Albadir iliyosomwa Tanga

Albadir iliyosomwa Tanga

Anasema hilo shoga pichani hapo juu albadir waliyosomewa wezi wa nazi huko tanga na yeye imemkuta.HUyu yeye hakuiba nazi isipokuwa utotoni alijipikilisha kwenye kifuu cha moja ya nazi zilizoibiwa .
duuu
 
The usual stuff. Halafu maalim seif atalalamika serikali imekodi wachawi kumuua, serious!!?
 
Mshana Jr Mimi sio muislam ila hivi vitu ni common sana kwa wale wanaotoka sehemu zenye Muslim wengi si kitu cha kushangaa
Kwetu kule kondoa kunavijana waliiba mazulia ya msikitini kikapigwa hicho kinachoitwa kisomo mkuu watu walioza kabla hawajafa nikasema kwa kweli hii kitu hii ni hatari
Mkuu we acha tu jirani na msikiti kuna kijana kafungua Saloon sasa akaweka mziki mkubwa km unavyojuaga saloon nyingi za kiume kuna tabia hii.
Basi wazee wa msikiti wakamfuata na kumweleza asiwashe mziki hayo maeneo anawaharibia watu Ibada kijana hakusikia na kejeli kibao akatoa wale wazee wakakaa chini wakapiga kisomo kesho yake kikajipa mziki ukaungua.
Aisee heshimu sana hv vitu
 
Haijulikana nani na nani hasa aliyeshiriki katika hilo tukio la kutaka kumuuwa TL na ndiyo kikasomwa hicho kisomo,ila ajabu imekuwa kwamba hata wakijamba watu wawili kwa pamoja basi tunachagua mmoja na kumuhusisha na hicho kisomo kwa kujamba kwake na yule mwengine tunasema kapumua tu ni hali ya kawaida.


Mwisho wa siku isije ikawa hicho kisomo kimetuathiri sie wenyewe bila kujua kama vile chizi anavyoona watu wengine hawana akili kumbe yeye ndiyo chizi.
 
albadir inaanza kupenya - taratibu tu watatajana kina mmoja kwa namna yake!! wacha nivute kigoda changu, niwashe mtemba wangu maana movi linakaribia kuanza, ni suala la muda tu.

Wazee wa Tanga.....mpoo....?? Majibu yanaanza huku.
 
Ndugu Mshana nadhan umeandika machache sana kati ya mengi, kwani ukichunguza kwa umakini na jicho la tatu utaelewa vyema kipi ndugu mtoa mada hajaviandika.

Anza tu kwa kutafakari, mfano wanayoyakataza na kuyakemea ndio ndio wayatendayo tena mbele za umma,,,,,, waliyoyaahidi na kuigamba kuyaweza et leo wanayakana hadharani.

Nb: Sikijui wala sikifahamu icho kisomo,,,,,,, ila mwenye macho haambiwi ona, seriously ukiwatazama vizuri pychologically asieeeeeee they are not happy, dhamira zao zinawasuta, hawajiamini tena, wanasifia visivyostahili katika jamii, muda si mrefu nao watakuwa wanalalamika tu kama wale.
 
Mshana eeeeeeh
Unataka niandike humu utanipa tuzo ya kuandika JF ha ha haaaaa tena ndio nazidi kufurahia mnaninoti jamani hadi raha tupuuuu

Uandishi wangu wa humu ndani ni kama kawa eeeeh na bado

Hata mkinisema najua mnapenda kuyasoma yangu na ndio Cocochanel..

Eti goma ha ha haaaaaaa pita hukoooooooo

Jerry mlitaka kumtenda mkashindwa!!! Nondo zake mnajua ni bombaaaaa.. humu watu wakishusha nondo mnawaita majina ya ajabu kama vile hawana akili ila tumewazoea.
 
Mshana kuna wakati huwa natamani japo kujua umri wako. Anyway,umri wa mtu ni siri yake hadi atakapoamua kuweka wazi.

Hongera mkuu kwa busara zako.
 
Nimependa namna ulivyofikisha ujumbe wako, umetumia vyema kiswahili pamoja na alama za uandishi.
Hongera sana mkuu.
 

Mshana, na Mama yake yule Sheikh alosoma akamwambia yule Sheikh, UKIRUDIA KUSOMA TENA HLUL BADRI KAMA HII SIKO RADHI NA WEWE DUNIANI NA AKHERA! nilisikia wakati nipo mdogo! Dhulma ni mbaya na Duaa ya Mdhulumiwa kwa Mwenye ez Mungu HAINA PAZIA! bila hata Ahlul Badri, Mwenye ez Mugu hapendi watu madhaalim
 
Mshana, na Mama yake yule Sheikh alosoma akamwambia yule Sheikh, UKIRUDIA KUSOMA TENA HLUL BADRI KAMA HII SIKO RADHI NA WEWE DUNIANI NA AKHERA! nilisikia wakati nipo mdogo! Dhulma ni mbaya na Duaa ya Mdhulumiwa kwa Mwenye ez Mungu HAINA PAZIA! bila hata Ahlul Badri, Mwenye ez Mugu hapendi watu madhaalim
Pia mwenyezi mungu hapendi tuwekeane dhana mbaya,kumdhania mtu kuwa anahusika na jambo baya sidhani kama ni vitu ambavyo mungu anavifurahia.
 
Back
Top Bottom