mtu mmoja alitumwa na mjomba wake aende sehemu fulani akamletee mwanamke, alipofika mwanamke akawaambia ataondokaje hajaacha pesa nyumbani, jamaa akampigia mjomba wake, mjomba akamwambia mpeni 50,000/- akawa hana lakini dereva wa tax akawa nazo wakampa kisha wakaondoka.
walivyofika hotelini wakaendelea na starehe za kawaida tu kula kunywa kisha jamaa akaondoka mjomba akajitwisha zigo lake ndani.
asubuhi mjomba akamuaga yule binti na 250,000/- ikabidi jamaaa apige kelele kwamba mjomba unahonga sana, mjomba mtu akamuuliza kwani wewe huwa unahonga ngapi, dogo akajibu ikizidi sana 10,000/- ukionga 10,000/- unabaki na ngapi, akadai naweza kubaki na 5000 akamwambia mjomba unahonga sana.
nini nataka kusema 4m inaweza kuwa haina thamani halisi kama 70,000/- kwakuwa kabla mahali haijapangwa huwa inafanywa tasmini ikiwa mwowaji anatoka katika familia gani na wanajiweza kwa kiasi gani.
lengo kubwa ni kupunguza dharau isionekane alimpata kirahisi mno na hii inamjengea heshima mwowaji na mwolewaji. nakumbuka tulivyo kuwa tunasoma shule ya msingi wanawake wa kabila fulani walikuwa rahisi ukienda na mia tano unapewa mke sasa fikiria nilikuwa darasa la tano lakini niliona wamedharauliwa.
hivyo toeni tu kwani hata huyo wa 70,000/- aliomba apunguziwe ndo ikafika hapo