo Care homes.
Ndio hata wana misemo eti; "Be kind to your children, they are the ones who will choose a care home for you!"
 
wakwe mwatafutana nao nini, mimi sidhani kama naweza kuishi na mama mkwe, akae kwake akija kutembea ama matibabu siku mbili tatu sawa hapo nitamtreat like a queen, akizidisha anakuwa burden. Nikitaka kuongea naye nampigia simu, salamu tu kujuliana hali. Mengine kila mtu atunze mji wake!!!
 
Nyegelesha mambo ya mama mkwe kutompenda mkwewe hayajaanza hivi karibuni,yameanza enzi za mababu huko,ila sina hakika la kina baba kutoheshiu wakwe zao hili naliona siku hizi au kuna yeyote anaejua historia Kama hii zamani?
 
Back
Top Bottom