CCM hamjawahi kusema ni kwa VIPI CDM wanaendesha Chama Kidini.Zaidi sana mnadhani ni propaganda nzuri ya kupambana na CDM kumbe mnaigawa Nchi katika vipande vya kidini kitu ambacho kitaleta machafuko hapo baadae.Mwanzilishi wa Udini Tanzania 1). Mh.Alhaji Ally Hassani Mwinyi, 2) Ndg.Jakaya Mrisho Kikwete. Wamekuwa wakitumia misikiti kutoa ahadi kwa dini yao, na watu wao, na bado haikutosha, wameitumia CUF kueneza propaganda za kidini kupitia misikiti, ushahidi ulishawekwa jukwaani ukimwonesha Lipumba alichokuwa akikiongea msikitini. CDM haijawahi kupita, au kutumia Jukwaa lolote la kidini kuahidi chochote kwa jukwaa hilo la kidini.
kuhusu unayemwita dogo Mheshimiwa wa Kigoma, hilo suala ni la kipuuzi sana. CDM imefukuza wengi tu,kabla ya huyo Dogo, hatukuwaona CCM mkilalamika na kuwatetea, tunaomba kujua mna maslahi gani na huyu dogo wa Kigoma?Mmekuwa mstari wa mbele kumtetea, na kuona maamuzi ya CDM yalikuwa mabaya, yalikuwa yanawahusu nini hayo maamuzi?Pilipili usiyoila yakuwasha nini?Au mnataka tucopy na kupaste kile CCM wanachoshindwa kukifanya kwa kina EL na wengine ndani ya CCM?Dogo haki yake itaonekana Mahakamani, na Kamati kuu ya Chama kama ipo, kama haipo basi aangalie ustaarabu mwingine.
kuhusu kung'ang'ania madaraka, nadhani CCM imeng'ang'ania madaraka tangu 1964, hilo hamlioni?hatujawahi kuwasikia CCM wakimwongelea Lipumba ama Mbatia kwenye hili suala la Uongozi.CCM kuna watu ni viongozi tangu kabla ya baadhi yetu kuzaliwa hadi leo.Mzindakaya alikaa kwenye ubunge kwa zaidi ya miaka 40.Kingunge yupo serikalini tangu lini?Ina maana CCM ina watu wachache sana wenye sifa za kiuongozi hadi kupelekea watu kukaa madarakani muda wote huo?Niambie, CCM mnapochagua Mwenyekiti Taifa huwa anapambana na nani?Kwa nini?Uchaguzi ni suala ambalo pia linaweza kuahirishwa, kama ambavyo CDM wamesema watafanya mwakani baada ya uchaguzi, kuna kosa gani?Uchaguzi wa CDM una madhara gani kwa CCM au ndo mlishaandaa watu wa kuiua CDM?
Kujisahau kivipi?
Mwisho,kama mnategemea CDM kufa, endeleeni kujaza maji kwenye gunia.Haifi.Matokeo mliyoyapata ni sehemu tu ya changamoto zinazopitiwa na CDM. Kwa Taarifa yako, hakuna Anguko lolote la CDM, nionacho ni propaganda kwamba CDM imeanguka. Tunasubiri Anguko rasmi la CCM.Msidhani kuwa hatujui kinachoendelea ndani ya CCM.MLICHOFANIKIWA ni kuufunika moto unaowaka ndani yenu ila sisi tunaona moshi.
Naamini hakuna mahali nilipokutukana Mamndenyi![/QUOT
Padre slaa ni din gani eti!?