Anasema nimuhudumie kila mwezi

Anasema nimuhudumie kila mwezi

Wakuu poleni na hongera katika shughuli zenu za hapa na pale

Sasa nimekuja kwenu, mnishauri mimi kama kijana wa kiume nisie na kazi na bado nawategemea wazazi kwa kuwa bado ninasoma

Iko hivi niko kwenye mahusiano na msichana kwa muda ambao ni kama miezi miwili tu.

Yuko chuo na mimi pia nipo chuo.

Sasa kilichonifanya kuja kwenu, anadai natakiwa niwe ninampa pesa ya kusuka kila mwezi kiasi cha sh 20,000 taslimu.

Na akaongezea ya kuwa kama sitampa hiyo hela hakuna mapenzi kwa sababu, haiwezekani niwe namtumia tu alafu nisiwe ninampa hela.

Isitoshe yeye anao mkopo na mimi ninao mkopo.

Lakini mimi sikai ndani ya chuo nipo nje nimepanga, nikipiga gharama za kodi na michango mingine kiukweli sitaweza toka na chochote katika pesa hii ya Boom.

Maana najitahidi nisave angalau visent kadhaa ili nikirudi kitaa nipate pa kuanzia.

Nimemshauri kuhusu swala la kukaa wote ili angalau tusave walau kiasi fulani, ili hapo baadae tuweze anzisha hata kabiashara, kama ikishindikana kuanzisha pamoja bhasi, kila mtu ataanzisha mradi wake na kama tuna malengo ya kweli tutaweza fika mbali, ukizingatia sasa hivi ajira ni changamoto.

Sasa naombeni ushauri wenu wakuu, Je hapo mimi kama kijana, ninae soma na kutegemea wazazi

Natakiwa nitoe 20,000 kila mwezi, nikishindwa nimeambiwa kutakuwa hamna mapenzi. Yatabakia ya mdomoni tu na mwisho yatakufa kabisa.

Ushauri wenu wakuu katika hili.
Ww umeambiwa ulipie pesa ya kusuka ,kuna mwenzako ameambiwa alipie bando la mwezi kuna mwenzako ameambiwa awe anatoa pesa ya kula kwa hiyo mmegawana majukumu ila ww huwajui wenzako na wenzako hawakujui ww kiufupi hamjuani, pole sana ,unachanganya mapenzi na elimu kuwa makini dogo. Hizo nyege mshindo zako zitakurudisha kwenu na kilo 2 achana na mambo hayo


Ww usitoe chochote na mpotezeee tu najua utaumia akiikuuliza vp mwambie cna pesa endelea na mambo yako Fanya kilichokuleta sio ulichokikuta,alafu zinaa dhambi mbele ya allah
 
Ndio mkuu, nilikua namsaidia baadhi ya mahitaji, sasa ameniambia sasa hivi niwe natoa 20,000 hata kama nikiwa likizo

Unawekewa vikwazo cha msingi fanya mambo ya maendeleo huku mtaani sio kuzuri kama huna pesa alafu mbaya zaidi huyo unaempa hiyo 20k siku ukishindwa kuitoa kutokana na hali halisi ya maisha hatokuelewa.
 
Nilimuuliza Je?, kama nikishindwa kukupa hiyo 20,000, akaniambia hakuna mapenzi labda ya mdomoni tu.

Sawa mkuu, wacha nimuache tu aendelee na maisha yake

Huyo hana mapenzi aliyokuwa nayo mwanzoni hiyo likizo kuna mjanja kakupiku.
Piga kitabu, wekeza for your future life ukiwa na hela mbona wanakujaga wenyewe tu we muone kama kashazeeka winda kafirst year kapya au used kwa mbali maisha yaendelee.
 
  • Thanks
Reactions: aad
Tumepita huko, wadogo zetu wamepita huko, marafiki zetu wamepita huko, watoto pia.

Nisikilize, hapo chuoni furahia mahusiano ila usiweke kambi, usiwekeze kwa mwanamke, usiwekeze na mwanamke.

Furahia mahusiano ila usiwekeze akili na muda wako hapo, usijifanye ww ni bingwa wa kupenda na kuhudumia, zaidi ya yote usijiingize kwenye mtego wa kusifiwa kuwa una demu mkali.

Usitengeneze mahusiano ukayakuza kwa kiwango cha kutambulika kama shemeji kwa marafiki wa mwanamke au yeye kuitwa shemeji na marafiki zako.

Furahia mahusiano ila piga shule, epuka kuongozana na mwanamke kama kumbikumbi. Kama mmeamua kushiriki katika tendo jikinge na usimwamini hata akiwa bikira. Usipagawe ukawekeza kwa binti uliyekutana nae chuo. Tulia, usiwe na papara.

Furahia mahusiano kirafiki zaidi, Usitumike kifedha ili upate ngono au sifa, kama ni lazima sana kushiriki ngono basi hakikisha una kinga na usiwekeze hapo kwa namna yoyote

Katika umri huo hutaona ila nakuhakikishia by 30 to 40 years utaelewa nilichokushauri.

Kumbuka pesa ya Boom ni mkopo utaurudisha.
 
kama hakunyimi mbunye mpe tuu ila kama hakupi kitu achana nae na ukimuona barabarani mpige mawe maana ni muhujumu uchumi.

nb.
mapenzi ya kulipa mshahara nimeachana nayo juzi juzi tuu.
 
  • Thanks
Reactions: aad
Wakuu poleni na hongera katika shughuli zenu za hapa na pale

Sasa nimekuja kwenu, mnishauri mimi kama kijana wa kiume nisie na kazi na bado nawategemea wazazi kwa kuwa bado ninasoma

Iko hivi niko kwenye mahusiano na msichana kwa muda ambao ni kama miezi miwili tu.

Yuko chuo na mimi pia nipo chuo.

Sasa kilichonifanya kuja kwenu, anadai natakiwa niwe ninampa pesa ya kusuka kila mwezi kiasi cha sh 20,000 taslimu.

Na akaongezea ya kuwa kama sitampa hiyo hela hakuna mapenzi kwa sababu, haiwezekani niwe namtumia tu alafu nisiwe ninampa hela.

Isitoshe yeye anao mkopo na mimi ninao mkopo.

Lakini mimi sikai ndani ya chuo nipo nje nimepanga, nikipiga gharama za kodi na michango mingine kiukweli sitaweza toka na chochote katika pesa hii ya Boom.

Maana najitahidi nisave angalau visent kadhaa ili nikirudi kitaa nipate pa kuanzia.

Nimemshauri kuhusu swala la kukaa wote ili angalau tusave walau kiasi fulani, ili hapo baadae tuweze anzisha hata kabiashara, kama ikishindikana kuanzisha pamoja bhasi, kila mtu ataanzisha mradi wake na kama tuna malengo ya kweli tutaweza fika mbali, ukizingatia sasa hivi ajira ni changamoto.

Sasa naombeni ushauri wenu wakuu, Je hapo mimi kama kijana, ninae soma na kutegemea wazazi

Natakiwa nitoe 20,000 kila mwezi, nikishindwa nimeambiwa kutakuwa hamna mapenzi. Yatabakia ya mdomoni tu na mwisho yatakufa kabisa.

Ushauri wenu wakuu katika hili.
Sasa kama bado mwanafunzi juu huna uwezo wa kupata 20,000/-
mapenzi ya nini?
Soma kwanza wanawake wapo tele ukishamaliza utampata mwanamke mzuri wa kumuoa.
 
  • Thanks
Reactions: aad
dogo nitumie namba yake nimuonye au nimwambie niwe nalipa iyo hela mwenyew
 
  • Thanks
Reactions: aad
Kila mwezi mkuu, hata kama nipo likizo
Mimi mwanamke akishaanza kuomba hela ambazo najua siwezi kumpaa tena mara kwa maraa.. Huwaga Mzuka unakataa kabisaaa so relation zangu zinakufaga natural death sababu Mizingaaa ikizidi ni keroo na kama siwezi kumpa wapo wanaowezaa so tusiumizanw kichwa
 
  • Thanks
Reactions: aad
Wakuu poleni na hongera katika shughuli zenu za hapa na pale

Sasa nimekuja kwenu, mnishauri mimi kama kijana wa kiume nisie na kazi na bado nawategemea wazazi kwa kuwa bado ninasoma

Iko hivi niko kwenye mahusiano na msichana kwa muda ambao ni kama miezi miwili tu.

Yuko chuo na mimi pia nipo chuo.

Sasa kilichonifanya kuja kwenu, anadai natakiwa niwe ninampa pesa ya kusuka kila mwezi kiasi cha sh 20,000 taslimu.

Na akaongezea ya kuwa kama sitampa hiyo hela hakuna mapenzi kwa sababu, haiwezekani niwe namtumia tu alafu nisiwe ninampa hela.

Isitoshe yeye anao mkopo na mimi ninao mkopo.

Lakini mimi sikai ndani ya chuo nipo nje nimepanga, nikipiga gharama za kodi na michango mingine kiukweli sitaweza toka na chochote katika pesa hii ya Boom.

Maana najitahidi nisave angalau visent kadhaa ili nikirudi kitaa nipate pa kuanzia.

Nimemshauri kuhusu swala la kukaa wote ili angalau tusave walau kiasi fulani, ili hapo baadae tuweze anzisha hata kabiashara, kama ikishindikana kuanzisha pamoja bhasi, kila mtu ataanzisha mradi wake na kama tuna malengo ya kweli tutaweza fika mbali, ukizingatia sasa hivi ajira ni changamoto.

Sasa naombeni ushauri wenu wakuu, Je hapo mimi kama kijana, ninae soma na kutegemea wazazi

Natakiwa nitoe 20,000 kila mwezi, nikishindwa nimeambiwa kutakuwa hamna mapenzi. Yatabakia ya mdomoni tu na mwisho yatakufa kabisa.

Ushauri wenu wakuu katika hili.
Kitu gani hiki cha kuomba ushauri?kwa hiyo unataka uwe unakula papuchi yake bure tu bila kugharamia?imekuwa sakrament ya ekaristi hiyo?
 
Back
Top Bottom