Ana kwa ana na Mwigulu Nchemba: Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Nitafute nikufafanulie maana inaonekana HUJUI KABISA

Halafu we Mwigulu acha utoto we dogo, umeleta uzi hapa jukwaani kwa mbwembwe na ukasema utatoa majibu, saa unataka watu wakufuate ukatolee majibu pembeni!

Kwanini badala ya kuleta uzi hapa usingewaalika watu huko pembeni ukawajibie huko? Huna uwezo wa kujibu maswali ya msingi, na sio ww tu, ni kuanzia mwenyekiti wako mpaka wanaccm wenzako wote. Ndio maana mnaishi kwa kujipendekeza ili mpate ulaji.
 
Wakati unamwita Abdul ni Kinyago ulikuwa unajua kuna kwenda Mbinguni?

Unaweza kuongeza hata unywele tu kwenye mwili wa Abdul?

Vipi ulishatubu juu ya hili?

Wakati fulani ukiwa Waziri wa internal affairs ulisema miili iliyokutwa baharini ni ya wahamiaji haramu

Ni wapi kwenye dunia hii muhamiaji haramu adhabu yake ni kifo?
Kesho Siku ya IBAADA KATUBU KWANZA NDIO UWATAZAME WENGINE. MAANA MBINGUNI HATUTAKWENDA KWA KUWAHUKUMU WENGINE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahaahah Maxence Melo inabidi utuwekee jukwaa ..la WANAOOMBA UTEUZI kwenye serikali yetu TUKUFU :cool::cool::cool::cool::cool:🤣🤣🤣.. tupo wengi aisee...likiwekwa, unataja tu mimi Becky nakuomba Magufuli uwaziri wa kupika visheti..yeye anapitia maprofile yetu afu anachagua….hahahaaaaaaaaaaaaaaaa
Kweliii... Maxence Melo NAUNGA MKONO HOJA
Mbunge wa Ukonga Mwita Waitara,Harmonise,Diamond na Mwigulu na wengine
 
Ukiwa kama mchumi na naibu waziri wa zamani fedha, unaonaje uelekeo wa uchumi wa nchi yetu?

Ukiwa kama Mbunge wa Iramba kwa miaka mingi, umewafanyia nini wana Iramba..?

Ukiwa kama Waziri wa zamani, hivi mkikaa kwenye vikao vya baraza la mawaziri mnajadili nini vyenye manufaa kwa watanzania hawa masikini??

Ukiwa kama msomi uliyebahatika kuwa Waziri, upi mchango wako na alama kama msomi uliyoiacha mahara na tunaweza sema hapa hii ni Mwigulu legacy..?

Yale maandishi ya chagua Mwigulu kwenye miundo mbinu yetu kama madaraja na barabara, Je ni wewe ndiye uliandika kwa kutuma vijana? au ni mashabiki wako? Je unajisikiaje kwa uchafuzi ule uliohujumu miundo mbinu na umechukua hatua gani..?

Watoto wako wanasoma International school fedha pale kama sijakosea, Tunaanzaje kupima Uzalendo wako huku watoto millions wa watanzania wanasoma Govt schools..??

Kwanini unaishi Dar es salaam halafu ukawa mbunge wa Iramba??

Nitarudi tena Mh, maswali ni mengi sana..
Akikujibu ni-Tag
 
Yes, HILI NI TATIZO, HII NI HOJA YA MSINGI.

Tar 20 tulikuwa na mjadala mpana SINGIDA, TATIZO HILI LINAWEZA KUPUNGUA KWA KUWEKEZA KWENYE MODERNIZATION OF PRODUCTION PRICESS MIKOANI KWETU, ILI SHUGHULI ZA UZALISHAJI ZITOE FAIDA ZINAZOLIPA HIVYO niZITENGENEZE AJIRA. HIVYO TULIKUWA NA RCC. TULICHAKATA SANA.

BUT AJIRA NI TATIZO NA NI MAADA PANA SANA, HAINA JIBU MOJA

Huna majibu ya tatizo la ajira ww na hao wenzako mliokaa kujadili, sana sana mlikuwa mnapiga porojo ili mpate maneno ya kuuza kwa wananchi wenye uelewa finyu. Nyie wenyewe bado mnanyenyekea ajira zilizopo, mtawezaje kupata ufumbuzi wa ajira mpya? Kwa ujumla uwezo wenu sio wa kupata ufumbuzi wa tatizo la ajira, bali uwezo na akili yenu upo kuifanya ccm iendelee kukaa madarakani kwa mbeleko ya vyombo vya dola.

Mfano mrahisi wa kwamba ww huna suluhisho la ajira nchi hii, ni wakati ulipokuwa waziri ulikuwa unategemea madaraka yako kuifanya Singida United kufanya vyema, ila ulipokosa uwaziri tu, tayari timu hiyo inayumba. Nilitarajia ww kama mchumi uendeshe timu hiyo Kisomi, lakini bado ni timu inayotegemea vyanzo vya unapokuwa na cheo! Katika mazingira hayo ww una jipya lipi la ajira mpya ndani ya nchi hii?
 
Kuna mtu ametupia uzi kuwa siku hizi sivai skafu, huu ni mkutano mkuu wa juzi tarehe 19/2/2020 wakati wa ziara ya mzee Mangula. Skafu nilikuwa navaa hata kabla ya kwenda Ilboru Sekondari haikuwa sare ya Uwaziri.

View attachment 1365715

Kama kuna maswali kunihusu, nitayajibu hapahapa
Mzee Lwakatare na familia yake kesho wanaenda kanisani kutoa shukrani kwa Mwenyezi Mungu kutokana yaliyotokana na kesi ya Ugaidi uliyoitunga kwa kushirikiana na Ludovic , subiri malipo ya Mungu
 
Yuko wapi Ben mwana wa saa 8? Hakika damu yake itakuwa juu ya kizazi chako.. Wewe ni mzazi, hebu jiweke katika nafasi ya wazazi wa Saanane, wewe ni baba na ni mme hebu jiweke katika nafasi ya familia ya Azory Gwanda.

Hawa watu wamepotea ukiwa wewe una dhamana ya kulinda watu Hawa.

Angalia watoto wako angalia mke, angalia wazazi wako wanafuraha pindi wakuonapo mzima, linganisha na hizo familia mbili, wambieni Hao wazazi, watoto, wake sehemu walipo ndugu zao hata kama wamekufa basi waonyeshe hata mabaki ya miili yao ili wawapumzishe ndugu zao kwa heshimu sehemu inapostahili bila hivyo hakika damu hii itakulilia wewe na kizazi chako..

Husiharibu future ya kizazi chako kwa mambo yasiowahusu.
Tenda uugwana Sema unalofahamu juu ya watu Hawa, vyeo vinapita, Leo umesimama kesho waweza lala chini kwa mateso.. Zingatia Karma.....
Umeongea kwa hisia sana mkuu...pole sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kitu ambacho nimegundua mweshiwa anachagua maswali marahisi..kwa maana nyingine anapiga chabo...anasahau yale maswali magumu ni compulsory kujibu...

mweshimiwa amza yako ya kugombea nafasi ya urahisi imeishia wapi?????? umeghairi au muda bado?????????????
 
Safi sana mkuu kada mtiifu.Swali langu ni hili: Hivi kuna ukweli wowote kua ili ufanikiwe kwenye siasa asa kupitia CCM ni lazma ufanye dhuluma, visasi na fujo?

Mwisho, hivi unajua kua Mh. Lissu hakufa na kuna uwezekano mkubwa ukatangulia wewe huko?

Ahsante
 
Mwigulu; wewe ni mlezi wa Singida Utd, but una tabia ya kuchukua wachezaji wazuri wa Singida kisha unawapeleka Yanga, huoni kwa kufanya hivyo unaihujumu Singida Utd kwa kuipunguza nguvu, now iko chini kwenye nafasi za kushuka daraja?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakua mwaka 2015 ulionyesha nia na ukaingia kwenye kinyanganilo cha uchaguzi ndani ya chama je mwaka huu 2020 utaingie tena kwenge kinyanganyilo ndani ya chama kuwanaia nafasi ya kupeperusha bendera ya chama
 
Kuna mtu ametupia uzi kuwa siku hizi sivai skafu, huu ni mkutano mkuu wa juzi tarehe 19/2/2020 wakati wa ziara ya mzee Mangula. Skafu nilikuwa navaa hata kabla ya kwenda Ilboru Sekondari haikuwa sare ya Uwaziri.

View attachment 1365715

Kama kuna maswali kunihusu, nitayajibu hapahapa
Kwanza nakupongeza kwa kuja kujadiliana hapa na kujibu maswali hilo ni jambo zuri sana tunapenda viongozi wetu muwe mnajitokeza kuweza kupeana just habar

Pia watu tujitahidi kuuliza maswali ya msingi dharau haisadii kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom