Mimi kuna mambo mengine naonaga wanawalaumu wasomi wa Kagera kimakosa sana. Pengine ni kimkakati ili kuendelea kufunika lengo la serikali kuubakisha mkoa wa Kagera nyuma. Hii inafanya kimakusudi kuharibu mindset za watu watoke katika kuwazia mipango ya serikali ikae kuwawazia watu mmoja mmoja wa Kagera.
Imagine watu wa kawaida na wanasiasa wanasema Kagera pamoja na kuwa na wasomi wengi imeshindwa kuwa na stend nzuri ya mabasi! Usomi unawasaidia nini? Ila ukiwauliza ni mkoa gani ambao wenyeji wa mkoa huo wamejijengea stend yao?
Wanasema sijui soko, siju miundo mbinu mjini, n.k wakiihusisha na usomi wa wahaya. Kuna kabila ambalo limejenga soko mjini kwao??
Kama hao maprofesa mnaowasema kuwa ni wasomi uchwara na hawajaleta maendeleo Kagera, mbona wao mmoja mmoja wako vizuri sana na familia zao na koo zao? Umeshaenda katika vijiji vya wahaya? Umeshaona walivyojijenga? Unaweza kulinganisha na mkoa gani tofauti na Kilimanjaro?
Suala la maendeleo ya jumla ya jamii ni jukumu la serikali. Serikali isijiegeshe kwenye kauli za ubaguzi. Wameshawahi kutenga bajet ya kujemga stend mpya ya kisada hela zikaliwa na hao wahaya maprofesa? Mbona mikoa mingine, tena hadi wilaya tu za mikoa wanapeleka hizo fedha?
Yaani wanasema Bukona mjini hamna hata taa za barabarani usiku, alafu mtu anasema PAMOJA NA USOMI WOTE WA WAHAYA, as if ni jukumu la mtu binafsi kuweka taa barabarani.
Mkoa hauna chuo kikuu pamoja na kuwa ndo mkoa ambao bado unasukuma wasomi wengi zaidi katika mfumo wa elimu wa taifa kuliko mikoa yote, lakini mtu badala ya kuoiga kelele serikali ifanye juhudi za kuketa chuo ili watoto wakasome ana kazi ya kuwananga ma doctors na wasomi wa kihaya kwa sababu tu ya chuki zake. Mnaweza kutwambia mkoa ambao wananchi wake wamejenga chuo kikuu??
Kahawa inazalidhwa Kagera lakini miaka yite mnada wa kahawa badala ya kufanyika Kagera eti ulikuwa unafanyika Moshi. Yaani kahawa ya Bukoba mpaka ipelekwe Kilimanjaro kuuzwa. Hili nalo ni la wasomi? Wizara zinakuwa hazioni? Kuna mambo mengi sana ya hovyo yanafanywa na serikali kuirudisha Kagera nyuma. So sad
Serikali imeitupa Kagera miaka mingi sana na kimakusudi kabisa. Zifanyike juhudi za wazi kuiamsha Kagera, na sio hizi propaganda za kuwalaumu watu wa Kagera kwa kuwa na akili za darasani na kudoma sana. Kwani ni makosa?? Wamevunja sheria gani??