blogger
JF-Expert Member
- Mar 13, 2012
- 13,378
- 16,694
kwenye swala la video hawa ndorobo niachieni mimi nitawapa elimu ya bure.
Kwanza naomba niwahakikishie kitu kimoja, nawajuwa vizuri wasouth africa wao huwa wanapenda vyao tu na vijana wa kisasa na waliokwenda shule wanapenda umarekani kwa sababu wanaamini ni marekani tu ndio imeizidi south africa. Si ajabu ukienda sinema theather kijana wa kisouth africa akakuuliza hii movie imetengenezwa cape town? Unajuwa ni kwa nini? Wao wenyewe wanashindwa kutofautisha muonekano wa nchi yao na ulaya au marekani na wengi wao hawatembei na wala hawaijui kabisa nchi yao.
Mandhari ya video ya kiba itapata viewers wengi wasouth africa kwa sababu ya mandhari ya video na ile gari nyekundu iliyotumika ndio kama icon ya wasouth africa zile gari zinaitwa caravele ni gari ghari sana na wezi wa magari wanazitarget sana maana ndio daladala za kwenye location za weusi hasa south and west townships (soweto).
Kuna vitu mimi binafsi kwa maoni yangu vinahitaji exposure zaidi kuvijuwa otherwise mtu atakuwa anabwabwaja tu.
Nota bene: South africa inashika nafasi ya tatu kidunia kwenye film industry, hollywood ikiwa ndio kinara na ndio gharama zao ziko chini ndio maana si ajabu leo movie kufanyika ulaya lakini makampuni yakachukuliwa south africa maana ni same quality kwa pesa ndogo kuliko gharama za hollywood.
aiache hukokuko soweto sasa.., anaanza kutukumbusha movie za sarafina leo.
Kama aliwatageti wale mahouse grls na vibaka wanaoonekana hvyo ktk video its well and good. Awapelekee hyo video sasa.