Ni sawa ila kwa kipindi hiki ni bora akakae kwa wazazi wake mpaka hiyo Jumapili.Kwanza ni hatari kuendelea kukaa nyumba moja kabla ya utatuzi wa jambo hili,Mkijibizana kidogo hasira uliyo nayo inaweza kukupeleka usikotarajia.Kama wazazi wanakaa mbali wasiliana nao akae hata kwa ndugu wa upande wake alie karibu;Ni kipindi kigumu jitahidi sana kucontrol temper na usinywe pombe nyingi kama ni mnywaji.Mlikuwa na ndoa inayotambulika? Huyo anaekwenda kuzungumza nae aondoke nae.Tumia huu muda mpaka Jpili kutafakari moyo wako unataka nini.Mwisho wa siku mwamuzi ni wewe ingawa kila mtu anaweza kukupa mawazo tofauti utakepima ni wewe kuona muamue nini kama hatima ya ndoa yenu.Pengine kadanganywa akifikiri kwa graduate mwezie maisha yangekuwa bora kumbe sivyo but ni LAZIMA awe muwazi kwako ni wapi alikuwa na kwa nini afanye hivyo.Vitu alivyofungasha karudi navyo?Kuna type ya wanawake huwa wanakusanya na kutoroka na vyombo vya nyumbani kila wakati na kurudi kuomba msamaha maisha yakishakuwa magumu.asikupitishe njia hiyo-hutapiga hatua!Pole sana