Aliyekudhuru ndo akuhudumie?

Aliyekudhuru ndo akuhudumie?

1. Wenye akili wengi wanahisia kama hizo. Hisia hizo zinachochewa zaidi na kitendo cha dereva wake kufichwa kusikojulikana na umaarufu wake ndani ya chama hadi kuanzwa kufikiriwa kuja kuwa mgombea wa urais au uenyekiti wa chama chake. Hisia (siyo tuhuma) kama hizi haziwezi kuepukika kwa urahisi. Chadema wamfikishe dereva huyo polisi ili akasaidie uchunguzi ili kupunguza hisia hizi zisizokuwa na rutuba kwa chama hiki kikuu cha upinzani (opposition not confrontation party).

2. Namna shambulio lilivyopangwa na kutekelezwa ni dhahiri kabisa lilifanywa na wahuni wasiokuwa na weledi wo wote. Wahuni walioliokodiwa na mtu au kikundi cha watu na kupewa silaha hiyo nzito (SMG) ya kufanyia huo unyama huo. Haingii kichwani eti mijitu inaifuata gari ya target wao kwa nyuma mchana saa saba hadi kwenye compound ya nyumbani kwake, target wao akiwa ana park gari yake mijitu hii inateremka kutoka kwenye gari yao na kuanza ku burst shoot target yao 38 bullets at close range na kui miss hiyo target na kuambulia kuipiga miguu na makalio only!!! It doesn't make sense. Hawa lazima wawe ni wahuni tu wa mitaani wasio na ujuzi wa silaha. A trained soldier angali hit the head or heart of the target with just one bullet fired when overtaking the target's vehicle in speed and that bullet would have been fired from a pistol and not an SMG!

3. Mienendo ya kisiasa aliyokuwa akifanya Tundu Lissu lazima itakuwa imemujengea chuki ndani ya makundi kadhaa ya jamii ndani na nje ya nchi. Tumeshuhudia katika hii miaka ya karibuni jinsi makundi fulani ya kisiasa (huko nyuma tuliyaita wakereketwa) yamekuwa yakifanya siasa za chuki na mapambano ya nguvu hadi kujeruhi wenzao. Imefikia mtu au kikundi cha watu kikionekana mtaani kimevaa uniform ya cha cha kijani kinavamia na kupigwa na makamanda wa chama fulani. Ushabiki wa vyama vya kisiasa badala ya kuwa kama ule tuliouzoea wa Yanga na Simba, sasa umekuwa ni wa matusi na kushambuliana hadi wengine kuuawa, kutekwa nk. Makundi haya yamekuwa ni ya uhasama. Yaliyotokea huko Kibiti na hata haya yaliyompata Lissu yanaweza yakawa yamesababishwa na makundi haya ya wakereketwa wa siasa za uhasama na mapambano. Lissu mwenyewe alikuwa na bado anaendelea kuwa kinara wa siasa hizi za uhasama na mapambano. It is absolutely wrong to point any accussation finger to the government on what befell of Mr Lissu.
Kama wenye akili wengi nawe ni mmoja wapo basi hilo kundi la "wenye akili" hilo sio jina sahihi la kuwaita bali "wenye upumbavu" wengi.
Kama washambuliaji lilikuwa kundi la wahuni ilikuwaje waingie kwenye makazi ya viongozi bila hofu na walinzi wawe hawapo siku hiyo? CCTV ziko wapi na nani kazing'oa? Lazima uwe kwenye kundi hilo la "wenye upumbavu" wengi ndio huwezi kujiuliza maswali kama hayo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wapumbavu huwa hawaishi duniani naam wapumbavu kama mleta maada,

Hawa ni watu wa kwahurumia na kuwaombea kwasababu hata kutubu wana kawaida ya kutoona umuhimu wa kutubu.
 
Kukataa kumuhudumia ndiyo kumedhihirisha kuwa CCM na serikali yake ndiyo imemmiminia Lisu risasi 38 kwenye nyumba za serikali baada ya kuwashinda kwa hoja.

Hii political assassination ni mistake itakayomganda Pombe katika maisha yake yote.
Trump should come to our rescue


Sent from my HM NOTE 1LTEW using JamiiForums mobile app
 
..good points.

..sasa ongezea hoja za TL.

..Area D Dodoma aliposhambuliwa TL, getini na kwenye makazi kunalindwa na askari 24/7.

..siku ya tukio hawakuwepo.

..CCTV camera zimeondolewa.

..katika makundi yote uliyoyataja hapo juu nani anaweza kufanya shambulizi ktk mazingira hayo?

Jan.17.17.Cheering.On_.Magufuli-1024x724.jpg


Ukielewa maudhui ya hichi kibonzo cha mchoraji maarufu kutoka Kenya Bwana GADO basi utakuwa umepata jibu la swali lako...!!!!
 
Nitangulize maneno machache juu ya ujinga [ujinga siyo tusi] wangu juu ya nani alihusika na jaribio la kutaka kuondoa uhai wa Tundu Lissu. Mimi sijui kabisa nani alihusika. Lakini pia najua tofauti kati ya kujua, kuhisi, kudhani, na kusadiki. Wenye akili mtakuwa mmenipata, natumai.

Sasa bana, jana Mh. Lissu kaongea na waandishi wa habari huko Nairobi, Kenya, ambapo kimsingi kamtuhumu rais Magufuli na CCM kuhusika moja kwa moja na hilo jaribio la mauaji dhidi yake.

Upande wa serikali naona umeamua kuchukua ‘the high road’ kwa kukataa kulumbana na ‘mgonjwa’, kama ulivyosomeka ule ujumbe wa msemaji wa serikali. Nikiri tu kuwa ule ujumbe ulinichekesha sana. Ulikuwa mfupi na wenye kueleweka.

Sasa kwa vile Mh. Lissu kaamua kutoa tuhuma zake hadharani namna ile, he is now fair game!

Yeye na makamanda wenzake hawaeleweki. Hawaeleweki kwa sababu, kwa upande mmoja wanadai kuwa serikali, rais Magufuli, vyombo vya dola, na CCM ndo walihusuka na mpango mzima. Na kwa upande mwingine wanalialia kuwa eti mpaka sasa bunge halijampa haki zake, mara sijui polisi hawafanyi uchunguzi wa nani aliyetaka kumuua na blah blah zingine kama hizo.

Ni dhahiri kuwa Lissu anaingiza siasa kwenye hizo tuhuma na shutuma zake. Vivyo hivyo, huenda hata upande wa serikali nao umeamua kucheza siasa.

Now it’s on. Nasubiri tu siku Magu aje alizungumzie hilo suala. Makamanda mtalia na kusaga meno maana bwana yule mdomo wake hauna breki.

Nyie chekeleeni tu hivyo vijembe vya huyo kamanda wenu Lissu kwa sasa. Lakini siku Magu atayoamua kujibu mapigo mtatafutana.

Muwe na Jumamosi njema.

Nyabi Ngabu,

Acha unafiki na propaganda za ki-Ficcm..!! Anachosema Lissu ndicho wanachokiona hata watu wasio Wanachadema au Watanzania. Hichi ndicho wanachokiona watu wa dunia nzima siyo CHADEMA tu....!!
Kikaragosi cha Mr. GADO kinaonyesha mtazamo wa watu walioko nje ya Tanzania. Huyu ni Mswahili mwenzetu tu aliyeko Kenya. Je, vipi wenzetu walio na akili kuliko wewe ambao kila siku Serikali yako inaenda kutembeza BAKULI ili tupate misaada au waje wachimbe madini au makinikia, watengeneze minofu ya samaki halafu wakuachie MAPANKI....??



Aug-25-16-Magufuli-and-the-Opposition.jpg
 
OHHH KUMBE NDIYO MAANA SERIKALI HAIMHUDUMII? NIMEKUELEWA Nyani Ngabu NA UMEJICHAGULIA JINA ZURI MKUU, NAKUKUMBUKA SANA NI MIONGONI MWA WATU AMBAO WANAFURAHIA KUPIGWA KWA LISSU NA NINACHIAMINI HUWA UNAMWOMBEA AFE, SASA MKUU UTAKUFA WEWE YEYE ATABAKI,MUNGU SI ATHUMANI NA WALA SYO NYANI
 
Kukataa kumuhudumia ndiyo kumedhihirisha kuwa CCM na serikali yake ndiyo imemmiminia Lisu risasi 38 kwenye nyumba za serikali baada ya kuwashinda kwa hoja.

Hii political assassination ni mistake itakayomganda Pombe katika maisha yake yote.

hata wangemuhudumia, ingefuta hiyo dhana, just be honest at least this once
 
Nyabi Ngabu,

Acha unafiki na propaganda za ki-Ficcm..!! Anachosema Lissu ndicho wanachokiona hata watu wasio Wanachadema au Watanzania. Hichi ndicho wanachokiona watu wa dunia nzima siyo CHADEMA tu....!!
Kikaragosi cha Mr. GADO kinaonyesha mtazamo wa watu walioko nje ya Tanzania. Huyu ni Mswahili mwenzetu tu aliyeko Kenya. Je, vipi wenzetu walio na akili kuliko wewe ambao kila siku Serikali yako inaenda kutembeza BAKULI ili tupate misaada au waje wachimbe madini au makinikia, watengeneze minofu ya samaki halafu wakuachie MAPANKI....??



Aug-25-16-Magufuli-and-the-Opposition.jpg

haujaeleweka mkuu!!

unasema serikali ya magufuli inahusika, kisha unalalmika hawajakuhudumia na unataka wachunguze??

does that makes sense?? naona umeenda mbali sana

assumption ni kuwa serikali inahusika!!! sasa anacholalamika Lissu ni nini ??
 
Kwenye hili LISSU anakosea sana alitakiwa kuwa neutral kabsa na kuacha kupoint mtu direct eti ndio muhusika kwenye jaribio la kutaka kumuua...

kwanini nashauri alitakiwa kuwa NEUTRAL ni kwa sababu HATA HUKO CHADEMA hayupo salama kama adhaniavyo.....Aache kumwamini m/kiti wake wala Nyeupe......

Lissu nakushauri kuropoka jihadhari ADUI ZAKO una wajua vizuri....Na si MAGUFULI.....
Mpaka sasa hivi ni wewe ndio umeshikiria mustakabali wa MBOWE NA EL hapo chadema.....
kwa sasa Mh. Lissu nadhani ni 'mateka'. Hana uhuru huko aliko ukizingatia afya yake. Yupo tayari kusema chochote kwa matakwa ya wale walioamua ku'mtekea' huko Nairobi. Tusimlaumu Mh. Lissu, ni 'mateka' yule.
 
kwa sasa Mh. Lissu nadhani ni 'mateka'. Hana uhuru huko aliko ukizingatia afya yake. Yupo tayari kusema chochote kwa matakwa ya wale walioamua ku'mtekea' huko Nairobi. Tusimlaumu Mh. Lissu, ni 'mateka' yule.
ccm.jpg
 
  • Thanks
Reactions: BAK
haujaeleweka mkuu!!

unasema serikali ya magufuli inahusika, kisha unalalmika hawajakuhudumia na unataka wachunguze??

does that makes sense?? naona umeenda mbali sana

assumption ni kuwa serikali inahusika!!! sasa anacholalamika Lissu ni nini ??

Waberoya,
Wewe hujaelewa ndo maana unasema sieleweki...!!Kama hujanielewa utasemaje sieleweki..?
TL ana hoja ya msingi hapa.....na dhana au hoja anayojenga kuwa Serikali ya CCM/Magufuli inahusika ni mtiririko wa matukio baada ya kupigwa risasi na hawa watu wasiojulikana. Naomba unipe majibu ya maswala haya ili tupate picha:
  1. Kwanini Lissu kama Mbunge na Chief Whip hajapata stahili zake za matibabu na posho(upkeep yeye na msaidizi) wake akiwa Nairobi Hospital?
  2. Kwanini Bunge limekaa kimya kuhusu hayo malipo ambayo yake kisheria?
  3. Kwanini zile CCTV na Ulinzi wa masaa 24/7 haujaweza kusaidia kuwabaini hawa washambuliaji wa Lissu?
  4. Kwanini zile Camera za CCTV baadaye zimeng'olewa pale kwenye makazi ya Viongozi wa Serikali, nini kinaficchwa?
  5. Kwanini Spika wa Bunge hajaenda kumwona Lissu wala hajatuma mwakilishi wake kwenda Nairobi Hospital?
  6. Je, kwa akili zako unafikri kwa vile Tundu Lissu anakosoa Serikali basi asilalamikie kuhusu kuhudumiwa na Bunge ambalo ni wajibu wake kwa Wabunge bila kujali itikadi zao?
  7. Hivi kama Lissu angelikuwa ni Mbunge wa CCM angetendewa haya anayofanyiwa Lissu???
 
Wapumbavu huwa hawaishi duniani naam wapumbavu kama mleta maada,

Hawa ni watu wa kwahurumia na kuwaombea kwasababu hata kutubu wana kawaida ya kutoona umuhimu wa kutubu.

LWENYI,

Hawa watu wasiojulikana kwa upande mmoja na Wanajulikana kwa upande mwingine kama Mafisi wa Lumumba adhabu yao ni kwenye Ziwa la Moto liwekalo kama kiberiti. ASEMA BWANA MUNGU WA MAJESHI.....!!!

Acha wafurahie maumivu ya Wapinzani kwa kuwatesa, kuwafunga na hata kuwapiga risasi lakini ni swala la muda tu. Iko siku zao zitakapokoma hapa duniani ndipo watajua nini maana ya kumtesha au kumwua binadamu mwenzako....!!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
hata wangemuhudumia, ingefuta hiyo dhana, just be honest at least this once

..tunalaumu tulipoangukia badala ya kuangalia wapi tumejikwaa.

..siasa zetu zingekuwa safi na siyo za kukamiana na kuingiliwa na vyombo vya dola naamini kusingekuwa na kutuhumiana na kushutumiana baina ya TL na serekali.

..sasa kwa kuanzia, huku serekali ikiendelea kuwasaka watuhumiwa, labda serekali ingefanya yale ambayo yako ndani ya uwezo wake kwa sasa hivi.

..serekali ingeeleza hali ya ulinzi area D aliposhambuliwa TL. Taratibu za ulinzi zikoje na kwanini siku ya tukio kulikuwa hakuna ulinzi.

..pia tuelezwe kilichomo ktk cctv cameras. Watoe picha za watu wanaotafutwa na watangaze donge nono kwa atakayefanikisha kupatikana kwa wahusika wa shambulizi la TL.

..Lingine wampe mafao na stahiki zake kama wabunge wengine. Kama serekali ni waungwana sana kutojibizana na mgonjwa, kwanini wanamnyima mgonjwa haki zake ikiwemo posho?

..Je, hata kupewa posho zake kama mgonjwa ni lazima madaktari wa Muhimbili waidhinishe?

..Mimi nadhani serekali ingefanya hayo machache niliyoyaeleze lawama na shutuma zisingekuwepo kwa kiasi hiki tunachokishuhudia.

Cc Nyani Ngabu
 
Nitangulize maneno machache juu ya ujinga [ujinga siyo tusi] wangu juu ya nani alihusika na jaribio la kutaka kuondoa uhai wa Tundu Lissu. Mimi sijui kabisa nani alihusika. Lakini pia najua tofauti kati ya kujua, kuhisi, kudhani, na kusadiki. Wenye akili mtakuwa mmenipata, natumai.

Sasa bana, jana Mh. Lissu kaongea na waandishi wa habari huko Nairobi, Kenya, ambapo kimsingi kamtuhumu rais Magufuli na CCM kuhusika moja kwa moja na hilo jaribio la mauaji dhidi yake.

Upande wa serikali naona umeamua kuchukua ‘the high road’ kwa kukataa kulumbana na ‘mgonjwa’, kama ulivyosomeka ule ujumbe wa msemaji wa serikali. Nikiri tu kuwa ule ujumbe ulinichekesha sana. Ulikuwa mfupi na wenye kueleweka.

Sasa kwa vile Mh. Lissu kaamua kutoa tuhuma zake hadharani namna ile, he is now fair game!

Yeye na makamanda wenzake hawaeleweki. Hawaeleweki kwa sababu, kwa upande mmoja wanadai kuwa serikali, rais Magufuli, vyombo vya dola, na CCM ndo walihusuka na mpango mzima. Na kwa upande mwingine wanalialia kuwa eti mpaka sasa bunge halijampa haki zake, mara sijui polisi hawafanyi uchunguzi wa nani aliyetaka kumuua na blah blah zingine kama hizo.

Ni dhahiri kuwa Lissu anaingiza siasa kwenye hizo tuhuma na shutuma zake. Vivyo hivyo, huenda hata upande wa serikali nao umeamua kucheza siasa.

Now it’s on. Nasubiri tu siku Magu aje alizungumzie hilo suala. Makamanda mtalia na kusaga meno maana bwana yule mdomo wake hauna breki.

Nyie chekeleeni tu hivyo vijembe vya huyo kamanda wenu Lissu kwa sasa. Lakini siku Magu atayoamua kujibu mapigo mtatafutana.

Muwe na Jumamosi njema.
Mimi nadhani Tundu Lisu amekosa self awareness (hajitambui),namna nzuri ya kudeal na mtu asiyejitambua ni kumdharau,ni heri mungu akunyime vyoote lakini akikunyima hekma ujue uko katika mtihani mzito sana.
Kwa hakika maneno aliyoyasema "huyu bwana" tena akiwa nje ya nchi ni mazito na kwa maoni yangu serikali haipaswi kuyadharau kwa kuwa impact yake ni kubwa katika anga za kimataifa na tena yanahatarisha usalama wa Taifa.
Kitendo cha kurusha tuhuma nzito kama hizo kwa serikali na mbaya zaidi kwa Mh.Rais tena bila ushahidi hakitakiwi kuchukuliwa poa hata kidogo kwani hatujui kesho nani mwingine ataibukia wapi kuzusha nini na wangapi hawataamini uzushi huo.
Mimi nadhani kwa kuwa Tundu Lisu amekosa imani na Mh.Rais na serikali iliyo madarakani kuhusu usalama wa uhai wake,kwa kumsaidia ilitakiwa asiruhusiwe tenakukanyaga ardhi ya TZ,hili ni muhimu kutokana na kwamba atakaporejea nchini na kupatwa na jambo lolote baya itakuwa ni rahisi kwa watu kuamini kwamba serikali inahusika na kimsingi hatujui bwana huyu ana maadui wangapi na wanawezaje ku-take advantage ya huku kuropoka kwake kuweza "kufanya yao"ili hatimaye ionekane ni serikali yetu tukufu.
Kiukweli kama ningepata nafasi ya kumshauri jambo Rais wetu mpendwa Dr JPM ningemshauri atoe tamko la kumzuia bwana huyu kukanyaga ardhi ya Bongo ili aendelee kukaa huko anakoona kuna serikali zenye usalama kwa maisha yake, HAIWEZEKANI UPANDE JUU YA NYUMBA KUUTANGAZIA UMA KUWA BABA MWENYE NYUMBA SI SALAMA KWAKO HALAFU UNASHUKA NA KUGONGA MLANGO ILI BABA MWENYE NYUMBA AKUFUNGULIE MLANGO UINGIE NDANI KULALA.
 
Nitangulize maneno machache juu ya ujinga [ujinga siyo tusi] wangu juu ya nani alihusika na jaribio la kutaka kuondoa uhai wa Tundu Lissu. Mimi sijui kabisa nani alihusika. Lakini pia najua tofauti kati ya kujua, kuhisi, kudhani, na kusadiki. Wenye akili mtakuwa mmenipata, natumai.

Sasa bana, jana Mh. Lissu kaongea na waandishi wa habari huko Nairobi, Kenya, ambapo kimsingi kamtuhumu rais Magufuli na CCM kuhusika moja kwa moja na hilo jaribio la mauaji dhidi yake.

Upande wa serikali naona umeamua kuchukua ‘the high road’ kwa kukataa kulumbana na ‘mgonjwa’, kama ulivyosomeka ule ujumbe wa msemaji wa serikali. Nikiri tu kuwa ule ujumbe ulinichekesha sana. Ulikuwa mfupi na wenye kueleweka.

Sasa kwa vile Mh. Lissu kaamua kutoa tuhuma zake hadharani namna ile, he is now fair game!

Yeye na makamanda wenzake hawaeleweki. Hawaeleweki kwa sababu, kwa upande mmoja wanadai kuwa serikali, rais Magufuli, vyombo vya dola, na CCM ndo walihusuka na mpango mzima. Na kwa upande mwingine wanalialia kuwa eti mpaka sasa bunge halijampa haki zake, mara sijui polisi hawafanyi uchunguzi wa nani aliyetaka kumuua na blah blah zingine kama hizo.

Ni dhahiri kuwa Lissu anaingiza siasa kwenye hizo tuhuma na shutuma zake. Vivyo hivyo, huenda hata upande wa serikali nao umeamua kucheza siasa.

Now it’s on. Nasubiri tu siku Magu aje alizungumzie hilo suala. Makamanda mtalia na kusaga meno maana bwana yule mdomo wake hauna breki.

Nyie chekeleeni tu hivyo vijembe vya huyo kamanda wenu Lissu kwa sasa. Lakini siku Magu atayoamua kujibu mapigo mtatafutana.

Muwe na Jumamosi njema.
Tofauti ya wenzetu nchi xulizoendelea na sisi tunaosemekana nchi zinazoendelea (au ulimwengu wa tatu) ni jinsi tinavyojali maisha ya wengine. Sisi hatujali kumwaga damu za watu wetu na wala hatujali hata kutafuta sababu nini kimetokea mwrnzetu akafa. Wenzetu ikitokea wanafanya kila liwezekanalo kulizuia na kutafuta chanzo. Sijajua kwa nini hii issue ya Bw Lissu imekuwa hivi!
 
Back
Top Bottom