Daniel Mbega
JF-Expert Member
- Mar 20, 2013
- 338
- 180
Ningefurahi zaidi kama hata sura ya huyo anayejiita 'aliyemtishia Nape bastola' ingeonekana hapa. Kwa teknolojia ilivyobamba, sidhani kama wabunge wote hao, akiwemo mwanahabari dada yangu Esther Bulaya, walishindwa hata kumfotoa ili walau watu waone sura yake na kuilinganisha na ile ya wakati uleee.Hili gazeti watakuwa ni wazushi tuu!, wanawezaje kumjua mtu aliyemtishia Nape bastola. ili hali ni mtu asiejulikana?!.
Japo mtu huyo alipigwa picha na video na sura yake kubainika wazi, lakini kwa mujibu wa vyombo husika, hawamjui mtu huyo. hivyo ni mtu asiyejulikana!, hawa Tanzania Daima watawezaje kumbaini mtu asiyejulikana wakati serikali yenyewe yenye mkono mrefu unafika kila mahali, wameshindwa kumpata?. Hawa Tanzania Saima watakuwa ni waongo hawa, wazushi tuu!, watajuaje?.
Nijuavyo mimi alyemtishia Nape bastola ni mtu asiyejulikana na mpaka sasa anatafutwa na vyombo vya sheria ili afikishwe mahakamani maana ni kosa la jinai, mtu kumtishia mtu bastola.
Hata waliomshambulia Tundu Lissu pia ni watu wasiojulikana na wanatafutwa!, kinachokwamisha kupatikana kwa watu hawa ni mtu pekee alyewashuhudia, amekataa kutoa ushirikiano kwa polisi ili wawakamate, hivyo mtu huyo anasubiriwa, akiishapatikana na kuelezea wakoje, ndipo uchunguzi wa kuwabaini uanze!.
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!.
P.
Kinachoonekana hapa ndugu zangu walisimuliwa, hawakuwepo kwenye tukio. Kimtazamo tu, angesimulia hapo mtu wa chama tawala kidogo ningeweza kusadiki japo kwa mbali, lakini kama jamaa zangu wamesimuliwa na wabunge wa upinzani wenye 'nasaba' na gazeti hilo, nachelea kuamini.
Hii habari ilifaa kuandikwa na 'magazeti pendwa' siyo TanzaniaDaima.
DM