Acha utani, kaofisi tu ka Chademakwanza kako vile! Mbowe naye kutwa kufuatiliwa kutokulipa kodi, madawa, biashara kwenye vyanzo vya maji kama sio kujilipisha maposho ya nguvu!Nashauri Mbowe au CDM ijipange iinunue Sahara Media
Atajinyonga?Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza Anthony Diallo yuko kwenye nafasi mbaya kisiasa, kimaisha, kibiashara na hata kimahusiano na jamii.
Baada ya kituo chake cha matangazo cha Star Television kutiwa kufuri za nyororo na TRA kwa kuidai kampuni yake zaidi ya shilingi 4.5bn, Diallo amefikwa na balaa jingine la pili baada ya benki moja ya jijini Mwanza kumshtaki kwa kushindwa kuilipa zaidi shilingi 600m alizoiomba benki hiyo iwe inawalipa mishahara wafanyakazi wa kampuni zake.
Pigo jingine la tatu ni hatua ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kuanza kutroti kuiwania nafasi yake ya uwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza, nafasi ambayo kwa njia moja ilikuwa ikimkinga kidogo na bughudha ndogo ndogo za vyombo vya dola na taasisi za fedha.
Pigo jingine linalomuathiri bwana mkubwa huyu aliyewahi kuwa waziri wa wizara mbali mbali katika awamu mbili zilizopita na ambaye Rais Kikwete aliwahi kumwombea kwa Magufuli wakati wa kampeni za urais ampe upendeleo wa kibiashara katika shughuli zake, ni kitendo cha kutengwa na waliokuwa washirika wake wa vyombo vya habari MOAT kumtenga baada ya kuonekana kukiuka taratibu zao walizojiwekea.
Kwa kifupi hivi sasa Diallo kashika njia inayoelekea katika lango kubwa lililoandikwa OFISI YA MUFLISI.
Bil 4.5 mkuu?Kama atatokea mtu kuinunua anaweza akayanunua na madeni halafu kituo akapewa karibu na bure, ikitokea wafanyakazi watabakia na kazi zao,
Aiseee[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Naona edo anapiga push up kununua sahara media....ngoja siku 14 ziishe
Post sent using JamiiForums mobile app
Haha! Mhenga kutoka chattleACHA WAISOME NAMBA EHEEEEEE
.......WAJINGA WALE
Post sent using JamiiForums mobile app
Ama hakika umetimia ule msemo WA mhenga mmoja kutoka chattle kuwa "matajiri wataishi kama mashetani" ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni
Diallo vuna ulichopanda 2015
Ndio mkuu maneno ya mhenga yanatimia sasaHaha! Mhenga kutoka chattle
Post sent using JamiiForums mobile app
Naona yaliyopelekea kifo cha kapt komba yakijirudia tenaDiallo alikuwaga team Lowassa kabla hajahamia team Membe,lazima akiwa Team Lowasa alifanyaga figisu kubwa mpaka naona hata favor hafanyiwi tena.JK njoo umuokoe Diallo atakufa kwa pressure.
Zambi ya usaliti ni mbaya sana, aliwasaliti wenzie kuhusiana na ishu ya bashite... Leo yamemrudia, safi sanaaaLazima akili zitamrudia tu huyu diallo
Ni mhaya huyo, SI unawajua tambo zao Mkuu
Hao jamaa hawakuwahi kuwa marafiki ila waliunganishwa na mtandao kwa maslahi binafsi,kumbuka kulikuwa na maadui wakubwa ndani ya mtandao km Sitta vs Prof Kapuya!Je before that ? Kumbuka JK na Lowassa walishawahi kuwa friends, Diallo na Lowassa pia walishawahi kuwa friends
Teh teh teh teh teh!!! Yaani wewe msukuma una vituko halafu nimekukumbuka kinomaDiallo alikuwaga team Lowassa kabla hajahamia team Membe,lazima akiwa Team Lowasa alifanyaga figisu kubwa mpaka naona hata favor hafanyiwi tena.JK njoo umuokoe Diallo atakufa kwa pressure.