Anna Abdalah: Makanisa yamekuwa mengi

Anna Abdalah: Makanisa yamekuwa mengi

Status
Not open for further replies.
Acha kamba wewe mfuasi wa Moh, Uislam umeanza miaka 500 baada ya Kristu. Habari za Urongo pereka kwenye mihadhara
ndio maana pia wafuasi wa mussa nae hawakumtaka yesu coz nae alikuja zaidi ya miaka miatano baadae pamoja na kwamba yesu alikua myahudi mwenzao lakini hawakutaka kumuamini mpaka kesho...
 
Usichanganye mambo mawili tofauti.

Mimi mwenyewe sifagilii makanisa kwa saaana.

Lakini nafagilia uhuru wa kuabudu (na kutoabudu) kwa saana kuliko nisivyofagilia makanisa kuibuka kama uyoga.

Kwa maana hiyo, ingawa naona makanisa hayana deal kwa sana kwangu binafsi, lakini naelewa kwamba yana maana kwa sana kwa wengine.

Na naheshimu hao wengine hata kama natofautiana nao. Mimi atheist siamini kama kuna mungu, lakini napenda uhuru wa kuabudu, kila mtu aabudu anavyotaka bila kubugudhiwa, wala kupangiwa idadi ya makanisa.

Hii ni haki ya kikatiba, na kusema makanisa ni mengi ni kuingilia haki ya kikatiba ya wananchi, kwa maana wakitaka hata kujenga kanisa kila mtaa wa pili, kama wanataka wao wenyewe, kikatiba sioni cha kuwazuia kimsingi.

Usichanganye kutetea kwangu haki za kukusanyika na kuabudu kama ni endorsement ya kwamba makanisa yana sehemu muhimu sana kwangu.

Natetea haki ya watu kuwa na makanisa yasiyo idadi bila ya kuwa muumini kama ninavyotetea haki ya watu wazima kuvuta sigara bila kuwa mvutaji (na ingawa kwa kweli nachukia uvutaji wa sigara).

Hapa cha msingi ni haki ya kikatiba kutovunjwa. Kwamba haki hiyo inaleta kitu chenye tija au sivyo, jibu langu na la mtu mwingine hayawezi kuwa sawa. Kwa hiyo sitaki kumjibia.

Nikitaka kumjibia ntakuwa dikteta kama serikali hii inayotaka kupanga namba ya makanisa.

Sitaki udikteta, nataka uhuru wa kuabudu (na kutoabudu pia)
Uhuru usio na mipaka ni sawa na fujo na ghasia nyingi, thru churches rotten deals kibao zimekuwa zikifanyika zikiwemo za madawa ya kulevya. kuna ukweli mkubwa sana kwenye kitabu na movie ya Davince Code... Anyway nashindwa kuielewa nukushi yako "Banda limesha vunjika, Jogoo kashaondoka, Vifaranga mkazane kumtoa nyoka"! Huoni kuwa vifaranga vingi sana vitafariki?...Opium?
 
Mhnnn...Huyu mama is now at the extream point. Michango yake yote zaidi ya hivi majuzi kuhusu maandamano na vijembe vyake dhidi ya upinzani na hili la makanisa limemifanya kuwa na maswali mengi juu yake.

Ni mama mzeee (sijui kama analikubali hilo) na ningemushauri haache siasa. Mawazo yake nanyakati tulizomo itamuwia vigumu kuendelea na siasa zamazoea ya ccm.
 
Ustaadhi jibu swali....weka evidence Uislam ni kabla ya Quran period! Great thinker will get only Wheat from the Chaff

Islam began with the first man, Adam, when he submitted himself to God. Therefore, the word “Islam” simply means Submission to God. The word also means Peace; and so, as the name of the Religion of God, it implies the peace that we can attain by submitting to God.


Inaonekana labda ni kweli unapenda kufahamu kitu kuhusu uislam!! Haya twende pamoja humu How Islam Began
 
Acha kamba wewe mfuasi wa Moh, Uislam umeanza miaka 500 baada ya Kristu. Habari za Urongo pereka kwenye mihadhara
Ni hatari kuw na makanisa mengi,ni kama ilivyotokea kwa Joseph Kibwetere,alianzisha kanisa lake na wenzake la Amri kumi za mungu,wakawachoma moto waumini wao,wapatao elfu moja,na wengine kuwauwa kwa mapanga na kuwanyonga na kuwapa sumu.
 
Uhuru usio na mipaka ni sawa na fujo na ghasia nyingi, thru churches rotten deals kibao zimekuwa zikifanyika zikiwemo za madawa ya kulevya. kuna ukweli mkubwa sana kwenye kitabu na movie ya Davince Code... Anyway nashindwa kuielewa nukushi yako "Banda limesha vunjika, Jogoo kashaondoka, Vifaranga mkazane kumtoa nyoka"! Huoni kuwa vifaranga vingi sana vitafariki?...Opium?

Uhuru una mipaka. Mipaka ya uhuru ni sheria. Ndiyo maana nikarejea kwenye sheria mama, katiba.

Serikali yetu imekataa hata kuweka kifungu cha kumuhesabu mtu kwa dini Tanzania, kwa kutambua "separation of church and state".

Sasa huyu mama anavyotaka kuja kutuambia leo makanisa mengi sana wakati hata hana jinsi ya kujua idadi ya Wakristo Tanzania kiserikali, kwa sababu serikali ilikataa kuwahesabu watu kwa dini, anajuaje kama makanisa ni mengi sana? Anaielezeaje ile principle ya "separation of church and state" iliyoifanya serikali ikatae kuhesabu watu kwa dini?

Serikali gani hii kigeugeu? Jana imekataa kuhesabu wakristo, kwa sababu haitaki kujiingiza kwenye dini, leo imehesabu makanisa na kuyaona mengi sana, hata bila ya kujua wakristo wako wangapi.

Inaingia akilini kweli hii?

Kama una matatizo na rotten deals, target rotten deals, usi target idadi ya makanisa ukafanya mtego wa panya unasao waliokusudiwa na wasiokusudiwa.

Unaweza kusema makanisa mwisho 500 nchi nzima, na bado hayo 500 yakawa na rotten deals vile vile kama huangalii rotten deals specifically. What has rotten deals to do with the number of churches?

Kama nina matatizo yoyote na waumini, kitu kimoja sina tatizo nao. Pale inapokuja haki yao ya kikatiba ya kuabudu naiheshimu, na naitetea.

Nakataa totalitarianism. Tukikubali serikali ituwekee namba ya makanisa leo, kesho serikali hiyo hiyo itarudi na kusema "magazeti mengi sana sasa, inabidi tuyapunguze"

Unaweka precedent ya kuipa serikali nguvu ya kuvunja katiba. Kuondoa uhuru wa kuabudu, kuondoa uhuru wa habari etc.

Tushaanza kusikia habari kwamba wanataka kutunga sheria kali dhidi ya maandamano, ambayo nayo ni haki ya kikatiba.

Ingawa sifagilii makanisa, sifagilii wananchi kunyimwa haki yao ya kikatiba ya uhuru wa kuabudu zaidi.

Where EMT at ?
 
Kwa kiasi fulani nakubaliana na huyu mama.
Nyumba za kuabudia zimekuwa zikijengwa ovyo bila mpangilo maalum, alafu unakuta wanapiga miziki sijui nini siku nzima. Yaani zimekuwa kero kwa kweli.
Mi nafikiri sheria ya ku regulate nyumba za ibada zitungwe. Yes tunataka Uhuru wa kuabudu, lakini basi tusibughuziane.

yaani mara nyingine unakuta kanisa ndani lina watu 2, lakini wamefungulia maspika mpaka mtaa wa tatu huko, ina bore sana

adhana ni kero pia, vipi misikiti ipo mingapi?
 
Hapa Mama kachemka..hata hivyo umri umeenda sana mpaka reasoning yake imeshaanza ku~Serukamba.. imefika wakati sasa afikirie kuachia ngazi ili nafasi yake iwe na mtu mwenye uwezo wa kureason.. nalionea sana huruma Bunge letu la sasa..
 
Mwambie aende akamuulize baba yake Moh wapi alilipata jina la Abdallah. Akisha pata jibu amuulize Allah wapi alipo Moh. Then she can talk her bogus and diabolic words. Pathetic Anna.

Shimba mbona unatapika hivi... huyo mama ni mgalatia mwenzio
 
adhana si kero inasomwa hata dakika tano haimaliziki,mziki mda wote kanisani,tena makanisa haya mapya,mbona katoliki,angalikana,
hawana fujo?wanasali kistarabu?

unaishi mtaa gani? adhana toka saa kumi usiku, unasika amka hilo shuka ni sanda, chumba kaburi, karibu saa nzima makelele mtindo mmoja, hivyo hivyo saa saba mchana na saa kumi jioni kuna maustadhi wako standby wanapiga yowe karibu saa nzima kabla ya ibada.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom