Aliyewahi kufanya mchakato wa talaka msaada

Aliyewahi kufanya mchakato wa talaka msaada

Nawashukuru kwa ushauri wa kutia moyo
Kuna baadhi ya maswali nitayjibu.
1.kwa nini nahitaji talaka kabla ya kuondoka
Kwa sababu sina chochote cha kuanzia pesa zangu zote nimewkeza hapa ikiwemo makato ya mwez
2.sio mambo mepes yanayoniondoa mengine siwez andika hapa ni ya aibu mnoo.
3.bado nampenda sana mume wangu na ndo fimbo yake kubwa kwangu.anajua nampenda na hili ndo linanifanya hili swala liwe gumu sana kwangu ila sina namna

Msije kuuana humo ndani, walioshauri uondoke wana uzoefu. Talaka haiji kabla ya separation, mnatengana kwanza then mnaanza process za kuachana rasmi. Naogopa msije kugawana maeneo, mmoja kwa mola mwingine mjengoni.
 
Wale therapists wako wapi? Bongo rate ya talaka ipo so alarming.
 
Aibu ipi kubwa ya kusababisha talalaka!?
1. Kazaa nje ya ndoa!? Hili la kawaida.
2. Kazaa na mdogo wako au kambaka!? Hili labda.
3. Mlevi hadi anajikojolea na kujinyea mtaani au kitandani!? Hapana linarekebishika.
3. Hawajali ndugu,Wazazi wako!? Linarekebishika.
4. Hakujali,hana mda na wewe,Anakuona kama dada yake,hataki kufanya mapenzi na wewe!?? Labda hili.
5. Umemfumania mara nyingi na michepuko na habadiliki!? Hili pia gumu kuvumilika.
6. Anakubaka, anakuingilia kinyume na maumbile !? Hili pia zito..
7. Kafilisi miradi mliyoanzisha kwa kuwaonga malaya!? Hili pia gumu.
8. Hajali familia,hanunui chakula,havishi watoto,halipi ada!?
9. Ni mshirikina!? Mwizi!? Jambazi!?
10. Au ana KIBA MIA!!?

Aibu ipi,.. Em tueleze.
Anampenda sana ukute ndugu ndo wanamchomoa hapo
 
All i can is pole sana, manake umeandika very short kiasi kwamba ni ngumu kushauri mana hatujui sababu, ila process nazani zimeshaorodheshwa na umeshapata mwanga wa pakuanzia. Ila kama katika yote hayo kuna swala la kupigwa my dear pack ur bags ana leave rite now mengine yatafuatia ukiwa kwenu/kwako
 
Shoga angu aliwahi kunambia matatizo yake analia Lia kweli basi nikamshauri amua moyoni mwako kipi Bora kwake na ajifunze kufurahi bila ntu, kesho yake jamaa kakubembeleza acha anigeuzie kibao Mimi ni mubaya na sio huyo mwanaume, mafumbo ka yote eti hawaachani, nikasema langu jicho, Ila jamaa akaendeleza tabia mbovu Sasa hivi wameachana kabisa. Mwanamke haachani mtu mpaka ajeruiwe au auwawe aisee
Hahaha.....kabisa mkuu caritha

Kushauri wapendanao wanaolalaga uchi ni kazi kweli kweli

Unamshauri wewe umevaa ila mwenzioa anaongea nae akiwa uchi[emoji1][emoji1][emoji1]

Kwema lakini mkuu
 
Una mpendaje asiye kujali huyo kashakuharibu akili ndio maana huoni bila yeye you can't survive, kuwa makini jipe furaha mwenyewe kuwa busy na Mambo yako ukiendelea kujiliza gunia la mkaa linakuhusu.
Na Kama unampenda acha kuomba talaka vumilia mateso yake hafu wanaume hatukuumbiwa kupenda.
Yani wewe unavo mpenda kuliko yeye anaona kero ndo anadhidi kukuchukia zaidi,
Jaribu kukaa miezi kadhaa pekee yenu mjitafakari mnataka Nini hasa?
We ni mWanaume kumbe..!? Pumbavu kweli
 
Talaka ni ruhusa au amri ya mahakama ya kisheria ambayo mume au mke hupewa wakati anapomwacha mwenzi wake. Mahakama ndio chombo pekee chenye
mamlaka ya kutoa talaka.

Pole sana mkuu
WAKATOLIKI WANA TALAKA ZAO,
 
Pole sana Masai Dada. Nakumbuka ulileta hapa malalamiko yako kuhusu ndoa yako na watu wakakushauri. Imeshindikana kabisa? Pole sana.
Mawazo ushauri sababu nahisi nakufa soon.
Aliyewahi pitia hili swala naomba ushauri
 
Mawazo ushauri sababu nahisi nakufa soon.
Aliyewahi pitia hili swala naomba ushauri
Nenda baraza landoa kwaajili ya usuluhishi.
Mkishindwana utapewa barua kuhusu kushindwana.
Nenda kwa wakili wa kujitgemea na ufungue kesi, jua mchango wako wa mali kwenye ndoa yako, jua nani akae na watoto .
Anda vielelezo vikiwa na nakala halsi.
Anda mashahidi walau wawili[si lazma sana].
Muombe Mungu na usitoe rushwa kwa karani wala hakimu.
Mpende mtalaka wako iwapo mtafanikiwa kuachana, na baada ya hapo , biblia inasema "huruhusiwi tena kuolewa mpaka mwenza wako afe" na yeye haruhusiwi kuoa mpaka mewnza wake [wewe ] uf, vinginevyo itakuwa ni uzinzi tu.
 
Story za upande mmoja huwa mara nyingi ni za kutafuta huruma!

Ninachojua ndoa ina mambo mengi na wanandoa wana mengi!

Hakuna mtakatifu ndio maana kuvumiliana ni nguzo muhimu ya ndoa!

Kuyaleta maisha yako binafsi kuja kuamuliwa mtandaoni kunaonyesha kuwa haukupaswa hata kuwa kwenye ndoa!

Think big, take control of your destiny!
Umeongea point ambayo nilikuwa naitafuta, hata mimi huyu naona kabisa ni mwanamke ambae hajielewi na kwa kuzingatia misingi ya ndoa hakustahili kuepo kwenye ndoa.

Angalia alichoandika...
1. Mume anampenda.
2. Ndoa haitaki.
3.kinachomzuia kuondoka ni mali.

Huyu akipitia kwenye mabaraza ya usuluhishi hatafanikiwa.
 
Back
Top Bottom