Alichokisema Lissu juu ya kesi ya Wema

Alichokisema Lissu juu ya kesi ya Wema

Ameandika wakili msomi Tundu lissu

Sio msokoto wa bangi. Hati ya mashtaka dhidi yake inasema Wema amekutwa na gramu 1.08 za bangi. Gramu, sio kilogramu. Polisi waliokamata 'madawa hayo ya kulevya' walifanya sachi saa tatu usiku.

Sheria inayohusu sachi inasema sachi inatakiwa kufanyika kati ya saa moja asubuhi na saa 12 jioni ili, obviously, kupunguza uwezekano wa polisi kupandikiza ushahidi.

Tunamsubiri Paul Makonda mahakamani aje atoe ushahidi wa namna alivyojua Wema anatumia madawa ya kulevya mpaka akamtaja hadharani. Asipokuja basi kesi hakuna.
Lissu Mungu anakuona [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Lissu bana


Ila kina Lissu nao wana maswalii duuu

Lissu:Umesoma

Shahidi:Ndio

Lissu: Una uelewa wa kidogo wa mambo ya sheria?

Shahidi: Mi hayo mambo ya sheria za mahakamani sijui,maana nilisoma Physics

Lissu: Hata Newton's Law of Motion si sheria pia?Nayo huijui!?

Shahidi: Najua...Zipo kama tatu

Lissu :Ok ok...Sasa unaweza kutuambia why the last drop of urine doesn't obey
the law of gravity unless u shake it
well!!

Shahidi:Mimi hiyo sikuisoma

Lissu:Sasa kitu ulichosema unakifahamu,sasa unasema hujui,sasa huoni hata huo ushahidi unaosema ulikuwepo hapa unaweza kuwa unaongea kitu usichokijua?

Shahidi:Sijui

C n P
Aisee hii ilitokea wapi?, dah huyu Lissu ni nyoko
 
Haujawahi kuwa na ndugu aliyebambikwa kesi na polisi wa Tanzania ?
Katika hilo hautumii nia ovu ya kuyumbusha mahakama kwa kutumia 'teknikalitizi chakachuzi'. Unajenga hoja kuonyesha uhalisia kuwa 'mteja wangu' amebambikiwa kesi. Sijasema mtu adhulumiwe haki yake, la hasha. Nina himiza haki ndiyo pekee itumike kutoa hukumu, si masuala ya uwasilishwaji wa mashtaka ndiyo yatumike kutoa haki.
 
Ni rahisi kupandikiza ushahidi ukizingatia udogo wa kidhibiti na muda (usiku) usio kubalika kisheria.
Wanapaswa waweke ulinzi hamna mtu wa kuingia wala kutoka. Thn ikifika saa 12 waanze kazi. Kama ni mtuhumiwa wa ujambazi hiyo ni case nyingine.
 
Police ina mipaka ya kulinda na kusimamia utii kwa wananchi kwa masaa?kituo cha police na kazi zao muda fulani kama office zingine hufungwa?
Hakika unachokitetea hukijui....

Kwenye Criminal Procedure Act, yametolewa maelekezo ni muda gani mtuhumiwa anapaswa kufanyiwa search.

Kisheria kama search hiyo imefanyika nje ya muda huo, maana yake ni kuwa search hiyo ni batili na kwa maana hiyo Jaji/Hakimu anaweza kuitupa kesi hiyo.....
 
Unaonekana bila mashaka yoyote kuwa wewe kwenye fani ya sheria ni " layman" ndio maana unaamini kila utumbo anoasema jamaa huyu
Mbona unakoboa pumba badala ya mahindi.
Definitely "layman" anajulikana kwamba ni mtu hasiye na uelewa wa sheria, yes sikatai kwamba naweza "kuonekana" hivyo.
Ila sasa wewe ambaye ni "Lawyer" probably a "mwanasheria pori" (bush lawyer) nilitegemea ungekuja walau na vifungu husika katika kupinga hoja husika ili sisi ma layman tuelewe, umeishia kuja na sandarusi za majina ya sheria.
 
Bashite mimi sio size yako... Mi nacheza na Sizonje we size yako akina Tunda pita hivi....
Kila la kheri na dhiaka zako kwa jina la yule aliyekuumba. Hata enzi za Gharika au Sodoma na Gomora kuna watu walionywa kwa tabia zako wakafanya kiburi na dharau kama wewe.
 
Andika kiswahili tu ili ueleweke mana unaonesha ulivyo mweupe kwa kichwa
Mweupe imekugusa hyo.tulia iingie acha ujinga kushabikia shabikia mambo ..tulia tafakari ndio uje hapa,ficha ujinga wako
 
Ombi langu kila siku kwa Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo ni kwamba; baba Mungu mimi nilishindwa kusoma kama Tundu Lisu lakini nakuomba mwanangu asome kama yeye. Baba ninaomba na kuamini Amina. Nitaendesha hii bodaboda mchana kutwa nitafute ada na naamini ataenda tu hata huko Marekani ili ajue sheria kwa undani
 
Kila la kheri na dhiaka zako na jina la yule aliyekuumba. Hata enzi za Gharika au Sodoma na Gomora kuna watu walionywa kwa tabia zako wakafanya kiburi na dharau kama wewe.
Mbona hata wewe una kiburi? Dhambi zote umebeba wewe... Narudia huwezi kumnywesha Mungu uji.....

Kwanza sijadiliani na vilazer... Mtu mwenyewe hata cheti cha form four huna!!
 
Back
Top Bottom