Anti-Social wenzangu tujuane tabia zetu

Anti-Social wenzangu tujuane tabia zetu

mpasta

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2011
Posts
919
Reaction score
2,007
Niende moja kwa moja kwenye mada, nina vitabia ambavyo ni ngumu kunibadilisha na kujibadilisha,
(1) Sipendi kuangalia TV, utaniona kwenye TV hasa kukiwa na mpira wa miguu vinginevyo mie ni mtu wa redio kwa sana, tena hasa TBC TAIFA na vipindi vyangu vile taarifa za habari, hotuba za baba wa taifa, muziki wa zilipendwa ukichambuliwa na MASOUD MASOUD mie kwangu burudani kabisa.

(2) Mwanamke/Msichana akijipodoa sana kwangu anaboa. Akijitoboa pua yake hata kutazama sura naogopa kabisa, akijifunga vikuu miguuni ananiboa, n.k.Napenda sana Mwanamke awe Natural, yaani aoge zake apake mafuta yake ya nazi na kumchana nywele zake au asile twende kilioni[emoji1787][emoji1787]

(3) Sherehe Sherehe hizi sijui za Ndoa, Birthday DAAAH hizo ndio sizipendagi kabisa, kama ndoa nitaishia kutoa mchango tu lakini ukumbini hunioni. Kichwani naona kama kupotezeana muda tu, watu wanaonyeshana uzuri wao, mavazi yao, na ratiba nyingi zisizo na kichwa wala miguu.

(4)Nipo DSM kwa zaidi ya miaka 20 tokea nipo Form 1 sijatoka tena lakini kwenda Beach kujipumzisha hata mara 10 hazifiki. Hayo maonyesho ya Sabasaba hata viwanja vyenyewe sijawahi kukanyaga, n.k.

Kwa ufupi kama sina Issue ya kunitoa Home, nitakaa tu na watoto wangu wanafanya home work zao za shule mie nipo pembeni yao nasoma vitabu vyangu vya riwaya tu vya akina Willy Gamba, Ben Mtobwa,Hammie Rajab, John Simbamwene, n.k nikichoka Riwaya nitarukia vitabu vya akina Kiyosaki,Robin Sharma.

NAENJOY maisha yangu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mimi sipendi mijumuiko ya watu huwa napenda kukaa peke yangu rafiki yangu mkubwa ni simu napenda game na kuingia kwenye social network tena kusoma vitu vya msingi.

Sipendi vichekesho, hapa kwenye Radio tumefanana kipindi nipo shule ilikuwa asubuhi nawasha nasikiliza BBC swahili mpaka wanafunzi wenzangu wakawa wananishangaa.

Wanawake sipendelei mpaka nilivyokuja kuoa na mkewangu ananiona naboa maana huwa simuongeleshi sana au kumchekesha na akiniambia kitu cha kuchekesha wala huwa sicheki
 
Mim sipend kujumuika na watu nisio wafaham , sipend kuongelewa, Sipend wanawake hasa wenye Usasa mim kwangu mwanamke hajawah kunisumbua kichwa changu kabisa, sipend kuingiliw kweny maamuz yangu, Sipend marafik wanafik wanaopenda Story na kupotezeana mda kwnye vijiwe, Inshort mim Sio muongeaji kabisa.

Napenda kusoma vitabu, Huwa napend kukaa Peke angu mda mwing naamin kukaa peke angu najiepusha na matatizo mengi sana......[emoji851][emoji851][emoji851] eeh thats is Me......
 
mimi sipendi mijumuiko ya watu huwa napenda kukaa peke yangu rafiki yangu mkubwa ni simu napenda game na kuingia kwenye social network tena kusoma vitu vya msing...
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]anaishi na Roboti
 
Mimi huwa sipendi kujumuika na watu.Muda mwingi huwa napendelea kusikiliza mziki,redio,kuperuzi JF au kucheza games pale niwapo huru na kazi.

Katika siku,naweza cheza games kwa hata saa nne,kusikiliza redio saa nne na kusikiliza mziki saa moja.

Huwa sipendi kujipendekeza.Salama kwa watu wazima huwa ni kila siku alafu nafanya mambo yangu.Ila salamu kwa vijana wenzangu utakuta leo namsalimia,kesho akipita akanipiga buyu asinisalimie yeye imeisha hiyo,nitakuwa nampita tu nafanya mambo yangu.Ila kama akipita akanisalimia huwa tunasalimiana 50/50 hakuna kujipendekeza kudadeki.Salamu ninayotoa 100/0 ni kwa walionizidi umri tu.

Wanawake ndiyo kabisa nilishagundua ukiwa unawasalimia salimia hovyo wanakuona kibaraka Chao.Huwa ninafanya mambo yangu alafu huwa sipendi kuongelewa au kuangaliwa.Jana nilienda dukani kuna manzi nayo ikaja haijatoa salamu wala nini ikawa inaniangalia,nikampigia mbuzi kudadeki akageuza kichwa mimi huyo nikaondoka zangu baada ya kupata huduma.

Halafu wanaume wamepungua kweli. Siku hizi unapita zako unaanza kushangaa wanaume wenzako wanakuangalia na hii ni obviously lazima wakuongelee.

Nipo kanda ya ziwa kikazi watu wa huku nilivyopata experience wana ukabila na wanajiona bora sana. Sasa mimi sitaki shobo na mtu ni mwendo wa mbuzi na mambo yangu na sitaki ushenzi ukileta mazoea nakuzingua,Ili wajue kuna wanaume nje ya kanda ya ziwa.

e147cc088e344dd9b9c3514208220bca.jpg
 
Mie napenda sana kuangalia movie, kuchati online na watu nisiowajua, kusikiliza miziki, kutomb na kusoma vitabu vyenye story za kusisimua. Sitaki kuamini mimi ni ant social ila kitendo cha kuwa busy na ma movie na vitu vingine vikanipelekea kuwa anti social. Nikiwa mbele za watu nikawa nakosa vya kuchangia, inakuletea uoga kuwa nikisema jambo nitakuwa nakosea. .

Nikaja kugundua life style yangu inanipeleka pabaya nikaanza kujenga mzoea na watu mpaka imekuwa kero. Nikitembea kilometers moja nishasalimiana na kila mtu na wamenipachika jina MWENYEKITI. Watu wa mtaani wanataka sana niwe mwenyekiti wao wa serikali za mtaa. .

Kuwa anti social sio maana ya kuwa usisalimiane na watu, kikubwa ni kusimamia au ku balance watu wa msingi wawepo kwenye circle yako. Kuna mda unasikia mtu kajiua kuwa mwenyewe na kujiaminisha huhitaji wengine ni jambo la kuangalia kwa jicho la tatu. .
 
Mwaka 2005 ilikuwa mwisho wangu kujihusisha na dini/ibada na ni baada ya padri kukataa kumzika classmate.

Sijawahi na sitowahi kuwakubali ccm au yanga/utopolo.

Sipendi kuongea sana hivyo ukinikuta na mtu ujue ni mtulivu kama mimi.

Nashabikia simba na ni mwanachama mkubwa tu ila sijawahi kuvaa jezi ya simba toka utotoni.

Sijawahi kuvaa nguo yenye maandishi au picha au mchoro wowote.

Mimi ni ngumi mkononi na nikipiga ni moja tu.

Sijawahi hudhuria sherehe yoyote, nikienda msibani sijawahi kutazama maiti.

Barabarani ukinizingua nakufata hadi ukipark nakueleza. Ukibishana nakupasua.
 
Niende moja kwa moja kwenye mada, nina vitabia ambavyo ni ngumu kunibadilisha na kujibadilisha,
(1) Sipendi kuangalia TV, utaniona kwenye TV hasa kukiwa na mpira wa miguu vinginevyo mie ni mtu wa redio kwa sana, tena hasa TBC TAIFA na vipindi vyangu vile taarifa za habari, hotuba za baba wa taifa, muziki wa zilipendwa ukichambuliwa na MASOUD MASOUD mie kwangu burudani kabisa.

(2) Mwanamke/Msichana akijipodoa sana kwangu anaboa. Akijitoboa pua yake hata kutazama sura naogopa kabisa, akijifunga vikuu miguuni ananiboa, n.k.Napenda sana Mwanamke awe Natural, yaani aoge zake apake mafuta yake ya nazi na kumchana nywele zake au asile twende kilioni[emoji1787][emoji1787]

(3) Sherehe Sherehe hizi sijui za Ndoa, Birthday DAAAH hizo ndio sizipendagi kabisa, kama ndoa nitaishia kutoa mchango tu lakini ukumbini hunioni. Kichwani naona kama kupotezeana muda tu, watu wanaonyeshana uzuri wao, mavazi yao, na ratiba nyingi zisizo na kichwa wala miguu...

(4)Nipo DSM kwa zaidi ya miaka 20 tokea nipo Form 1 sijatoka tena lakini kwenda Beach kujipumzisha hata mara 10 hazifiki. Hayo maonyesho ya Sabasaba hata viwanja vyenyewe sijawahi kukanyaga, n.k
Kwa ufupi kama sina Issue ya kunitoa Home, nitakaa tu na watoto wangu wanafanya home work zao za shule mie nipo pembeni yao nasoma vitabu vyangu vya riwaya tu vya akina Willy Gamba, Ben Mtobwa,Hammie Rajab, John Simbamwene, n.k nikichoka Riwaya nitarukia vitabu vya akina Kiyosaki,Robin Sharma.
NAENJOY maisha yangu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ulivyoitaja tu TBC kama ndio redio pendwa kwako wenye akili tayari wanakujua ni mtu wa aina gani, hukuwa na haja ya kuandika gazeti.
 
Mimi huwa sipendi kuogea sokoni na wala sijawahi tombea uchochoroni kama akina nanihino
 
Tunafanana yote mkuu, kama mapacha vile. Ila tu tofauti kwenye novel, mimi nasoma na naandika miswada yangu, nina riwaya na plays zaidi ya 40, sijaanza kuchapisha.

Pia huwa naweza kaa mwezi na zaidi sijawatembelea hata majirani nipo zangu ndani na shughuli zangu tu.
 
Niende moja kwa moja kwenye mada, nina vitabia ambavyo ni ngumu kunibadilisha na kujibadilisha,
(1) Sipendi kuangalia TV, utaniona kwenye TV hasa kukiwa na mpira wa miguu vinginevyo mie ni mtu wa redio kwa sana, tena hasa TBC TAIFA na vipindi vyangu vile taarifa za habari, hotuba za baba wa taifa, muziki wa zilipendwa ukichambuliwa na MASOUD MASOUD mie kwangu burudani kabisa.

(2) Mwanamke/Msichana akijipodoa sana kwangu anaboa. Akijitoboa pua yake hata kutazama sura naogopa kabisa, akijifunga vikuu miguuni ananiboa, n.k.Napenda sana Mwanamke awe Natural, yaani aoge zake apake mafuta yake ya nazi na kumchana nywele zake au asile twende kilioni[emoji1787][emoji1787]

(3) Sherehe Sherehe hizi sijui za Ndoa, Birthday DAAAH hizo ndio sizipendagi kabisa, kama ndoa nitaishia kutoa mchango tu lakini ukumbini hunioni. Kichwani naona kama kupotezeana muda tu, watu wanaonyeshana uzuri wao, mavazi yao, na ratiba nyingi zisizo na kichwa wala miguu...

(4)Nipo DSM kwa zaidi ya miaka 20 tokea nipo Form 1 sijatoka tena lakini kwenda Beach kujipumzisha hata mara 10 hazifiki. Hayo maonyesho ya Sabasaba hata viwanja vyenyewe sijawahi kukanyaga, n.k
Kwa ufupi kama sina Issue ya kunitoa Home, nitakaa tu na watoto wangu wanafanya home work zao za shule mie nipo pembeni yao nasoma vitabu vyangu vya riwaya tu vya akina Willy Gamba, Ben Mtobwa,Hammie Rajab, John Simbamwene, n.k nikichoka Riwaya nitarukia vitabu vya akina Kiyosaki,Robin Sharma.
NAENJOY maisha yangu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Umeshazeeka mkuu kama unasikiliza TBC taifa
 
Tunafanana yote mkuu, kama mapacha vile. Ila tu tofauti kwenye novel, mimi nasoma na naandika miswada yangu, nina riwaya na plays zaidi ya 40, sijaanza kuchapisha.

pia huwa naweza kaa mwezi na zaidi sijawatembelea hata majirani nipo zangu ndani na shughuli zangu tu.
Habari mkuu.

Naweza kuku-pm kupata angalau vionjo vya riwaya zako?
 
Mimi kwanza sipendi kukaa kijiweni nikirudi kazini ndani na angalia movie ,music na kuchezea simu na mke wangu akiwa karibu yangu kwa sababu yakutopenda kukaa kijiweni najiona Nina IQ kubwa kushinda wao kwanini hakuna dili zidi ya kupigana vizinga mtu anakuomba 200 ya sigara ukiniona kijiweni ni kazini muda wa kula . Kwa ufupi napenda kuwa busy sipendi story na pia sipendi majungu kumdisi mtu fulani
 
Mimi kwanza sipendi kukaa kijiweni nikirudi kazini ndani na angalia movie ,music na kuchezea simu na mke wangu akiwa karibu yangu kwa sababu yakutopenda kukaa kijiweni najiona Nina IQ kubwa kushinda wao kwanini hakuna dili zidi ya kupigana vizinga mtu anakuomba 200 ya sigara ukiniona kijiweni ni kazini muda wa kula . Kwa ufupi napenda kuwa busy sipendi story na pia sipendi majungu kumdisi mtu fulani
Ndiyo ni kweli hapo kwenye majungu.Hivi vijiwe vimewabadilisha wanaume wengi kabisa.Yale tuliyoyazoea kwa wanawake mambo ya umbeya yameamia kwa wanaume.

Si ajabu wengine wakawa wanaongelea mafanikio yako huku wakijawa wivu na vinyongo tu.Huo muda wa vijiweni wangekuwa wanaingiza pesa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom