Anthony Diallo abanwa kona zote nne

Anthony Diallo abanwa kona zote nne

Sisi wa Pwani tunasema KILICHOMKUTA MAMBA NA KIBOKO KITAMKUTA

Post sent using JamiiForums mobile app
Sisi wa MSANGA CHOLE na MANEROMANGO tunaitaga BOKO

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Waulize kilicho mfika Capt John Komba

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Dialo kaajiri watanzania wangapi?

Anyway,hili ni funzo kwa wamiliki wengine wa vyombo vya habari na matajiri wa nchi hii kwa ujumla.

Mawaziri wa leo mna la kujifunza pia pamoja na wabunge mnaotunga sheria za nchi hii.
Billions of money anazodaiwa huzioni, unaona ajira tu[emoji15] [emoji15] [emoji15]

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Namuona samadu hassan yuleeeee azam

Post sent using JamiiForums mobile app
 
IMG-20170716-WA0001.jpg


Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Wakati akimpigia msukuma kampeni 2015,Mlikuwa mkimsifia sana Diallo na kusema ni kada mtiifu kwa chama.Ila leo na akili zenu za kishikiwa,Mnamgeuka na kusema anakwepa kodi,Ulishawahi kujiuliza kipindi cha kampeni pia alikuwa anadaiwa kadi pia na ndio lengo la kumsupport Ngosha ili ampe ahueni akipata urais?...
Au mlikuwa mnapiga makofi tu kama majuha.

In this world,It doesn't matter who you are,But what you do to Survive.


Mtu anaposafiri sio lazima atumie gari lake.
Unaweza ukapanda gari la mtu na ukafika unapokwenda.
Dialo kazi yake iliishia wakati wa kampeni kama mwenyekiti wa Chama wa mkoa wa Mwanza. Alipiga kampeni kama mwenyekiti wa mkoa na ndiyo kazi yake aliyoomba kwa faida yake na chama chake . Suala la kumfanya aendelee kukwepa kodi halipo kwenye ilani ya chama chake.

Nasema tu bado kazi ndio imeanza , kama TRA wanauchoma mti mbichi itakuaje kwa mti mkavu?? Tafakari !!
Hakuna mtu aliyeiiibia hiii nchi atakayesalimika.
Roho ya Nyerere na ya Sokoine zimeungana zikaja kwa roho moja ya JPM.
Waliokwapua kwa makusudi rasilimali za umma wajiandae kuzirejesha fasta kama Ngeleja. Hakuna kuremba. Hakuna mambo ya sijui kada wa CCM , MCC sijui CUF , FUC wala Chadema au Madecha wapeleke huko vyama vyao sisi tunataka nchi yetu yenye haki sawa kati ya matajiri na maskini. Kila mtu apate mali zake kihalali na kwa kiwango cha uhalali wake na sio kuiba mali za umma kwa mwendokasi.


Post sent using JamiiForums mobile app
 
Wahaya tuna msemo: "OLWO SHULA MKASHO LWIJA NANYOKO" kwa kiswahili lina maana ya "UKIMUOMBA MUNGU AFE MAMA YAKO WA KAMBO BADALA YAKE ANAKUFA MAMA YAKO MZAZI" kwa kifupi unashauriwa hata siku moja usiwatakie/ombea wanadamu wenzako mambo mabaya mfano magojwa au kifo.
Haya hongera nimejua kuwa wewe mhaya

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Fedha za ufisadi zina jeuri ya ajabu hata sijui ndege zile ziliishia wapi.
Zingelikuwepo mpaka leo kila mhaya angelikuwa ameishapanda ndege kwa wanavyopenda sifa.

Post sent using JamiiForums mobile app
Ahahahahaaa acha ukuda mshikaji loooh unataka kubadili mada. Wasukuma ndo hawapendi sifa?!!!
 
Mh.Rais wetu Magufuli hana urafiki na mkwepa kodi hata kama ni mkewe au mwanawe wa kumzaa.Asipolipa kodi funga biashara.
Amewambia TRA maneno mawili tu FUNGA.

Hata kwenye vituo vya mafuta ni maneno mawili tu "FUNGA".

Iwe ni kada wa CCM au nani asipolipa kodi FUNGA biashara .
Maneno ni mawili tu FUNGA.



Post sent using JamiiForums mobile app
FUNGA ni neno moja ila lenye silabi mbili yaaa FU na NGA na lina herufi tano.....F-U-N-G-A.
 
Mh.Rais wetu Magufuli hana urafiki na mkwepa kodi hata kama ni mkewe au mwanawe wa kumzaa.Asipolipa kodi funga biashara.
Amewambia TRA maneno mawili tu FUNGA.

Hata kwenye vituo vya mafuta ni maneno mawili tu "FUNGA".

Iwe ni kada wa CCM au nani asipolipa kodi FUNGA biashara .
Maneno ni mawili tu FUNGA.



Post sent using JamiiForums mobile app
FUNGA ni neno moja ila lenye silabi mbili yaaa FU na NGA na lina herufi tano.....F-U-N-G-A.
 
Jamaa alikipambania sana chama chake kwenye kampeni za mwaka juzi, akiangukie chama kimsaidie kwa kweli, mapigo yote hayo at once hawezi kuchomoka.
 
Mnacho sahau kila mfanya biashara ana madeni hilo ni jambo la kawaida kabisa - Serikali yenyewe ina madeni sembuse Dk.Diallo? Kama kuna wanao mdai au masuala ya kodi sina shaka watafikia muhafaka wa jinsi ya kulipana - watapeana timeframe ya kupunguza deni na siyo kufunga makampuni/ biashara zake, Dk.Diallo alianza kufanya biashara/Makampuni/Viwanda tangu enzi za Baba wa Taifa, si mtu wa kuchukuliwa kimzaa mzaa, kama kuna tatizo walimalize kistaarabu.

Hapa naona baadhi ya members wa vyama vya upinzani wamevalia njunga suala hili wakati hawajui kinacho endelea - wanaweka mbele chuki binafsi tu, kisa? Eti kwa nini hakushirikiana na MOAT kumkandia RC wa Mkoa wa Dar - mambo ya kitoto kabisa!!

Kwanza MOAT wana mamlaka gani katika Taifa letu zaidi ya kutumika kisiasa - nani hakushuhudia maigizo yao yaliyo kuwa na lengo la kujaribu kumshinikiza JPJM amfukuze kazi Makonda wa watu, ukijaribu kutafakari hoja walizo kuwa wanatoa zote zilikuwa zinaonekana wazi wazi zimechongwa tu, wakati mwingine sisi Watanzania tunakuwa na tabia za ajabu sana.

Ume andika sana afu hamna point
 
Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza Anthony Diallo yuko kwenye nafasi mbaya kisiasa, kimaisha, kibiashara na hata kimahusiano na jamii.

Baada ya kituo chake cha matangazo cha Star Television kutiwa kufuri za nyororo na TRA kwa kuidai kampuni yake zaidi ya shilingi 4.5bn, Diallo amefikwa na balaa jingine la pili baada ya benki moja ya jijini Mwanza kumshtaki kwa kushindwa kuilipa zaidi shilingi 600m alizoiomba benki hiyo iwe inawalipa mishahara wafanyakazi wa kampuni zake.

Pigo jingine la tatu ni hatua ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kuanza kutroti kuiwania nafasi yake ya uwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza, nafasi ambayo kwa njia moja ilikuwa ikimkinga kidogo na bughudha ndogo ndogo za vyombo vya dola na taasisi za fedha.

Pigo jingine linalomuathiri bwana mkubwa huyu aliyewahi kuwa waziri wa wizara mbali mbali katika awamu mbili zilizopita na ambaye Rais Kikwete aliwahi kumwombea kwa Magufuli wakati wa kampeni za urais ampe upendeleo wa kibiashara katika shughuli zake, ni kitendo cha kutengwa na waliokuwa washirika wake wa vyombo vya habari MOAT kumtenga baada ya kuonekana kukiuka taratibu zao walizojiwekea.

Kwa kifupi hivi sasa Diallo kashika njia inayoelekea katika lango kubwa lililoandikwa OFISI YA MUFLISI.
Hulka ya binadamu ni kushangilia anguko la waliofanikiwa... Diallo alifanikiwa kimaisha kiasi chake lakini mafanikio yake akayatumia vibaya.... Huyu mwacheni tu watu wafurahie anguko lake

Post sent using JamiiForums mobile app
 
A
Hulka ya binadamu ni kushangilia anguko la waliofanikiwa... Diallo alifanikiwa kimaisha kiasi chake lakini mafanikio yake akayatumia vibaya.... Huyu mwacheni tu watu wafurahie anguko lake

Post sent using JamiiForums mobile app
Alifanikiwa kwa kukwepa kodi kama hivo, upo hapo
 
Back
Top Bottom