Ana kwa ana na Mwigulu Nchemba: Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

Mheshimiwa!

Kwanza nakusalimia na pili nakupongeza kwa ushujaa wako wa kukubali mdahalo na wehu wa humu JF,

Wengi wao humu bila kuuma maneno ni waliopagawa na kuchanganyikiwa hasa baada ya awamu ya tano kuziba mirija yote ya ujanja ujanja.

Na sasa wameigeuza JF kuwa platform ya wamwaga sumu.

Usidhani JF hii ndio ile tulioianza miaka ile ikijaa mijadala yenye afya na hoja zenye mashiko la hasha.

Hii JF ya sasa imegeuka kuwa platform ya wapingaji wa kila kitu,na imeporomoka kwa kasi sana.

Naomba uwe mvumilivu.

Karibu sana tuko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe kwisha habari yako, ulinyanyasa na kuwatesa sana watu, ulijivua ubinadamu, ukajivisha ukatili, ukasahau kuwa cheo ni dhamana. Leo upo Unaishi kwa hofu ya kupoteza ubunge. Pole sana. Ndio ujifunze. Wakati mwingine usiwe limbukeni wa cheo. Waambie na wenzako.
Hii ndiyo Dira, asipoizingatia basi atakuwa mburula
 
Nitafute nikufafanulie maana inaonekana HUJUI KABISA
Umesema watu wakuulize maswali na utawajibu.

Watu wanakuuliza maswali halafu unasema wakutafute ndio utawajibu. Je wakutafute wapi zaidi ya hapa? Na kwanini unashindwa kuyajibu hapa jukwaani ili kila mtanzania ajue ukweli badala yake unakwepa kwa ujanja ujanja?


Wewe kama ni msomi jibu kila swali kwa maelezo yanayojitosheleza. Jitofautishe kwa kuonyesha credibility yako na sio unajibu maswali kihuni huni.

Sincerely yours,

Andresen, Next President of URT .
 
Mwambie aje afute maneno yake hayo hapa Ruvu Darajani!
Mh Rais JPM aliwahi kukuambia ukafute maandishi uliyoyaandika au kuwatuma vijana wako wakachore kwenye mawe hasa yaliyo kando mwa barabara karibia nchi nzima yaliyoandikwa kwamba wewe ndio Rais 2015, Je umefanya hivyo? na kama hujafanya hivyo ni dharau umeamua kuonesha kwa Mwenyekiti wa chama na Rais wako?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mheshimiwa!

Kwanza nakusalimia na pili nakupongeza kwa ushujaa wako wa kukubali mdahalo na wehu wa humu JF,

Wengi wao humu bila kuuma maneno ni waliopagawa na kuchanganyikiwa hasa baada ya awamu ya tano kuziba mirija yote ya ujanja ujanja.

Na sasa wameigeuza JF kuwa platform ya wamwaga sumu.

Usidhani JF hii ndio ile tulioianza miaka ile ikijaa mijadala yenye afya na hoja zenye mashiko la hasha.

Hii JF ya sasa imegeuka kuwa platform ya wapingaji wa kila kitu,na imeporomoka kwa kasi sana.

Naomba uwe mvumilivu.

Karibu sana tuko

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata shetani ana wafuasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
vipi kwenye maombi ya lissu?, matisho yako yalisaidia kuwanyamazisha waombaji wenye kumuombea lissu kupona?.unasemaje kuhusu kupona kwa lissu licha ya wewe kuwatisha na kuwaonya wale wote waliokuwa wanamuombea apone?, je unahabari jamaa kapona licha ya risasi zote zilizompata mwailini na ukazuai waombaji kumuombea apone ?
 
Wewe kwisha habari yako, ulinyanyasa na kuwatesa sana watu, ulijivua ubinadamu, ukajivisha ukatili, ukasahau kuwa cheo ni dhamana. Leo upo Unaishi kwa hofu ya kupoteza ubunge. Pole sana. Ndio ujifunze. Wakati mwingine usiwe limbukeni wa cheo. Waambie na wenzako.
Tupe ushahidi wa hayo usimsingizie mtu kwa sababu ya kumpaka matope kisa watu wengi watasoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtu ametupia uzi kuwa siku hizi sivai skafu, huu ni mkutano mkuu wa juzi tarehe 19/2/2020 wakati wa ziara ya mzee Mangula. Skafu nilikuwa navaa hata kabla ya kwenda Ilboru Sekondari haikuwa sare ya Uwaziri.

View attachment 1365715

Kama kuna maswali kunihusu, nitayajibu hapahapa
Swala la wewe na skafu ni dogo sana, ukupaswa kulitolea ufafanuzi hapa......
Leta vitu vya MAANA ...kutoa IRAMBA......uchaguzi upo mlangoni ...
 
Ukipenda kitu sio lazima imsaidie mtu, kwani unapovaa jezi ya Chelsea au Man u huwa inatusaidia Nini hata UINGEREZA HUJAFIKA. MIMI NAJIVUNIA UTANZANIA WANGU, HIYO BENDERA YA TAIFA
Mh.Mwigulu,wakati unasoma Ilboru kulikuwa hizi skafu?Ilikuwa part of school uniforms?

Pia nahisi kuna baadhi ya maswali ya msingi ambayo yanahitaji majibu haujayajibu.Will you?
 
Habari Mheshimiwa,

Tunashukuru kuona umeamua tena kujitokeza hapa JamiiForums kushiriki mijadala na sisi.Binafsi nina jambo moja tu nalopenda utueleza na hili ni lile linalohusiana na tukio la Lissu kushambuliwa kwa risasi pale Dodoma ingawa kuna mengi zaidi yanayohitaji majibu kuhusiana na tukio zima.

Wakati Tundu Lissu anapigwa risasi,wewe ndio ulikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani mwenye dhamana ya usalama wa raia na mali zao.

Hata hivyo,mpaka unaondolewa uwaziri sina hakika kama uliwahi kuwaeleza watanzania kupitia Bunge au Waandishi wa habari juu ya nini hasa kilipelekea camera za CCTV katika jengo lilokuwa karibu na eneo la tukio kuondolewa na ziliondolewa na nani na pia zilepelekwa wapi.

Jambo lingine,ulishindwa kuwaagiza hata waliokuwa chini yako(Polisi) kutoa ufafanuzi kwa umma ni nilni kilipelekea zile camera kuondolewa?

Je,siku ukiingia utawala mwingine,huoni hata wewe unaweza kuja kuwa ni mmoja wa watu watakaotakiwa kusaidia upelelezi wa tukio hili?
 
Kuna tuhuma kwmba kuna wakati ulikuwa ukiwasomesha watoto waliofaulu kwenye jimbo lako. Lakini ukaishia mitini baada ya baadhi kudai ada. Yupo mmoja alikuwa Bwiru Girls mpaka leo hajachujua vyeti vyake kwa sababu alishindwa kumalizia malipo pale shule.

Hili limekaaje mheshimiwa Mwigulu Nchemba?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Mwigulu Nchemba kwa hulka yake, angefanikiwa kuwa Rais wa Tanzania angekuwa ni Dikteta mbaya kuliko hata Magufuli. Kiwango chake kingekuwa cha Iddi Amin Dada.

Ukisoma posts zote utagundua kuwa members wanamuhusisha na mauaji kuanzia akiwa Naibu Katibu Mkuu CCM Bara wakati Emmanuel Nchimbi akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani na kipindi cha JPM na yeye Mwigulu akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Namuona Mwigulu kuwa siyo mvumilivu wa kukosolewa ndiyo maana amekuwa ndiye master mind ya utekaji na mauaji.
 
Wanasiasa hawaaminiki. Nimepita kurasa zote,hakuna alilojibu! Anarukaruka tu kama kuku alokatwa kichwa. Abdul Nondo njoo pande hii, Mh Mwigulu anasema alikuokoa,ilikuwa upotee kwa demu wako. Leta ushahidi kama ni kweli,au naye alihusika ili akuokoe baadaye. Nimekumbuka yale Mh Makonda na kupotea kwa Roma
 
Je, Ni Lini UTAWAOMBA RADHI Wapinzani kwa kuchana HOTUBA YA UPINZANI BUNGENI Huku ukijiita wewe MCHUMI DARAJA LA KWANZA ?
 
Back
Top Bottom