Nawashukuru kwa ushauri wa kutia moyo
Kuna baadhi ya maswali nitayjibu.
1.kwa nini nahitaji talaka kabla ya kuondoka
Kwa sababu sina chochote cha kuanzia pesa zangu zote nimewkeza hapa ikiwemo makato ya mwez
2.sio mambo mepes yanayoniondoa mengine siwez andika hapa ni ya aibu mnoo.
3.bado nampenda sana mume wangu na ndo fimbo yake kubwa kwangu.anajua nampenda na hili ndo linanifanya hili swala liwe gumu sana kwangu ila sina namna
Pole rafiki, na hongera sikuwa najua kama ulishaolewa.
Kiukweli sijaona andishi lako la awali kwamba kipi hasa kinakufanya uhitaji talaka, hata hivyo ni wewe ndie muhusika mkuu unajua yanayokusibu humo
Lakini kubwa, umeangalia faida na hasara za nyie kutengana?
Umewaza jinsi mtoto atakosa malezi na upendo wa upande mmoja?
Umewaza jinsi utakavyopata sonona ya nafsi mara mtoto anapohitaji upendo wa baba au lah wewe utakapokwama kumuhudumia ikawa shida kwa mtoto?
Unajua kulea mbalimbali matatizo yake ikiwemo baadhi ya wanaume kususia kuhudumia?
Si kwamba nakwambia usihitaji talaka ila ni vema pia uangalie faida na hasara. Kama faida ya kupata talaka ni kubwa kuliko hasara basi endelea na mchakato.
Ikiwa kinyume chake , vumilia, hakuna ndoa rahisi, sio ndoa tu ila hakuna jamii inayocheka kila siku, maumivu yanatukomaza, ndoa wakati mwingine inahitaji mmoja ajifanye mjinga ili maisha yaendelee
Ndoa inahitaji kujitoa, ndoa ni kama vyombo vikichafuka vinaoshwa vinatumiwa tena hatuvitupi kwa kuwa ni vichafu.
Hivyo rafiki, tulia utafakari, na mwisho kabisa sisi tutashauri chochote tunachojisikia ila hayo ni maisha yako peke yako, sisi ukifanikiwa hatupo wala ukifeli hatupo, kazi yetu ni kusema pole na hongera baaasiii.
Nakutakia kila la kheir, na Mungu akusimamie ufanye maamuzi yaliyo sahihi kwa maisha yako na mwanao