Midnight
JF-Expert Member
- Apr 24, 2021
- 229
- 675
Naandika ujumbe huu nikiwa na loss ya Kama 50k+ hivi.
Aisee kuna hivi vi-pub ushenzi vimemiminika kila baada ya mlango mmoja wa flem, yaani ni mwendo wa duka la nguo, pub, duka la chakula pub... Hivyo hivyo kwa nguvu ya 5G hadi hatulali na pesa siku hizi.
Sasa basi wamiliki wengi wa vi-pub hivi ni either ma barmaid wastaafu au mastistaduu waliokubuhuu kwenye shughuli za uchunaji, leo basi si nimejifanya kuwatoloka wana ukoo, nikasema ngoja nijichimbie hapo kijiwe nongwa jicho moja, mguu na meza upande duka la nguo upande salon ya kike, aisee kumbe mchezo wao sio wa kitoto yaani ukiagiza yako moja na yeye anachukua yake moja, ukinywa ya pili na yeye anakunywa nyingine Sasa nimeshtuka hapa nimeacha kumchekea chekea nataka anieleze hii bili ni yangu au yake maana sikumpa go ahead ya kujihudumia mwenyewe.
Kama mtaona kimya sana kesho mjue nitakuwa nimeungana na ndugu Sabaya, maana nataka nifanye ambush ya viwango vya Mwamposa hapa Pabun.
Aisee kuna hivi vi-pub ushenzi vimemiminika kila baada ya mlango mmoja wa flem, yaani ni mwendo wa duka la nguo, pub, duka la chakula pub... Hivyo hivyo kwa nguvu ya 5G hadi hatulali na pesa siku hizi.
Sasa basi wamiliki wengi wa vi-pub hivi ni either ma barmaid wastaafu au mastistaduu waliokubuhuu kwenye shughuli za uchunaji, leo basi si nimejifanya kuwatoloka wana ukoo, nikasema ngoja nijichimbie hapo kijiwe nongwa jicho moja, mguu na meza upande duka la nguo upande salon ya kike, aisee kumbe mchezo wao sio wa kitoto yaani ukiagiza yako moja na yeye anachukua yake moja, ukinywa ya pili na yeye anakunywa nyingine Sasa nimeshtuka hapa nimeacha kumchekea chekea nataka anieleze hii bili ni yangu au yake maana sikumpa go ahead ya kujihudumia mwenyewe.
Kama mtaona kimya sana kesho mjue nitakuwa nimeungana na ndugu Sabaya, maana nataka nifanye ambush ya viwango vya Mwamposa hapa Pabun.