Arrgghh! Mkwe!...

MJ1 naona unaongelea ndoa yangu, shemeji yako alikudokeza kitu?...mhh mama mkwe wangu habebeki jamani, hayo ya kutoka out na kila m2 anarudi kivyake ndio tunayoyafanya na mr mama akiwepo huku, jamani mama mkwe wangu cjui nimbebe na mbeleko gani, lakini cku hizi najitahidi kumwacha alivyo japo bila support ya mr nicngeweza, kwa mama mwanae ni kama bado anatambaa vile, hakuna mtu anaeweza kumwonyesha njia ya maisha zaidi yake yeye....

Hahahaha Mamiie wala usihofu hayako kwako tu haya lol umenichekesha lakini.

Una afadhali nyamayao kuwa Prezidaa wako anamuelewa mama yake wengine hawataki kuelewa na badala yake wanaside nao basi we mwana wa kuja unanyanyaswa hadi unashika adabu mwishowe unaona upuuzi unauvua utu wewe na kuanza malumbano, nyumba waigeuza uwanja wa mashambulizi ya wake wenza.

Bora mwakaa mbali mbali mwee!!....................
Mi nakwambia bibi yangu naye alikuwaga na yake, basi akikutana na mwanae wa kike (aliyetoka kwa mumewe kisa mama mkwe) wanamsimanga mama yangu yaani nilikuwa naumia ila vikizidi (hapo nlikuwa darasa la nne at) nawapaka.. na kuwazomea kitoto hayooooo hayana kazi kazi kumsema mama yangu .... na wao walivyokuwa na akili zao wenyewe wanatoka wananikimbiza ah..Siku hizi ni best kweli na yule shangazi lol.
 
Duh nahisi mamkwe ilibidi anywee.... lol mama wakwe wana visa. Mie nina dada yangu (rafiki) mama mkwe hakumpenda tangu mwano alikuwa anataka mwanae asioe mnyambala ... basi alikuwa anapata shida huyo... kila siku mameno, mwaka wa kwanza akapata mtoto wa kiume ambaye kidogo amwondoe duniani kwa alivyo umwa, wakaamua na mumewe wapumzike angalau miaka minne kabla ya kumpata mwingine mama ntu ikawa ikila kukicha yuko ndani ya Sumry anakujaangalia kama tumbo la dada limevimba na mikashfa kibao yaani hapo hata mtoto hatatimiza mwaka!..ilipofika miaka miwili akamtolea uvivu akamwambia ..........O alikuwa tu mbishi angemwoa yule wa nyumbani sasa hivi angekuwa na watoto wawili!!........dada kwa hasira akamwambia ........wamekuwa mboga kuwa kila akija mgeni wachinjwa??....... Ikawa mwanzo wa bifu. Hadi leo hawaivi na dada tangu aolewe alikanyaga mara moja tu huko kwa mkwewe na sasa ni miaka 13

MJ1 umenimaliza mbavu zangu...wakati mwingine inabidi kwa kweli, mie cku hizi namwacha aseme tu wewee, mwanae akitoka job kamdaka wapo kibarazani ataongea na mwanae mpaka saa 5 ucku, ukiwa umeingia kulala kosa, kwanini hakusubiri muingie room pa1, hakuna kizuri kwake, ukipika utaambiwa umepika hivi nimevila sana nyumbani ningetamani kula hiki, hapo nilishamuuliza mama unajickia kula nn ananijibu chochote tu, kuna cku kweli nami ilibidi tu,alikuwa anakaribia kuondoka nikasema niende nae eneo moja linaitwa garisa akajichagulie mwenyewe vitu anavyotaka kwenda navyo nyumbani, tena kwa pesa yangu bila cent ya mwanae, tumerudi anachambua vitu vya kwenda navyo vingine akaviacha kwamba havitamfaa, kote huko alichagua mwenyewe bila mie kumpangia, nyumbani kamuona mwanae akanifanyia alichonifanyia, ktk mzigo wote kachagua vitu kama vi3 tu vingine havimfai lakini alivichagua mwenyewe....hapo uzalendo ulinishinda, kesho yake wakati anapanda shuttle na shuttle hiyo hiyo nikaviweka vitu alivyovikataa viende kwa mama yangu, kuanzia cku hiyo akija wala cjiguc kumuuliza hata kama ana mswaki.....
 
Hahahaha Mamiie wala usihofu hayako kwako tu haya lol umenichekesha lakini.

Una afadhali nyamayao kuwa Prezidaa wako anamuelewa mama yake wengine hawataki kuelewa na badala yake wanaside nao basi we mwana wa kuja unanyanyaswa hadi unashika adabu mwishowe unaona upuuzi unauvua utu wewe na kuanza malumbano, nyumba waigeuza uwanja wa mashambulizi ya wake wenza.

Bora mwakaa mbali mbali mwee!!....................
Mi nakwambia bibi yangu naye alikuwaga na yake, basi akikutana na mwanae wa kike (aliyetoka kwa mumewe kisa mama mkwe) wanamsimanga mama yangu yaani nilikuwa naumia ila vikizidi (hapo nlikuwa darasa la nne at) nawapaka.. na kuwazomea kitoto hayooooo hayana kazi kazi kumsema mama yangu .... na wao walivyokuwa na akili zao wenyewe wanatoka wananikimbiza ah..Siku hizi ni best kweli na yule shangazi lol.

leo umeniamulia kunivunja mbavu....MJ1 kuna mambo unaweza kuyavumilia mengine hayavumliki kabisa, anataka akiwepo nyumbani nibadilike kimavazi, ooh mbona umebanwa hivyo huko ofcn kuna usalama, mara mama kwann unapenda kuvaa nguo za kuonyesha ulivyo kwann acvae kitenge, kitenge kuendea ofcn jamani MJ1, akiwepo kila jmc inabidi nijiendee ofcn kuepuka kero, jmc yenyewe hiyo navaa ka jeans nitaulizwa mama huko ofcn ukivaa hivyo mbona kama unawatenda vibaya wafanyakazi wenzio? yaani MJ1 hapana...lakini yeye huyo huyo kwa kulalamika kwamba mtoto wake wa kike anateswa na mama mkwe hajambo, yaani akianza kulalamika hapo hadi machozi, mie kirohoni nasema sawa kabisa!.
 
MJ1 umenimaliza mbavu zangu...wakati mwingine inabidi kwa kweli, mie cku hizi namwacha aseme tu wewee, mwanae akitoka job kamdaka wapo kibarazani ataongea na mwanae mpaka saa 5 ucku, ukiwa umeingia kulala kosa, kwanini hakusubiri muingie room pa1, hakuna kizuri kwake, ukipika utaambiwa umepika hivi nimevila sana nyumbani ningetamani kula hiki, hapo nilishamuuliza mama unajickia kula nn ananijibu chochote tu, kuna cku kweli nami ilibidi tu,alikuwa anakaribia kuondoka nikasema niende nae eneo moja linaitwa garisa akajichagulie mwenyewe vitu anavyotaka kwenda navyo nyumbani, tena kwa pesa yangu bila cent ya mwanae, tumerudi anachambua vitu vya kwenda navyo vingine akaviacha kwamba havitamfaa, kote huko alichagua mwenyewe bila mie kumpangia, nyumbani kamuona mwanae akanifanyia alichonifanyia, ktk mzigo wote kachagua vitu kama vi3 tu vingine havimfai lakini alivichagua mwenyewe....hapo uzalendo ulinishinda, kesho yake wakati anapanda shuttle na shuttle hiyo hiyo nikaviweka vitu alivyovikataa viende kwa mama yangu, kuanzia cku hiyo akija wala cjiguc kumuuliza hata kama ana mswaki.....
................ Hahahahahahah duh huyu wako kiboko loh yaani hapa anataka kuonyesha kuwa umempa kidogo loh ndio wale ambao wakipewa chakula wanaficha then akija mtoto wake anasema kanyimwa chakula loh...... umenichekesha eti shuttle alopanda ndilo ulopakiza vya kwenda kwa mamako loh kweli alikutifua... Mimi sipati picha ningepata mama mkwe wa hivyo ningekondaje maana kusema siwezi loh............ I wish
 
Hahahaha Mamiie wala usihofu hayako kwako tu haya lol umenichekesha lakini.

Una afadhali nyamayao kuwa Prezidaa wako anamuelewa mama yake wengine hawataki kuelewa na badala yake wanaside nao basi we mwana wa kuja unanyanyaswa hadi unashika adabu mwishowe unaona upuuzi unauvua utu wewe na kuanza malumbano, nyumba waigeuza uwanja wa mashambulizi ya wake wenza.

Bora mwakaa mbali mbali mwee!!....................
Mi nakwambia bibi yangu naye alikuwaga na yake, basi akikutana na mwanae wa kike (aliyetoka kwa mumewe kisa mama mkwe) wanamsimanga mama yangu yaani nilikuwa naumia ila vikizidi (hapo nlikuwa darasa la nne at) nawapaka.. na kuwazomea kitoto hayooooo hayana kazi kazi kumsema mama yangu .... na wao walivyokuwa na akili zao wenyewe wanatoka wananikimbiza ah..Siku hizi ni best kweli na yule shangazi lol.
Jamani mie ctaki ........Mbu asijesema tumechakachua sred. but hatujatoka nje ya biti ati lol

Hapana nyamayao huyu wako hapana loh eti?? kitenge uvae kazini kama nakuona bidada....... na lemba kichwani hahahaha mi ctaki bwana ah. Ah wengine tulikwua na bahati kumbe?? mie nlikuwa nafanyiwa kutafutiwa swaga yaani asione mtu kapitisha hand bag za kisasa tena zenye majina ya madesign analo, ntawekwa mie na kupigiwa simu nije niangalie nikipenda ninunue...ah nlikula raha zangu jamani ndo hivyo tena haikuwa rizki lol. But she is my best friend ever.
 
MJ1 naona unaongelea ndoa yangu, shemeji yako alikudokeza kitu?...mhh mama mkwe wangu habebeki jamani, hayo ya kutoka out na kila m2 anarudi kivyake ndio tunayoyafanya na mr mama akiwepo huku, jamani mama mkwe wangu cjui nimbebe na mbeleko gani, lakini cku hizi najitahidi kumwacha alivyo japo bila support ya mr nicngeweza, kwa mama mwanae ni kama bado anatambaa vile, hakuna mtu anaeweza kumwonyesha njia ya maisha zaidi yake yeye....

...ddddoooooossshhhh!
Pole sana Nyamayao,...lakini naomba nikuulize hapo penye wekundu;
kwanini wewe Nyamayao umefikiria na kutamka hivyo?
Kitu gani kimekupelekea ku influence judgment yako kwenye hisia hiyo?
 
Hawa mama mkwe na mka mwana wanasumbuliwa na ugonjwa wa UKIRO. Wakipatiwa tiba hakutakuwa na ugomvi baina yao.

...ahaha! shukran Baba Mtu, lakini kuwa muwazi zaidi basi,..UKIRO ndio nini na fafanua maambukizi, dalili, tiba na hata kinga za 'ugonjwa huo?'
 
Duh nahisi mamkwe ilibidi anywee.... lol mama wakwe wana visa. Mie nina dada yangu (rafiki) mama mkwe hakumpenda tangu mwano alikuwa anataka mwanae asioe mnyambala ... basi alikuwa anapata shida huyo... kila siku mameno, mwaka wa kwanza akapata mtoto wa kiume ambaye kidogo amwondoe duniani kwa alivyo umwa, wakaamua na mumewe wapumzike angalau miaka minne kabla ya kumpata mwingine mama ntu ikawa ikila kukicha yuko ndani ya Sumry anakujaangalia kama tumbo la dada limevimba na mikashfa kibao yaani hapo hata mtoto hatatimiza mwaka!..ilipofika miaka miwili akamtolea uvivu akamwambia ..........O alikuwa tu mbishi angemwoa yule wa nyumbani sasa hivi angekuwa na watoto wawili!!........dada kwa hasira akamwambia ........wamekuwa mboga kuwa kila akija mgeni wachinjwa??....... Ikawa mwanzo wa bifu. Hadi leo hawaivi na dada tangu aolewe alikanyaga mara moja tu huko kwa mkwewe na sasa ni miaka 13

...ha ha! yaani MWJ1 umestahmili weee mwishowe umeamua kumwaga mboga,....kumbe kweli eeh mama wakwe wana visa?
Swali langu halijapatiwa ufumbuzi;

...Hivi, ni Kwanini?
Mbona kina dada/kina mama wengi wanamatatizo sana kimahusiano na 'mama mkwe?'
---Shida ni nini?---
Mbinu gani mbadala/muafaka huchukuliwa kusuluhisha/kuepusha gogoro hili la enzi na enzi?

 
Jamani mie ctaki ........Mbu asijesema tumechakachua sred. but hatujatoka nje ya biti ati lol

...la la la! ha ha ha!
hamjachakachua wala nini, ndio kwanza mmeweka msisitizo hizi kesi zipo na zinawahusu hata madada zetu mliopo hapa jf!
 
Mkuu Mbu ugomvi wa mama mkwe na mkamwana wake mara nyingi unasababishwa na vitu vingi sana.Mengi ameyazungumza MJ.1 hapo juu.Lakini kubwa kuliko vyote ni ile hali ya kumgombea mwanaume kati ya mama(anataka mtoto) na mke(anataka mume)na mara nyingi kwa sisi waafrika ugomvi huo husababishwa na material things kama vile pesa,nyumba,magari,na zawadi nyingine ndogondogo.

...Paka Mweusi, sasa narudi kwa post yako mkuu. Umesema kwamba ni mara nyingi hizi material things zinachangia 'msukosuko' baina ya mama mkwe na mamsapu, ni jinsi gani wewe Mwanaume utaweza kuepusha/kutatua mgogoro huo apart kwa haya uliyoyaandika hapa chini?

Binafsi nimeshashuhudia mke kaolewa hata hajamaliza mwezi anawaambia wifi zake msifikiri mna kitu hapa hata kama mume wangu akifa leo mali zote ni za kwangu.Na nimeshashuhudia mama mkwe anatamka wazi kuwa huyu mwanamke kaja kula hela ya mwanangu tu hapa,hiyo ni mifano tu ambayo nimeishuhudia ikitokea na inaweza kuelezea ni vipi ugomvi unapoweza kuanzia kati ya pande hizo mbili.
Ili kuweza kuweka mambo sawa kwanza mwanaume kama kichwa cha familia alitakiwa achukue hatua mwanzo kabisa kabla mambo hayo hayajaingia katika hayo mafacebook,inaonesha kuwa hapo situation ni critical kiasi cha watu sasa kupeana vijembe kama waimba taarab.Anatakiwa kwanza asiwe na upande wowote yaani awe neutral katika ugomvi huo asiwe upande wa mama wala mke,kisha awakalishe chini wote wawili ikiwezekana wawepo na watu wengine kama vile baba,wajomba,shangazi au yeyote anayeaminika ambaye umri unakaribiana na wa mama.Kisha kwa upole mwanaume ndio aanzishe mjadala ili kujua tatizo liko wapi kati ya mama na mke,na katika hilo mwanaume ajitahidi kurekebisha aina yeyote ya hasira au hamaki itakayojitokeza wakati wa mazungumzo hayo.Akiweza kufanikisha hilo atoe nafasi kwa waalikwa wa kikao hicho kuchangia mtazamo wao kwa tukio zima toka lilipoanza mpaka kufikia hatua hiyo.Baada ya hapo uamuzi ufikiwe kama vile kutoa onyo,karipio au adhabu kutegemeana na hali itakayojitokeza kisha pande zote mbili ziridhie kwa kusameheana na kushikana mikono.Likishindikana hilo basi inabidi kuwatenganisha kama uwezekano huo upo kisha kutafuta suluhu nyingine ambayo nitakueleza ukirudi kuniambia yameshindikana.

...Mkuu Paka Mweusi, kuwatenganisha una maana gani? Kwa kesi hii, Mke na mume wanaishi ughaibuni, na mama mkwe anaishi Nyumbani Tanzania

MUHIMU ni huyo jamaa asichelewe kuchukua hatua maana kuna msichana mbichi tu alipoteza maisha kwa njia ya utatanishi baada ya kuwa haelewani na mama mkwe wake na kila mtu alisema ni mama mkwe ndio kamroga,siombei hayo ila kuepusha balaa linalonukia ni bora jamaa akasimama imara na kutatua tatizo hilo,na asikosee kuzungumza na kila mtu peke yake maana waswahili walisema,msema pweke hushinda.

...loh, hapo kwenye suala la mama mkwe kusingiziwa kuloga nayo ni kesi nyingine hiyo. Binafsi nishakumbana sana na hizo kesi eti mama mkwe kaloga mke asipate ujauzito, au mtoto akizaliwa anakufa, au kuumwa umwa kwa mtoto, kwanini kila 'jicho la husuda' wanasingiziwa mama wakwe jamani?



 
...Paka Mweusi, sasa narudi kwa post yako mkuu. Umesema kwamba ni mara nyingi hizi material things zinachangia 'msukosuko' baina ya mama mkwe na mamsapu, ni jinsi gani wewe Mwanaume utaweza kuepusha/kutatua mgogoro huo apart kwa haya uliyoyaandika hapa chini?



...Mkuu Paka Mweusi, kuwatenganisha una maana gani? Kwa kesi hii, Mke na mume wanaishi ughaibuni, na mama mkwe anaishi Nyumbani Tanzania



...loh, hapo kwenye suala la mama mkwe kusingiziwa kuloga nayo ni kesi nyingine hiyo. Binafsi nishakumbana sana na hizo kesi eti mama mkwe kaloga mke asipate ujauzito, au mtoto akizaliwa anakufa, au kuumwa umwa kwa mtoto, kwanini kila 'jicho la husuda' wanasingiziwa mama wakwe jamani?






Mkuu naona jinsi hali lilvyo ngumu katika kutatua tatizo hilo.Lakini ikumbukwe kuwa ni ukweli tu ndio humuweka mtu huru bila ukweli basi hakuna ufumbuzi utakaopatikana,na ni lazima mwanaume achukue hatua ili kujua chanzo cha ugomvi huo ni nini ,bila kujua chanzo amani haiwezi kupatikana,na katika kutafuta chanzo hicho mwanaume asimamie ukweli unaoonekana na kusiwe na visingizio vya aina yeyote.
Niliposema kuwatenganisha nilidhani kuwa wanaishi pamoja katika nyunba moja kama ilivyo mara nyingi,lakini kama mmoja yuko ughaibuni mwingine yuko nyumbani basi hapo inakuwa rahisi zaidi kwa jamaa ,yeye apige marufuku kwanza communication yeyote baina yao iwe kwa simu,e mail facebook n.k.Na ahakikishe kuwa hawawasiliani ndipo atafute jinsi ya kuwaweka chini pamoja,bila ya kuwaweka pamoja hapo hakuna suluhu maana inaonesha mke amechukizwa sana kiasi cha kufikia hatua hiyo.Na hata ikishindikana kusafiri kurudi nyumbani kuwakutanisha basi teknolojia zipo kikao kinaweza kufanyika hata kwa njia ya simu kila upande ukiwa na loud speaker yote hayo ni katika kutafuta ukweli.Hilo la kushikana uchawi lipo mkuu iwapo mmoja kati ya hao wawili atapata madhara ya aina yeyote au mikosi ya maisha.
 
Kaka Paka Mweusi umesema vema kwa kweli ni hali ya ajabu hii na ni wazi kuna kitu kikubwa kilichojificha ambacho ni ukweli tu pekee ndio utasaidia kutatua tatizo hili. But cha kujiuliza ni kuwa iweje mke awe na guts za kumvua nguo mama mkwe hadharani kama hana mkono wa mume nyuma yake??? Unless mseme mume hajui kabisa kuwa mamake anatucwa hadharani kitu ambacho kinanifanya niamini kuwa huyu mwanamke ana hitilafu kichwani kama si kuwa na wapambe wanaompa kichwa katika hili.

I mean sipati pich akama nyamayao awe na bifu na mamkwe wake kisha aanze tu kumwaga sumu Fasibukuni yaani hainiingii kabisa unles Mr. Nyaamayao awe amempa mkewe go ahead kufanya afanyavyo kitu ambacho sidhani kama inawezekana.

Nway sijui lakini bado naona mke hajatumia busara kabisa
 
MJ1 umenimaliza mbavu zangu...wakati mwingine inabidi kwa kweli, mie cku hizi namwacha aseme tu wewee, mwanae akitoka job kamdaka wapo kibarazani ataongea na mwanae mpaka saa 5 ucku, ukiwa umeingia kulala kosa, kwanini hakusubiri muingie room pa1, hakuna kizuri kwake, ukipika utaambiwa umepika hivi nimevila sana nyumbani ningetamani kula hiki, hapo nilishamuuliza mama unajickia kula nn ananijibu chochote tu, kuna cku kweli nami ilibidi tu,alikuwa anakaribia kuondoka nikasema niende nae eneo moja linaitwa garisa akajichagulie mwenyewe vitu anavyotaka kwenda navyo nyumbani, tena kwa pesa yangu bila cent ya mwanae, tumerudi anachambua vitu vya kwenda navyo vingine akaviacha kwamba havitamfaa, kote huko alichagua mwenyewe bila mie kumpangia, nyumbani kamuona mwanae akanifanyia alichonifanyia, ktk mzigo wote kachagua vitu kama vi3 tu vingine havimfai lakini alivichagua mwenyewe....hapo uzalendo ulinishinda, kesho yake wakati anapanda shuttle na shuttle hiyo hiyo nikaviweka vitu alivyovikataa viende kwa mama yangu, kuanzia cku hiyo akija wala cjiguc kumuuliza hata kama ana mswaki.....

...Nyamayao nikukate kauli, chanzo cha 'mvutano huu' ni nini? Na mume anamsimamo gani kwako juu ya hili?
Unauafiki msimamo wake?

Nafikir tatizo kubwa huwa ni conflict of interest

...bado nasubiri uchanganuzi hapa.

Kaka Paka Mweusi umesema vema kwa kweli ni hali ya ajabu hii na ni wazi kuna kitu kikubwa kilichojificha ambacho ni ukweli tu pekee ndio utasaidia kutatua tatizo hili. But cha kujiuliza ni kuwa iweje mke awe na guts za kumvua nguo mama mkwe hadharani kama hana mkono wa mume nyuma yake??? Unless mseme mume hajui kabisa kuwa mamake anatucwa hadharani kitu ambacho kinanifanya niamini kuwa huyu mwanamke ana hitilafu kichwani kama si kuwa na wapambe wanaompa kichwa katika hili.

I mean sipati pich akama nyamayao awe na bifu na mamkwe wake kisha aanze tu kumwaga sumu Fasibukuni yaani hainiingii kabisa unles Mr. Nyaamayao awe amempa mkewe go ahead kufanya afanyavyo kitu ambacho sidhani kama inawezekana.

Nway sijui lakini bado naona mke hajatumia busara kabisa

...haha! MwanajamiiOne unaunogesha mjadala,
enhee? ...
Unapata hisia kuna waume wanachangia kuwatukanisha mama zao ee?
 
...Nyamayao nikukate kauli, chanzo cha 'mvutano huu' ni nini? Na mume anamsimamo gani kwako juu ya hili?
Unauafiki msimamo wake?



...bado nasubiri uchanganuzi hapa.



...haha! MwanajamiiOne unaunogesha mjadala,
enhee? ...
Unapata hisia kuna waume wanachangia kuwatukanisha mama zao ee?

Mbu kwa jinsi hili lilivyo na unasema mume kakaa kimya si ni kama katoa go ahead kwa mamsap aendelee kumwaga sumu dhidi ya mama mkwe?? (kama anajua lakini kuwa mamake anaanikwa huko nje). Pengine mama alikuwa na visaaaa, wifi kavumiliaaaa kaona hapana, kamweleza mpenzi mumewe sasa hapa hatujui kama mume alipuuza au vipi maana mwingine awezajibu ah bwana mtajuana wenyewe huko......au hebu mpuuze tu achana naye... au anaamua kumtetea mamake tena kwa kuside naye kabisa sasa wifi ndo chuki inazidi kupanda na mama mkwe akiona anapata support ya mwanae wa kiume (na mawifi kama wapo) basi ndo machejo yanazidi so wifi anaamua tu kuuvua utu.

Lakini kama mume anakuwa makini pale anapohisi au kupelekewa malalamiko asipuuze ajaribu kuangalia namna atakavyosuluhisha yeye kama mume wangu, mtoto wa mama mkwe wangu na vile vile kama Prezidaa ya himaya yetu. Asiniambie tu ah mtajuana wenyewe au aside na mamake kunisema au kulalamika hapatakuwa panatosha........ wanaume wengine ni wa ajabu sana ..mie nina ndugu yangu wa karibu kabisa, alikuwa ameolewa na bahati mbaya mumewe hakuwa na maelewano mazuri na babake mlezi ambaye alimlea tangu akiwa mdogo (walikorofishana kwa kuwa baba hakutaka huyu shem amuoe dadangu kwa kuwa alishamtafutia mwingine huko kwao) Bahati mbaya uhasama ulikuwa mkubwa sana..........baada ya muda shemeji akaona hawezigombana na ndugu zake kisa mwanamke....so akaenda kwa huyo babake na kuanza kumwambia maneno ya ajabu kuhusu mkewe na kudai anawagombanisha yeye na babake so wakaungana na kuwa kitu kimoja..... saa ngapi mawifi,shemeji mpaka baba mlezi mwenyewe wasianzishe jeshi??? Wakalipanda basi binadamu wale vruuu hadi Dar nyumbani kwa ndugu yao (hapo shemeji anajitia hana alijualo- tena ndo kwanza walipomwambia wamekaribia ubungo yeye akawasha gari na kutoweka). Dada anashtukia wageni, hana hili wala lile akaanza kushambuliwa kwa maneno na kuitwa mchawi, malya na kila aina ya vurugu. Kabaki anashangaa. Anampigia simu mumewe anajibiwa mie bwana sijui mtajuana wenyewe umewafanya nini hadi wakufungie safari?>....... Ah mbona mashetani yalimpanda, upole akauvua kwanza naye akafungulia bomba la matusi kwanza kabla ya kuwasweka ndani kwa kuja kumfanyia vurugu nyumbani mwake.............na ndoa ikafa.

So ninaposema mume kutia mkono ni kama hivyo Mbu
 
Mnanikumbusha ile hadithi ya mchina alikuwa haelewani na mama mkwe wake, akaenda kwa mganga akiomba dawa ya kumwua. Mganga akamwambia nitakupa dawa inayoua taratibu kwa sababu kama akifa ghafla utashtukiwa. Mganga akampa majani yaliyosagwa vizuri akamwambia nenda mpikie chakula kizuuuuuri umwekee na hii daya kidogo. So kila siku ufanye hivyo na wewe umwonyeshe upendo yaani uwe naye karibu na umpe kila akitakaco. Akikutukana wewe cheka ni sehemu ya dawa so hata akijakufa watu hawatakushtukia wewe sana sana watakuonea huruma.

Bi dada akaanza kazi ya "kuua" akawa anajipikilisha vinono, anamcare yaani kuliko hata anavyomcare mumewe au mamake mzazi. Baada ya mwezi wakawa marafiki wa kufa yaani wakawa wanapiga story kupita maelezo. Ikabidi bi dada arudi kwa mganga amwambie anaomba dawa ya kupunguza makali ya sumu alokuwa anampa mama mkwe kwa kuwa kwa sasa hataki tena kumpoteza amekuwa rafiki yake mkubwa. Mganga akamwambia wala ile haikuwa sumu ni vitamins tu na kilichobadilisha tabia yake ni atitude yako na upendo na kujali unakompatia so endelea tu kuishi kwa furaha na rafiki yako.

So sometimes na sie wanawake tunapaswa kuangalia attitudes zetu towards wamama hawa. Ingawa nakiri wapo wale ambao hawapendeki yaani hata ufanye nini umlambe miguu kila asubuhi kama ishara ya kumshukuru kwa kukuzalia chema wapi.......atakubetulia mdomo. Mie huwa naangalia sana movie za kinigeria hasa zile za Patience Ozokwor "Mama Gee". akiamua kucheza kama mama mkwe mwenye roho mbaya huwa ananimaliza kabisa. But najifunza mengi
 
Back
Top Bottom