Huihui2
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 5,277
- 7,979
Madini hata wakati wake Magufuli yalikuwa yanaibwa tu, tofauti na sasa ni kwamba vyombo vya habari viko huru kuripoti bila woga.Hivi madini ya pesa nyingi kamaa hizi yanatoroshwa na kwenda kuunzwa nje mamlaka husika hazina taarifa, huu ni uzembe mkubwa sana.
Taifa linaibiwa rasilimali zake kama shamba la bibi.
Hayati JPM alidhibiti haya mambo. Maana huko nyuma hata Nairobi ndio ilikuwa soko kubwa la dhahabu ya Tanzania na ilikuwa inatoroshwa kama pipi.
Leo hii ruby ya bil 240 na ushee inatoroshwa kama vile mtu anavusha ubwabwa kwenye hotpot?
Kama angekuwepo hayati JPM vyombo vya ulinzi vingekuwa makini zaidi. Huu uzembe usingefanyika kabisa.
Pili hata Magufuli mwenyewe alikuwa mshirika kwenye uwizi wa madini kwa kushirikiana na Paul Kagame. Je unaikumbuka tukio la Magufuli kuingia gereza la Butimba na kuamuru watuhumiwa wa uvushaji dhahabu waachiwe? Kwa taarifa yako zilikuwa ni dhahabu zake na Kagame ila Polisi hawakujua ndiyo maana walizikamata