Anachokitafuta RC wa Kagera atakipata

Anachokitafuta RC wa Kagera atakipata

Kagera ni maskini kama mikoa mingine tu, kinacho iponza ni uwepo wa wasomi wengi

Halafu serikali inajivua jukumu la kupeleka miundombinu kwa kisingizio cha wasomi wa kagera watafanya

Sema ufala wa wanakagera ni ujuaji, yaani kila mmoja kagera ni mjuaji (iwe ndani ama nje ya mkoa )

Nimeenda bukoba mara ya kwanza mwaka 2011 nakuta mgogoro wa kujenga stendi (kuihamishia kule rwami/sido) nimeenda mwaka juz bado hakuna la maana ni ubishani tu (ujuaji wa kibwege )

Mzee wangu kafanya kazi hapo mwaka 78 tulikuwa nae mwaka juzi anasema hakuna mabadiriko ya maana toka ameondoka mwaka huo hadi leo

punguzeni ujuaji wana kagera
Miundo mbinu ipi mnahitaji,Barabara? Meli? Kiwanja cha ndege?
 
CHANZO CHA UMASIKINI KAGERA KWA MAWAZO YANGU NI TOFAUTI NA WATAWALA WANAOWAZA KISIASA.

Kinachonisikitisha ni kwamba kila anayepanda jukwaa kuelezea kinachoitwa umaskini wa Mkoa wa Kagera anakuja na ngonjera za wingi wa maprofesa na Ma-PhD holders kutoka mkoani mwetu.

Lawama zote zinarundikwa kwa watu hao na Wanakagera kwa jumla. Huo ndio utawala wetu ambao tumezoea kwa miaka mingi sasa. Watawala wanajifanya kama hawajui chanzo halisi cha kile wanachokiita umasikini uliokithiri mkoani humo.

Bila tafakuri yoyote ya "tafiti" zinazodaiwa kufanywa na Serikali, wanakuja tu na porojo za jumlajumla kuhusu "umasikini" huo. Tafiti hizo za kimangumashi hazielezei chanzo cha tatizo la Mkoa wa Kagera. Haziangalii matokeo ya Vita vya Kagera na uharibifu wa usalama na miundombinu uliosababishwa na ugomvi wa Serikali na Iddi Amin.

Kwamba shughuli za uzalishaji na kiuchumi zilikufa kabisa kutokana na vita hiyo. Hawaoni kwamba Serikali ilikosea (kwa makusudi) kutotangazwa kwa hali ya hatari mkoani humo, kwa maana ya kujenga miundombinu upya na kuwasaidia Wanakagera kurudia maisha yao ya kabla ya vita. Hawasemi Serikali ilifunga mpaka na Uganda, hivyo kusitisha shughuli zote za kiuchumi, ambapo soko kuu la mkoa wa Kagera lilikuwa Uganda.

Baada ya vita Ukimwi uliotokea Uganda ulimaliza nguvukazi kubwa ya mkoa huo kwa kupuputisha maisha ya maelfu ya nguvukazi wa Kagera. Wanajifanya hawajui kwamba MV.

Bukoba ilizama na kuua mamia ya watu, wengi wao wakiwa Wanakagera. Hapohapo, MV. Victoria "iliharibika" na kufanya Wanakagera kukosa kabisa usafiri wa kuwaunganisha na nchi yao, huku mazao yao ya kiuchumi yakishindwa kusafirishwa kwenda kwenye masoko makubwa ya kibiashara ya hapa nchini kama Mwanza na Dar es Salaam.

Serikali haikuona umuhimu wa kuwapa Wanakagera vyombo vingine vya usafiri ili wajimudu kiuchumi. Ndipo pia ulipoingia "Ugonjwa wa Mnyauko" wa migomba uliopigilia msumari wa mateso na umasikini wa Wanakagera. Yapata sasa zaidi ya miaka 15. Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwasaidia wakulima wa kilimo cha migomba mkoani Kagera? HAKUNA.

Wakati huohuo Wanakagera walikatazwa kuuza kahawa yao nchini Uganda ambako walikuwa wanapata bei nzuri kulingana na gharama za uzalishaji.

Waliopatikana na uvushaji wa zao hilo waliadhibiwa, ikiwemo vifungo au kufilisiwa, huko kahawa ikilimbikiziwa "TOZO" lukuki bila kutilia maanani gharama za wakulima za uzalishaji.

Wanasahau tetemeko la ardhi ambapo serikali haikusaidia chochote badala yake serikali ilisema nyumba wamezisukuma wenyewe wafe maana majanga makubwa yote uanzia Kagera kama UKIMWI na majanga mwngine makubwa hakuana msaada uliotolewa mbali na kunyang'anywa kidogo kilichopatika na kuzuia waliokuwa tayari kusaidia ndugu zao kuzuiwa kwa kile serikali ilichosema kuwa vitu vyote vikusanywe kwenye mfuko wa mkoa pale Boari lakini vile vitu viliyeyuka na wananchi kuambulia biskuti mpaka sasa watu wengi wanaishi kwenye turubai.

Kwa kagera kama ambavyo imekuwa ikifanya kwa baadhi ya mikoa ambayo iliwahi kupata majanga kama mafuriko, njaa nk.

Leo hii tunashuhudia jitihada za serikali kuhamisha watu kutoka kwenye hifadhi nakupelekwa kwenye kijiji ambacho imewaadalia wanakuta kila kitu sembuse wanakagera ambao walipata janga la tetemeko na serikali haikujali wala haikujiusisha kabisa na jambo hilo bali ilikuwa ni kuwazuia hata waliokuwa tayari kusaidia.

Hiyo ni mifano michache tu ya hujuma ya Serikali dhidi ya Mkoa wa Kagera kwa miongo mingi sasa. Matokeo yake ni nini? Wananchi wa Mkoa wa wa Kagera waliona Serikali ilikuwa haiwataki, haiwapendi. Wakasema isiwe taabu, wakaamua kuhamia mikoa nyingine nchini na kuwekeza huko.

Je Serikali inajifanya haioni uwekezaji wao mkubwa na uliotukuka katika mikoa mingine nchini, ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na kwingineko?

Serikali imekuwa ikipiga kelele nyingi eti Wahaya wameshindwa kujenga soko na kituo cha mabasi mjini Bukoba, ikijifanya haijui kwamba jukumu hilo ni lake na vyombo vyake, ikiwemo TAMISEMI.

Kwani vituo vya mabasi na masoko ya Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko vimejengwa na nani kama sio Serikali?

Nimalizie kwa kuishauri Serikali kwamba iwekeze mkoani Kagera kama ambavyo imekuwa ikiwekeza sehemu nyingine nchini. Ikiwekeza Kagera, kama ambavyo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imepanga kufanya kwa kujenga kitengo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), mkoani humo, basi itarajie kwamba maprofesa na PhD holders kutoka mkoani Kagera watarudi nyumbani kufaidi fursa za uwekezaji wa Serikali.

Ni matumaini ya wengi mkoani Kagera kwamba Mkuu mpya wa Mkoa wa kagera, Mhe. Chalamila ataelewa chanzo cha "UMASIKINI WA MKOA WA KAGERA".

Kwani ni mnataka wanakagera tujenge stendi na soko?

Kwani WASOMI mnaosema ni watumishi wa serikali? Wanakusanya kodi gani? Maeneo mnakopeleka miradi ya maendeleo kama stendi, soko na vyuo vikuu hakuna wasomi? Kigezo icho nichakikatiba?

Mwanza imejengwa viwanda kwakuwa hakuna wasomi? Arusha, Dodoma, Mbeya, Dar Es Salaam nk. Hakuna wasomi?

Mwambie Mkuu wa mkoa awaeleze ukweli wanaKagera kuwa umasikini na utapia mlo wanaousema Kagera ni mradi wa CCM ili waendelee kutawala.

Najua hamna majibu inawezekana mkanifungulia kesi nyingine kwakuwa nimesema ukweli mimi ni Muhaya na mzalendo wa Kagera nachukia unafiki na Majungu

Serikali timiza wajibu wenu acha kurukaruka kama maharage sufuriani.
kidogo wahaya wa bukoba mjini walisha ikataa ccm lakini wilaya zilizo baki uwambii kitu kuhusu ccm pamoja na kuwa susa sawa na wanyilamba wa singida na wanyatulu na tabora ccm aiwataki lakini wananchi vig,ang,nizi
 
Aliyesoma hiyo habari anifanyie summarization... All in all Kagera imejaa uchawi uvivu na ubaguzi vyote hivi husababisha Umasikini mkubwa ktk mkoa huo... Ndio maana huwez kukutana na Muhaya tajiri...
chunguza mika yote isiokuwa na wafugaji na wakulima wakazi wake wengi masikini
 
Vita ya Kagera (1978) Ila Kagera bado maskini Vs Rwanda Genocide (1994) Ila Rwanda Leo inapiga hatua kubwa za maendeleo, **punguza visingizio! Wana-Kagera wabinafsi na sifa za kijinga
tutajie mkoa wako kisha utaje wewe kama wewe umewekeza nini
 
Wengi ya wananchi wa Kagera wana Ushamba na Upuuzi,Ujinga. Hawajaelimika. Wachawi sana... Hilo ni tatizo kubwa pia. Mengine uliyoandika ni muendelezo wa ujinga huo huo wa miaka nenda rudi.
tutajie mkoa wako usio kuwa na wachawi na umasikini tujue kama unasema kweli
 
Kagera ni maskini kama mikoa mingine tu, kinacho iponza ni uwepo wa wasomi wengi

Halafu serikali inajivua jukumu la kupeleka miundombinu kwa kisingizio cha wasomi wa kagera watafanya

Sema ufala wa wanakagera ni ujuaji, yaani kila mmoja kagera ni mjuaji (iwe ndani ama nje ya mkoa )

Nimeenda bukoba mara ya kwanza mwaka 2011 nakuta mgogoro wa kujenga stendi (kuihamishia kule rwami/sido) nimeenda mwaka juz bado hakuna la maana ni ubishani tu (ujuaji wa kibwege )

Mzee wangu kafanya kazi hapo mwaka 78 tulikuwa nae mwaka juzi anasema hakuna mabadiriko ya maana toka ameondoka mwaka huo hadi leo

punguzeni ujuaji wana kagera
wewe mkoa wako ni hupi usio kuwa na wajuaji na masikini?amae shele maji soko sitendi vituo via afiaya wamejenga wananchi sio erikali
 
Hawakuwai kushtuka mapema kuona kuwa ubinafsi utawaletea umasikini.

Nilihadithiwa na mtu mmoja kuwa; kwenye maduka yao huduma ni kwa muhaya kwanza.

We mchaga utasubiri kwanza pembeni.
tutajie mkoa wako usio kuwa na masikini na wajuaji na kabila lako nilipi?
 
Ujuaji mwingi sana na ubaguzi mwingi, mimi nilisoma kule ilikuwa inafikia mwalimu anatumia kihaya kufundishia , kwani mnakuta darasa zima ambao sio wahaya mko kama 4 tu!!nenda mkoani pale hadi yule RC masawe, akapandika vibao "SPEAK KISWAHILI" yaani hata ofisini kwa wewe usiye mhaya kazi unayo' kule sio ILE ONDOKA USEMWE"Pale ni hata ukikaa hapo hapo utasemwa tu.Na wao wakishakutana tena wanaanza kubaguana kutegemea na eneo wanalotoka huko kijijini!!Tatizo lao kila mtu anataka aonekane anawazidi wengine , ili anyenyekewe!!!
kweli wahaya watu wabaya sana tafadhari nawe tutajie kabila lako hili tujue uzuli na ukalimu wenu na utajiri wenu
 
Maendeleo ya Kagera yatakuja iwapo mtaelewana kwanza ninyi wenyewe bado bifu za kitawala za kichifu zinawatesa kwenye maamuzi na kuwa wamoja. Mkiondoa uziba, uyoza, uyangiro, unyambo,.........mtapiga hatua haraka sana.
kabila lako tafadhari na mkoa wake ubaguzi wa wahaya umetaja sasa ni zamuyako tujue kabila lako
 
CHANZO CHA UMASIKINI KAGERA KWA MAWAZO YANGU NI TOFAUTI NA WATAWALA WANAOWAZA KISIASA.

Kinachonisikitisha ni kwamba kila anayepanda jukwaa kuelezea kinachoitwa umaskini wa Mkoa wa Kagera anakuja na ngonjera za wingi wa maprofesa na Ma-PhD holders kutoka mkoani mwetu.

Lawama zote zinarundikwa kwa watu hao na Wanakagera kwa jumla. Huo ndio utawala wetu ambao tumezoea kwa miaka mingi sasa. Watawala wanajifanya kama hawajui chanzo halisi cha kile wanachokiita umasikini uliokithiri mkoani humo.

Bila tafakuri yoyote ya "tafiti" zinazodaiwa kufanywa na Serikali, wanakuja tu na porojo za jumlajumla kuhusu "umasikini" huo. Tafiti hizo za kimangumashi hazielezei chanzo cha tatizo la Mkoa wa Kagera. Haziangalii matokeo ya Vita vya Kagera na uharibifu wa usalama na miundombinu uliosababishwa na ugomvi wa Serikali na Iddi Amin.

Kwamba shughuli za uzalishaji na kiuchumi zilikufa kabisa kutokana na vita hiyo. Hawaoni kwamba Serikali ilikosea (kwa makusudi) kutotangazwa kwa hali ya hatari mkoani humo, kwa maana ya kujenga miundombinu upya na kuwasaidia Wanakagera kurudia maisha yao ya kabla ya vita. Hawasemi Serikali ilifunga mpaka na Uganda, hivyo kusitisha shughuli zote za kiuchumi, ambapo soko kuu la mkoa wa Kagera lilikuwa Uganda.

Baada ya vita Ukimwi uliotokea Uganda ulimaliza nguvukazi kubwa ya mkoa huo kwa kupuputisha maisha ya maelfu ya nguvukazi wa Kagera. Wanajifanya hawajui kwamba MV.

Bukoba ilizama na kuua mamia ya watu, wengi wao wakiwa Wanakagera. Hapohapo, MV. Victoria "iliharibika" na kufanya Wanakagera kukosa kabisa usafiri wa kuwaunganisha na nchi yao, huku mazao yao ya kiuchumi yakishindwa kusafirishwa kwenda kwenye masoko makubwa ya kibiashara ya hapa nchini kama Mwanza na Dar es Salaam.

Serikali haikuona umuhimu wa kuwapa Wanakagera vyombo vingine vya usafiri ili wajimudu kiuchumi. Ndipo pia ulipoingia "Ugonjwa wa Mnyauko" wa migomba uliopigilia msumari wa mateso na umasikini wa Wanakagera. Yapata sasa zaidi ya miaka 15. Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwasaidia wakulima wa kilimo cha migomba mkoani Kagera? HAKUNA.

Wakati huohuo Wanakagera walikatazwa kuuza kahawa yao nchini Uganda ambako walikuwa wanapata bei nzuri kulingana na gharama za uzalishaji.

Waliopatikana na uvushaji wa zao hilo waliadhibiwa, ikiwemo vifungo au kufilisiwa, huko kahawa ikilimbikiziwa "TOZO" lukuki bila kutilia maanani gharama za wakulima za uzalishaji.

Wanasahau tetemeko la ardhi ambapo serikali haikusaidia chochote badala yake serikali ilisema nyumba wamezisukuma wenyewe wafe maana majanga makubwa yote uanzia Kagera kama UKIMWI na majanga mwngine makubwa hakuana msaada uliotolewa mbali na kunyang'anywa kidogo kilichopatika na kuzuia waliokuwa tayari kusaidia ndugu zao kuzuiwa kwa kile serikali ilichosema kuwa vitu vyote vikusanywe kwenye mfuko wa mkoa pale Boari lakini vile vitu viliyeyuka na wananchi kuambulia biskuti mpaka sasa watu wengi wanaishi kwenye turubai.

Kwa kagera kama ambavyo imekuwa ikifanya kwa baadhi ya mikoa ambayo iliwahi kupata majanga kama mafuriko, njaa nk.

Leo hii tunashuhudia jitihada za serikali kuhamisha watu kutoka kwenye hifadhi nakupelekwa kwenye kijiji ambacho imewaadalia wanakuta kila kitu sembuse wanakagera ambao walipata janga la tetemeko na serikali haikujali wala haikujiusisha kabisa na jambo hilo bali ilikuwa ni kuwazuia hata waliokuwa tayari kusaidia.

Hiyo ni mifano michache tu ya hujuma ya Serikali dhidi ya Mkoa wa Kagera kwa miongo mingi sasa. Matokeo yake ni nini? Wananchi wa Mkoa wa wa Kagera waliona Serikali ilikuwa haiwataki, haiwapendi. Wakasema isiwe taabu, wakaamua kuhamia mikoa nyingine nchini na kuwekeza huko.

Je Serikali inajifanya haioni uwekezaji wao mkubwa na uliotukuka katika mikoa mingine nchini, ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na kwingineko?

Serikali imekuwa ikipiga kelele nyingi eti Wahaya wameshindwa kujenga soko na kituo cha mabasi mjini Bukoba, ikijifanya haijui kwamba jukumu hilo ni lake na vyombo vyake, ikiwemo TAMISEMI.

Kwani vituo vya mabasi na masoko ya Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko vimejengwa na nani kama sio Serikali?

Nimalizie kwa kuishauri Serikali kwamba iwekeze mkoani Kagera kama ambavyo imekuwa ikiwekeza sehemu nyingine nchini. Ikiwekeza Kagera, kama ambavyo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imepanga kufanya kwa kujenga kitengo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), mkoani humo, basi itarajie kwamba maprofesa na PhD holders kutoka mkoani Kagera watarudi nyumbani kufaidi fursa za uwekezaji wa Serikali.

Ni matumaini ya wengi mkoani Kagera kwamba Mkuu mpya wa Mkoa wa kagera, Mhe. Chalamila ataelewa chanzo cha "UMASIKINI WA MKOA WA KAGERA".

Kwani ni mnataka wanakagera tujenge stendi na soko?

Kwani WASOMI mnaosema ni watumishi wa serikali? Wanakusanya kodi gani? Maeneo mnakopeleka miradi ya maendeleo kama stendi, soko na vyuo vikuu hakuna wasomi? Kigezo icho nichakikatiba?

Mwanza imejengwa viwanda kwakuwa hakuna wasomi? Arusha, Dodoma, Mbeya, Dar Es Salaam nk. Hakuna wasomi?

Mwambie Mkuu wa mkoa awaeleze ukweli wanaKagera kuwa umasikini na utapia mlo wanaousema Kagera ni mradi wa CCM ili waendelee kutawala.

Najua hamna majibu inawezekana mkanifungulia kesi nyingine kwakuwa nimesema ukweli mimi ni Muhaya na mzalendo wa Kagera nachukia unafiki na Majungu

Serikali timiza wajibu wenu acha kurukaruka kama maharage sufuriani.
Hili povu lako ni dhabiti na la kweli kabisa. Lakini mtoa povu nikupe kisa kimoja ili nyie wana kagera mjijue kwamba kinachowaangusha ni mbwembwe zenu, uvivu na kupenda sana chini badala ya kupiga kazi. Wakati wa vita kuu ya pili ya dunia ujerumani ya hitler na wajerumani walipondwa pondwa sana na majeshi ya ulaya na marekani. Nchi yote iligeuka kifusi. Lakini miaka 10 baadae, ujerumani iliamka tena na kuwa taifa kubwa ulaya licha ya vikwazo walivyowekewa. Jamaa walipiga kazi hasa.
Sasa nyie wakora waitu, vita ya kagera iliisha zaidi ya miaka 40 iliyopita, bado mnaitumia kama kigezo cha umasikini wenu?

Kutokana na uvivu na makidai yenu huenda ndiyo maana magufuli alikataa kuwapa ile michango ya tetemeko.

Eti unataka serikali iwapendelee. Serikali gani inapendelea wavivu? Mwafaaaaa
 
wewe mkoa wako ni hupi usio kuwa na wajuaji na masikini?amae shele maji soko sitendi vituo via afiaya wamejenga wananchi sio erikali
huwezi kuwq unatoka mkoa wa kagera wewe hata kuandika hujui hahahaha
 
Kilichoua na kinachoendelea kuua Tanzania ni Ujamaa na sera zake. Kila kitu serikali hiki, serikali kile, Pembeni ya nyumba yako umetupa taka mpaka kumeweka dampo unaulizwa nini kifanyike, jibu ni serikali ije kusafisha. Ujamaa umeua independent thinking.

Vita si sababu ya kufanya miaka 45 mbele balo sehemu ipo vile vile. Hiroshima ilidondoshewa atomic bomb ilioua maelfu na aftermath ilikuwa ya kutisha kuliko vita vyovyote vilivyowahi kutokea na kuifanya Japan kuwa masikini kushinda Tanzania kipindi hiko. Lakini leo hii hakuna jiji la Tanzania linalofikia Hiroshima, leo hii unataka kutuambia vita vya Kagera ndo kumefanya mkoa uwe masikini mpaka leo?

Tuache kulalamika, tujue maendeleo hayaji kwa mdomo, bila kazi kufanyika na kupunguza vizingiti vya biashara watu wafanye kazi kuinua maisha yao

View attachment 2345872
Hiroshima before and after; Unaniambia Kagera imepitia crisis kubwa kuliko hii?

Kwa hiyo miundo mbinu ya Hiroshima baada ya vita imejengwa na watu binafsi??
 
😳 Aliyesoma hiyo habari anifanyie summarization... All in all Kagera imejaa uchawi uvivu na ubaguzi vyote hivi husababisha Umasikini mkubwa ktk mkoa huo... Ndio maana huwez kukutana na Muhaya tajiri...
Mkuu ulipiga kwenye mshono.
"Mnyamahanga" ukihamishiwa kufanyia kazi Kagera, utapigwa vita vya ukabila na fitina hadi uhamishwe ama ufukuzwe kazi.
 
Wahaya ni watu wema ingawa ukikuta mhaya mwenye roho mbaya ya ubaguzi ni mbaguzi hatari.

Sana, Wahaya wanatafunwa na roho mbaya ya ubaguzi na upendeleo.

Ila mambo mengine siyo tatizo.

Mkka wa Kagera binafsi naona unafanana na Kilimanjaro. Hawapendi kufanya maeneo yao kugeuka Urban areas lakini wanapenda kukimbilia mijini.
kweli wahaya wanaroho mbaya sana vipi wewe kabila lako mko na roho nzuli? tutajie hilo kabila lako
 
Back
Top Bottom