huu upuuzi peleka Lumumba mvaa hirizi weweWenye akili nyingi huwa hawafikiri in a simple way kama ulivyofanya. They think in a complex way wakiangalia all possible circumstances. Kwa mfano:
1. Saa hizo wabunge wengi walikuwa wanarejea kwenye eneo hilo walilopanga kwenda kupata chakula cha mchana kwenye nyumba zao. Eneo lina nyumba nyingi ila geti la kuingilia eneo hilo ni moja likiwa na mlinzi mmoja (armed or unarmed). Magari yaliyobeba hao waheshimiwa yanaingia kila baada ya muda wa dakika tano au kumi. Gari la Mh Lissu linakuja likiwa limeongozana na gari la waheshimiwa wengine (Nissan nyeupe). Kwa mazoea yetu waheshimiwa hawa wabunge na wengine huwa hawapendi mlinzi wa geti asimamishe magari yao getini na kuanza kukagua waliomo ndani na kuwahoji wao ni akina nani. Kwetu tendo hilo la kudodosa waheshimiwa ni ukosefu wa nidhamu kwa mlinzi mwenye tabia kama hiyo. Kwetu nidhamu ya mlinzi ni kufungua geti mara moja anapoona gari la mheshimiwa linapokuja ili mheshimiwa na alioambatana nao waweze kuingia bila bughudha ya kufanyiwa thorough search! Ndivyo watanaznia tulivyo, tumelemazwa na amani. Kwa kutumia mwanya huo 'waheshimiwa' waliokuwa kwenye shangingi nyeupe iliyoongozana na shangingi nyeusi ya Mh Lisu waliingia kwa pamoja ndani ya eneo hilo na kusimamisha magari yao. Then in seconds mmoja wa waliokuwemo kwenye lile gari jeupe alitoka na kuanza ku spray bullets from a heavy automatic gun!! Wenye akili wanaona scnerio ilivyokuwa kihalisia na reaction ya huyo au hao walinzi wa geti la waheshimiwa kama alikuwa au walikuwa karibu na risasi zilipokuwa zinamiminwa. Reflex reaction kwa askari yo yote kwenye such a situation ni kulala chini and craw fast to a nearet cover to save his life. Hayo mambo yalitokea in seconds na hao assillants kutokomea, geti likiwa bado liko wazi na magari mengine ya waheshimiwa wabunge hayajafika kwenye eneo hilo kuja kupata chakula cha mchana.
Ni ujinga kuamini kuwa walinzi waliokuwapo eneo hilo la geti na sehemu zingine hawakuhojiwa na polisi. Pia ni upumbafu kufikiri kuwa mlinzi au walinzi waliokuwepo getini wangaliweza kujibu mapigo hayo ya risasi. Vita ya risasi si lelemama, adui yako akikuwahi unachoweza kufanya kama una bahati ni ku take cover. Pia ni ujinga kuamini kuwa kwa sababu eneo hilo linalindwa na askari basi ni salama kwa asilimia 100%. Hata kambi za jeshi na vituo vya polisi vimewahi kumiminiwa risasi na askari kuuawa mara nyingi tu, sasa sembuse hilo eneo na kwa mazingira yetu kama hayo.
Pia ni upumbafu kuamini kuwa uwepo wa CCTV kwenye eneo hilo ndiyo solution ya kuwezesha kuonekana sura za wahalifu hao. Even the most expensive high quality high definition external rotating CCTV cameras hazina uwezo wa kutoa clear images at all 360 degrees anytime and at all distances from object. When the object is more than 3m from camera huwezi pata clear images za kuweza kutambua sura za hao wahalifu. Wenye akili wanajua kwamba the effectiveness as a security tool kwa kunasa sura za wahalifu wa aina hii is almost zero. Tumeshudia huko ulaya magaidi yanavyamia na kushambulia kwa risasi kumbi za burudani na kuua watu, cctvs zao hazikuwa na msaada wa maana katika kuwatambua wahalifu hao. Hapa kwetu ambapo tulizoea madili hiyo kampuni iliyolipwa mabillion kufunga hizo CCTV kwenye eneo hilo la serikali si ajabu kuwa quality ya hizo cameras zilizofungwa ni za quality ya lugumi, hivyo aidha no images or just blurred images.
Isitoshe siku hizi ili kukwepa kuonekana sura zao kwenye ma cctv au kwa watu wengine, wahalifu wa aina hii huvaa masks au miwani myeusi + kofia zilizoshushwa chini kuficha sura zao. Mtu pekee anayejua sura za assaillants hawa pamoja na gari yao ni dereva wa Lissu. Yeye kwa maneno yake alishasema hata kabla ya hitimisho la tukio kwamba ameshawaona mara nyingi tu kuanzia Dar. Wameshawahi hata kukaa kwenye bustani moja ya hoteli fulani huko Dar na wahalifu hao wakiwa kwenye mishe mishe hiyo ya kutaka kumzuru Lissu. Bahati nzuri siku hiyo wakaweza kuwakwepa watu hao na wakatoa majigambo kwenye vyombo vya habari kwa mafanikio hayo.
Dreva wa Lissu anawafahamu vizuri sana watu hao kwa sura na hata namba ya gari lao analijua (ingawa inaweza kuwa feki). Hata walipokuwa wameficha sura zao kwa kofia pale kwenye eneo la tukio aliweza kuwatambua kuwa ni wale wale.
Sasa watu wenye akili inawawia ngumu kuelewa hicho kigugumizi cha huyo dereva kugoma kwenda kuisaidia polisi katika uchunguzi wa hilo tukio sababu yake ni nini haswa? Dereva amefichwa, huko Nairobi haonekani na huku kwetu haonekani. Mke na watoto wake ha2amuoni. Tuelewe nini sasa? Jee naye katekwa na kama katekwa ni nani huyo kamteka kama siyo chama chake. Tunaambiwa eti atasaidia tu jeshi la scotland yard la uingereza au la FBI la amerika lakini siyo jeshi hili la Siro katika uchunguzi wa tukio hili! Ni shida bin shida. Ni siasa za kupambana na serikali iliyowekwa kihalali na watanzania walio wengi!