Ally Hapi: Vijana msiogope kuoa, wanawake ni wengi. Anayetelekeza watoto ni mwanaume suruali

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,511
8,147
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa, Ally Hapi amewataka Wanaume kuacha kutelekeza Watoto huku akiwasisitiza Vijana kuoa .

Hapi amesema hayo akiwa Mkoani Singida May 10,2024 ambapo amesema “Nataka tuone mkakati kweli tuna tatizo kubwa la Watoto wa Mitaani na sio Singida tu ni kote Nchini, Vijana tumekuwa Mabingwa wa kufanya yale mambo, Watoto wakipatikana unajifanya upo bize hutaki kulea, meseji yangu kwa Wababa na Vijana hakuna jambo baya kama kutelekeza damu yako, mbaya sana, kuzalisha Mwanamke ukamtelekeza Mtoto ni mbaya sana”

“Wakina Baba tutunze Watoto, kila anayejua ana Mtoto wake amemtelekeza sehemu tukitoka hapa mtafute Mtoto wako mtunze usitelekeze damu yako, Mwanaume imara na shupavu hatelekezi Watoto, wewe ukiona unatelekeza Watoto ni Mwanaume suruali, baadaye Watoto wakifanikiwa mnaanza ooh tuyamalize”

“La pili Vijana tuoe, Vijana sasa hivi tunaogopa kuoa, Wakina Mama na Wadada ni wengi kuliko sisi wewe unakaa gheto unajipilikisha, ushajua kukanda maandazi na chapati, unakaanga mpaka rosti kwanini huoi?”
 
Wanaokimbia watoto ni watoto wa kike Wenye sura na maumbile ya kiume. Hakuna mwanaume duniani anakimbia mtoto.

Nina rafiki yangu, mwaka 2020 alipata mtoto akakimbia, akanitafuta akaniomba ushauri, nikamwambia kaka njia nzuri ya wewe kukua kiakili na kutambua nini unahitaji katika hii dunia ni kumchukua huyo mtoto umlee kwa namna yoyote ile hata kama ni kwa kulala wewe njaa ila nenda ukafate damu yako.

Jamaa ikabidi amtoe mtoto na mwanamke kwao akaanza kukaa nyumbani kwao vyumba vya nje, akamwambia baba yake anataka kuishi kama mpangaji ajipime uanaume wake( nilicheka sana kipindi ananihadithia hili) akaanza kuishi kwao analipa kodi , akiamka asubuhi anaona mtoto analia inamkumbusha aaamke kwenda kutafuta, ikafika wakati anakosa hata nauli ya kwenda kwenye shuguli zake, Mke wake ikabidi aanze kuuza chakula mama ntilie. Akawa anamuomba mpaka nauli Mke wake.

Ananiambia passion kiukweli katika kipindi akili ilikomaa na kukua ni kipindi nilipokubali kubeba jukumu la kuwa mwanaume.

sasahivi yupo CCTTFA ( central corridor transit transport facilitation Agency) anamuendesha kigogo mmoja pale na alishajenga yupo dodoma.

Tatizo la vijana sio wote baadhi hatutaki kutoka kwenye comforts zone zetu na ku embrace disruption za dunia.
 
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa, Ally Hapi amewataka Wanaume kuacha kutelekeza Watoto huku akiwasisitiza Vijana kuoa .

Hapi amesema hayo akiwa Mkoani Singida May 10,2024 ambapo amesema “Nataka tuone mkakati kweli tuna tatizo kubwa la Watoto wa Mitaani na sio Singida tu ni kote Nchini, Vijana tumekuwa Mabingwa wa kufanya yale mambo, Watoto wakipatikana unajifanya upo bize hutaki kulea, meseji yangu kwa Wababa na Vijana hakuna jambo baya kama kutelekeza damu yako, mbaya sana, kuzalisha Mwanamke ukamtelekeza Mtoto ni mbaya sana”

“Wakina Baba tutunze Watoto, kila anayejua ana Mtoto wake amemtelekeza sehemu tukitoka hapa mtafute Mtoto wako mtunze usitelekeze damu yako, Mwanaume imara na shupavu hatelekezi Watoto, wewe ukiona unatelekeza Watoto ni Mwanaume suruali, baadaye Watoto wakifanikiwa mnaanza ooh tuyamalize”

“La pili Vijana tuoe, Vijana sasa hivi tunaogopa kuoa, Wakina Mama na Wadada ni wengi kuliko sisi wewe unakaa gheto unajipilikisha, ushajua kukanda maandazi na chapati, unakaanga mpaka rosti kwanini huoi?”
TUOE ILI IWE NINI KWA MFANO?
TUOE ILI TUSAIDIWE KUPIKIWA ROSTI?
ACHA KILA MTU AKIMBIE MBIO ZAKE.

#KIJANA KATAA NDOA
 
Back
Top Bottom