Leo nilimsikiliza bungeni huyu mama akitoa wimbo mpya. Kwamba makanisa yamekuwa mengi na nadhani kwa kauli yake hiyo anahitaji yapunguzwe, sijui kiasi gani anajua mwenyewe. Jamani, kila siku tunaomba viongozi wetu hawa wa weigh out kauli zao kabla ya kuzitoa.
Hivi ngoja nimuulize tena mama Anna Abdalah, mbona sijawahi kusikia akilalamika kuwa vituo vya polisi vimekuwa vingi? Hivi anajua kazi za makanisa? Naona sasa anataka kuleta hoja kuwe na makanisa mangapi nchini??
Mama Anna kwa hili ulichemka kabisaaaaaa na tukisema ni udini unakusumbua utakataa? najua utakataa kwa kigezo cha majina yako lakini rohoni umejaza udini.:angry: